Qurayh ni jina la kabila la Mtume Muhammad S.A.W. Sura hii itakwenda kukujulisha neema ambazo Maquraysh wamepewa na hawataoewa wao wowote baada ya wao.
SURAT AL-QURAYSH
Sura hii ina majina mawili. Inaitwa Qureish na pia inaitwa Li ii laafi. Ibni Abbas anasimulia ya kuwa ilishuka Makka. Qureish ni jina la kabila lililotoka kwa Nadhir bin Kinana (Razi).
Wengine wanasema neno Qureish limetoka katika neno Qarsh ambalo ni jina la samaki mkubwa wa bahari anayekula samaki lakini yeye haliwi. Hivyo kwa ukubwa wa kabila lao na kwa kuheshimiwa na watu wote nao wakaitwa Kureish. Makureish walikuwa watu wa Makka na walinzi wa Kaaba, na kwa sababu ya kuilinda Kaaba waliheshimiwa sana.
Sura hii imeshuka kwa maqurayshi kama alivyosema Mtume (s.a.w) “Allah amewapa neema Maquraysh ambayo hajampa yeyote kabla yao na hatampa yeyote baada yao:
Ukhalifa umepewa mtu katika wao, uangalizi wa nyumba tukufu ya Allah umepewa mtu miongoni mwao, kazi ya kuwapa maji mahujaji imepewa mtu katika wao, utume umepewa mtu katika wao, wamepewa ushindi dhidi ya jeshi la tembo, walimuabudu Allah kwa miaka saba ambapo hakuna yeyote aliyekuwa akimuabudu Allah, na sura kwenye quran imeshushwa kwa ajili yao na hakuna yeyote aliyetajwa kwenye surahiyo ila wao (kwa kupewa jina la al-quraysh)
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Mada zipo katika makundi mawili ambayo ni madda far-iy na mdada twab-iy.
Soma Zaidi...Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Maulamaa katika elimu ya Quran wametofautiana juu ya aya ya mwisho kushuka. Hata hivyo hapa nitakutajia ambayo imependekezwa zaidi
Soma Zaidi...Hapa utajifunza maana ya Tajwid kilugha na kisheria. Pia nitakujuza jukumu ya kusoma tajwid.
Soma Zaidi...SURAT AL-QURAYSH Sura hii ina majina mawili.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukuorodheshea aina saba za viraka vya usomaji wa Quran.
Soma Zaidi...Sura hii inaonya vikali tabia ya kusengenya na kusambaza habari za uongo. Wameonywa vikali wenye tabia ya kujisifu kwa mali, kukusanya mali bila ya kuitolea zaka.
Soma Zaidi...