picha

Kutokea Kweli Matukio yaliyotabiriwa katika Qur-an

Kutokea Kweli Matukio yaliyotabiriwa katika Qur-an

(vi)Kutokea Kweli Matukio yaliyotabiriwa katika Qur-an:



Ushahidi mwingine unaonesha kuwa Qur-an ni neno la Allah (s.w) ni kutokea mambo kama yalivyotabiriwa hapo awali na Qur-an. Katika mwanzo wa kushuka Qur-an kuna mambo mbali mbali ambayo Mtume (s.a.w) aliahidiwa pamoja na Waislamu kuwa yatatokea hapo baadaye. Pamoja na kuonekana kwa watu kutokuwa na uwezekano kutokea hayo yaliyotabiriwa kulingana na hali halisi iliyokuwapo wakati huo ukweli ni kwamba yalitokea. Kwa mfano, katika siku za mwanzo za Utume, Mtume (s.a.w) na Waislamu waliahidiwa na Allah (s.w) kuwa pamoja na ugumu uliokuwa ukiwakabili na pamoja na udhaifu wa mali na uwezo waliokuwa nao, hali yao itazidi kuwa nzuri siku hadi siku na baadaye watafarijika na kuwa juu ya maadui zao. Ahadi hizi tunazikuta katika aya zifuatazo:


Na bila shaka wakati ujao utakuwa ni bora kwako kuliko uliotangulia,na Mola wako atakupa mpaka uridhike. (93:4-5)


Na kwa hakika baada ya dhiki (huja) faraja. Hakika baada ya dhiki (huja) faraja. (94:5-6)
Tukiangalia maisha ya Mtume na maswahaba wake, ahadi zote hizi zilitimia. Waislamu waliongezeka siku hadi siku na Uislamu ulisimama na kuwa juu ya Dini zote (njia zote za maisha) katika kipindi kifupi cha miaka 23 tu.Mfano wa pili wa utabiri wa Qur-an uliotokea kweli baada ya kipindi kifupi tu ni ule uliotolewa katika suratur-Ruum katika aya zifuatazo:



Warumi wameshindwa katika nchi iliyo karibu (na nchi ya Bara Arabu, nayo ni Sham) nao baada ya kushindwa kwao watashinda, katika miaka michache: Amri hii ni ya Allah kabla (yake) na baada (yake) na siku hiyo Waislamu watafurahi kwa nusra ya Allah (Atakayowapa wao. Nayo ni kuwashinda Makuraishi siku hiyo) (Allah) Humnusuru amtakaye; naye ni Mwenye Nguvu; Mwenye Rehma. Hii ni ahadi ya Allah, Allah havunji ahadi yake lakini watu wengi hawajui. (30:2-6)



Katika mwaka wa sita au saba wa Utume, palikuja habari Makka kuwa Warumi ambao ni watu wa Kitabu (Ahlal-Kitab) wameshindwa vita na Waajemi ambao walikuwa ni washirikina kama washirikina wa Makka. Tukio hili liliwafurahisha sana washirikina wa Makka na kuwaambia Waislamu: "Wakristo, watu wa Kitabu kama nyinyi, wameshindwa na washirikina wenzetu, na hii ni ishara kuwa na sisi hivi karibuni tutakushindeni." Ndipo Qur-an ikatangaza katika aya hizi bishara mbili; bishara ya kwanza ni kuwa katika muda wa miaka tisa Waajemi watashindwa na Warumi na ya pili ni kuwa Waislamu siku hiyo nao watafurahi na kuwacheka Washirikina wa Makka, yaani makafiri wa Makka nao watashindwa vibaya sana na Waislamu. Hivi ndivyo ilivyotokea, kwani katika mwaka 624 A.D. Warumi waliwashinda Waajemi na mwaka huo huo Waislamu 313 walishinda jeshi la makafiri wa Makka lililokuwa na askari 1000 katika vita vya Badr, kwa hiyo ahadi ya Allah(s.w) aliyoitoa katika Qur-an ilitimia. Je hii haithibitishi kuwa Qur-an ni maneno ya Allah (s.w), Mjuzi wa yote yaliyopita na yajayo?



Hebu tuangalia tena mfano mwingine unaoonesha kutokea kweli ahadi alizozitangaza Allah(s.w) katika Qur-an. Katika suratul-Fat-h tunafahamishwa:


Bila shaka Tumekwisha kupa kushinda kuliko dhahiri. (48:1)
Katika mwaka wa 6 A.H. Mtume (s.a.w) na baadhi ya Maswahaba wake walitoka kwenda Makka kufanya Umra (Hija ndogo) lakini walipokaribia kuingia Makka makafiri waliwakatalia kata kata wasiende kufanya ibada hiyo.



Waislamu walikasirika sana mpaka kukaribia kupigana ndipo Allah (s.w) akawateremshia utulivu na wakakubaliana kufanya mkataba wa (Hudaibiya), kisha Allah (s.w) akawaahidi kupata ushindi baada ya muda mfupi. Ndivyo ilivyotokea.



Baada ya miaka miwili tu, na baada ya makafiri wenyewe kuvunja ule mkataba wa amani, Waislamu waliuteka mji wa Makka na kuwa mwisho wa kuabudiwa miungu mingine pamoja na Allah(s.w) katika Nyumba Takatifu (Al-Kaaba) na katika muda mfupi huo watu wengi walisilimu. Je, kutimia kwa bishara hii ambayo iko wazi mno katika historia, haioneshi kuwa haikutolewa na yeyote ila ni yule mwenye elimu ya hakika juu ya yote yaliyopita na yajayo?




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 1665

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 ai web app    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Qur-an Yenyewe Inajieleza kuwa ni Ufunuo Kutoka kwa Allah (s.w)

(ii)Qur-an Yenyewe Inajieleza kuwa ni Ufunuo Kutoka kwa Allah (s.

Soma Zaidi...
As-Sab nuzul

Sababu za kuteremshwa baadhi ya sura Katika darsa hii tutaangalia sababu za kushuka kwa aya na sura ndani ya quran.

Soma Zaidi...
Fadhila za kusoma Quran na umuhimu wa kusoma Quran

Unazijua faida za kusoma Quran, na je ni faida gani utapata ukisoma Quran?

Soma Zaidi...
Hukumu ya tafkhim na tarqiq katika usomaji wa Quran tajwid

Tarqiq ni kuisoma herufi kwa kuipa wepesi na tqfkhim ni kuisoma herufi kwa kuipa uzito.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka kwa Surat Al-Asr

Surat Al-Asri imeteremshwa Makka, na hapa utazujuwa sababu za kushuka kwa sura hii

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al adiyat

Sura hii iliposhuka ilikuwa kama imekuja kuwasuta Wanafiki waliokuwa wakizungumzahabari za uongo kuhusu jeshi alilolituma Mtume wa Allah.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al alaqa

Asbsb nuzul surat al alaqa, sababu za kushuka surat alaqa. Sura hii imeshuka Makka na ina aya 19. Ni sura ya 96 katika mpangilio wa Quran.

Soma Zaidi...
Maana ya qalqala na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid

Qalqala imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Qalqalatul qubra yaani qalqala kubwa na qalqalat as shughura yaani qalqala ndogo.

Soma Zaidi...