image

Mtume hakufundishwa quran na Jabir na Yasir

Mtume hakufundishwa quran na Jabir na Yasir

(c)Dai la Kufundishwa na Jabir na Yasir:



Makafiri wengine wanadai kuwa Mtume (s.a.w) alifundishwa na Jabir na Yasir waliokuwa watumwa kutoka Ethiopia (Uhabeshi) na wakasilimu mbele ya Mtume (s.a.w). Wanadai hivyo kwa kuwa bwana wao aliyekuwa akiwatesa sana kwa sababu ya kusilimu kwao alikuwa akiwapiga sana na kuwaambia: "Mnamfundisha Muhammad?" na walikuwa wakijibu "Kwa jina la Allah hatumfundishi bali ndiye anayetufundisha na kutuongoza".



Bila ya kuangalia majibu ya Jabir na Yasir, wameshikilia swali alilouliza bwana wao kuwa ndio ushahidi wao kuwa Mtume (s.a.w) alifundishwa Qur-an na watu hao.
Makafiri wengine wamedai kuwa Mtume (s.a.w) aliiandika Qur-an kwa kusaidiwa na Salman aliyekuwa Mfursi (Persian). Salman alikuwa Mzoroastian kabla ya kuwa Mkristo huko Sham (Syria). Baadaye Salman alisafiri kwenda Madina ambapo alikutana na Mtume (s.a.w) na kusilimu.



Madai haya ni dhaifu kwa sababu mbili. Kwanza, karibu theluthi mbili ya Qur-an ilishuka Makka kabla Mtume (s.a.w) hajahamia Madina ambapo alikutana na Salman. Pili, fasihi ya lugha iliyotumika katika Qur-an ni ya hali ya juu mno kiasi ambacho wanafasihi mashuhuri wa Kiarabu walijaribu kwa miaka mingi kuigiza Qur-an bila ya mafanikio yoyote, itakuwaje Mfursi awe ndiye aliyeiandika?



Madai haya yamerejewa kwenye Qur-an kama tunavyosoma katika aya ifuatayo:



"Na bila shaka tunajua kwamba wanasema:"Yuko mtu anayemfundisha," (lakini) lugha ya yule wanayemuelekezea (kuwa anamfundisha Mtume) ni ya kigeni na hii (lugha iliyotumika katika Qur-an) ni lugha ya Kiarabu fasaha (bulbul)." (16:103)



Madai yote haya pamoja na madai mengine mengi ambayo yamekuwa yakitolewa katika muda wote wa historia tangu ishuke Qur-an mpaka hivi leo, ni madai dhaifu mno ambayo hayana ushahidi wowote wa kiakili au wa kihistoria kuwa mwandishi (mtunzi) wa Qur-an ni mwengine asiye kuwa Allah (s.w).



Historia ya Mtume (s.a.w) imeandikwa na kuhifadhiwa vema kuliko historia ya mtu yeyote ulimwenguni, lakini hatuoni katika historia hiyo mahali popote tunapofahamishwa kuwa alikaa kitako kwa mtu yeyote kujifunza chochote. Kwani kama Muhammad (s.a.w) angelikuwa amesoma kwa Makasisi na Mapadri wa Kiyahudi na Kikristo au kwa mtu yeyote yafuatayo yangelijitokeza.



(a)Muhammad (s.a.w) hangelificha kueleza hayo kwani alikuwa mashuhuri katika maisha yake yote kwa kuhubiri na kusema ukweli. Aliitwa As-swadiq - Mkweli.
Ndani ya Qur-an yenyewe yamezungumzwa mambo yake ya ndani lakini bado hakuyaficha bali aliyadhihirisha kama yalivyo.



(b)Hangelifundisha imani iliyo tofautiana sana na Ukristo na Uyahudi hasa kuhusu misingi ya dini hizo. Lakini imani ya Kiislamu ni mbali na ni kinyume kabisa na imani ya Kikristo na Kiyahudi.


(c)Yeyote yule aliyemfundisha angeliweza kuandika kitabu mfano wa Qur-an angalau sura moja. Lakini hakutokea mtu yeyote mwenye uwezo huo.



(d)Mayahudi ambao katika Qur-an wameitwa "Ahlul-Kitaabi" au wana wa Israil (Bani Israil) wamekuwa katika muda wote wa utume wake wakimhoji-hoji Mtume Muhammad (s.a.w) na kumcheza shere na walikuwa wakimficha Mtume vitabu vyao. Kunawezekanaje watu hawa kama ndio waliomfundisha Mtume Qur-an wawe wanamhoji hoji tena juu ya Qur-an? Kama wangalikuwa wamemfundisha Mtume chochote, kwa nini wasingelikuwa watu wa kwanza kutangaza kwa watu kuwa wao ndio waliomfundisha ili kuonesha uongo wa utume wake?



(e)Mtume Muhammad (s.a.w) asingelikuwa mkweli katika utume wake na mwaminifu katika kutoa ujumbe aliotumwa autowe kwa watu, wafuasi wake wasingelikuwa wanyenyekevu kwake kiasi hicho na wasingelijizatiti katika kusimamisha mafundisho yake kiasi hicho katika mazingira magumu ya kufa na kupona. Historia inaonesha kuwa Waumini waliomfuata hawakumsaliti hata chembe.



Qur-an Inasadikisha Ukweli:
Sifa ya Qur-an ni kuwa inasadikisha yaliyo ya kweli katika vitabu vilivyopita. Hivyo Muislamu anaweza kujua kwa urahisi kabisa lipi ni sahihi katika Biblia na lipi si sahihi. Lolote lililomo katika vitabu vilivyotangulia ambalo linawafikiana na Qur-an ni sahihi. Na lolote linalokwenda kinyume na Qur-an ni batili.



Jambo la kusisitiza hapa ni kuwa kuhusu vitabu vilivyotangulia Qur-an imevitaja kuwa ni Suhf, Zabur, Taurat na Injili. Muislamu anayevikana vitabu hivi katika asili yake anakoma kuwa Muislamu.


Kama tulivyokwishasema Biblia inavyo kwa uchache vitabu 66. Agano la Kale lina vitabu 39 na Jipya inavyo 27. Katika vile 39 vya Agano la Kale ni vitano tu ndivyo vinavyoitwa Taurati ya Musa.



Qur-an inapotaja Taurati haikusudii Biblia au vitabu 39 vya Agano la Kale wala hivyo vitano vinavyodaiwa kuwa viliandikwa na Musa. Qur-an imeitaja Taurati kama ni ufunuo kutoka kwa Allah. Lakini tunaona kitabu cha Mwanzo ambacho kina taarifa za zamani sana kabla ya yeye (Musa) kuzaliwa. Hatuna uhakika kama kitabu hicho cha Mwanzo ilikuwa ni sehemu ya ufunuo alioupata kwenye mlima Sinai.



Isitoshe nusu ya kitabu cha Kutoka inazungumzia habari za kutoka kwa Wayahudi Misri. Hayo pia yalitokea kabla ya Musa kupata Taurati. Kitabu cha Kumbukumbu la Torati ambacho inadaiwa kiliandikwa na Musa kimeandikwa pia habari za kufariki kwa Musa:



Basi Musa, mtumishi wa BWANA, akafa huko, katika nchi ya Moabu, kukabili Beth-peori; lakini hapana mtu ajuaye kaburi lake hata leo. Musa alikuwa mtu wa miaka mia na ishirini alipokufa; jicho lake halikupofuka, wala nguvu za mwili wake hazikupunguka. Wana wa Israeli wakamwombolezea Musa katika uwanda wa Moabu siku thelathini; basi siku za maombolezo ya matanga ya Musa zikaisha. (Kumbukumbu la Torati 34:4-1 2)



Ni dhahiri kuwa upo wasiwasi kama Nabii Musa (a.s) ndiye mwandishi wa kitabu hiki kwa sababu asingeweza kusimulia habari ya kifo chake na matanga yake mwenyewe.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 565


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Naman ya kuiendea quran na kuifanyia kazi baada ya kuisoma
Soma Zaidi...

hukumu za kujifunza tajwid
Kujifunza tajwid ni katika mambo muhimu wakati wa kusoma Quran Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat an-Nas na surat al Falaq
Sura mbili hizi pia hujulikana kwa jina la al muawidhatain ambazo ni surat an Nas na surat al falaq. Soma Zaidi...

Fadhila za kusoma surat al Imran
Post hii itakufundisha fadhila na faida za kusoma surat al Imran Soma Zaidi...

Sababu za kushuka kwa Surat al-Kawthar na fadhila zake
SURATUL-KAUTHAR Imeteremshwa maka, na sura hii imeshuka kwa sababu al-aAs ibn Waail. Soma Zaidi...

surat al mauun
SURATUL-MAM’UUN Imeteremshwa Maka, anasimulia Ibn Jurayj kuwa Abuu Sufyan ibn Harb alikuwa na kawaida ya kuchinja ngamia wawili kila wiki, hivyo siku moja yatima mmoja alikuja kwake na kumlilia shida, na hakumsaidia kwa chochote na hatimaye akampiga yat.. Soma Zaidi...

quran na sayansi
Soma Zaidi...

Dai kuwa Muhammad (s.a.w) aliitunga Qur-an ili Kuwania Madaraka na Ukubwa
(x) Dai kuwa Muhammad (s. Soma Zaidi...

Quran haikutoka kwa Mtu zezeta wala mwenye upungufu wa akili
Soma Zaidi...

Sababu za Quran kuwa mwongozo sahihi wa maisha ya mwanadamu
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Je Qur-an ilikusanywa na kuandikwa katika msahafu wakati wa uongozi wa Abu-Bakr(r.a)
Je Qur-an ilikusanywa na kuandikwa katika msahafu wakati wa uongozi wa Abu-Bakr(r. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka suratul al-quraysh na fadhila zake
SURAT AL-QURAYSH Sura hii ina majina mawili. Soma Zaidi...