(c)Dai la Kufundishwa na Jabir na Yasir:
Makafiri wengine wanadai kuwa Mtume (s.a.w) alifundishwa na Jabir na Yasir waliokuwa watumwa kutoka Ethiopia (Uhabeshi) na wakasilimu mbele ya Mtume (s.a.w). Wanadai hivyo kwa kuwa bwana wao aliyekuwa akiwatesa sana kwa sababu ya kusilimu kwao alikuwa akiwapiga sana na kuwaambia: "Mnamfundisha Muhammad?" na walikuwa wakijibu "Kwa jina la Allah hatumfundishi bali ndiye anayetufundisha na kutuongoza".
Bila ya kuangalia majibu ya Jabir na Yasir, wameshikilia swali alilouliza bwana wao kuwa ndio ushahidi wao kuwa Mtume (s.a.w) alifundishwa Qur-an na watu hao.
Makafiri wengine wamedai kuwa Mtume (s.a.w) aliiandika Qur-an kwa kusaidiwa na Salman aliyekuwa Mfursi (Persian). Salman alikuwa Mzoroastian kabla ya kuwa Mkristo huko Sham (Syria). Baadaye Salman alisafiri kwenda Madina ambapo alikutana na Mtume (s.a.w) na kusilimu.
Madai haya ni dhaifu kwa sababu mbili. Kwanza, karibu theluthi mbili ya Qur-an ilishuka Makka kabla Mtume (s.a.w) hajahamia Madina ambapo alikutana na Salman. Pili, fasihi ya lugha iliyotumika katika Qur-an ni ya hali ya juu mno kiasi ambacho wanafasihi mashuhuri wa Kiarabu walijaribu kwa miaka mingi kuigiza Qur-an bila ya mafanikio yoyote, itakuwaje Mfursi awe ndiye aliyeiandika?
Madai haya yamerejewa kwenye Qur-an kama tunavyosoma katika aya ifuatayo:
"Na bila shaka tunajua kwamba wanasema:"Yuko mtu anayemfundisha," (lakini) lugha ya yule wanayemuelekezea (kuwa anamfundisha Mtume) ni ya kigeni na hii (lugha iliyotumika katika Qur-an) ni lugha ya Kiarabu fasaha (bulbul)." (16:103)
Madai yote haya pamoja na madai mengine mengi ambayo yamekuwa yakitolewa katika muda wote wa historia tangu ishuke Qur-an mpaka hivi leo, ni madai dhaifu mno ambayo hayana ushahidi wowote wa kiakili au wa kihistoria kuwa mwandishi (mtunzi) wa Qur-an ni mwengine asiye kuwa Allah (s.w).
Historia ya Mtume (s.a.w) imeandikwa na kuhifadhiwa vema kuliko historia ya mtu yeyote ulimwenguni, lakini hatuoni katika historia hiyo mahali popote tunapofahamishwa kuwa alikaa kitako kwa mtu yeyote kujifunza chochote. Kwani kama Muhammad (s.a.w) angelikuwa amesoma kwa Makasisi na Mapadri wa Kiyahudi na Kikristo au kwa mtu yeyote yafuatayo yangelijitokeza.
(a)Muhammad (s.a.w) hangelificha kueleza hayo kwani alikuwa mashuhuri katika maisha yake yote kwa kuhubiri na kusema ukweli. Aliitwa As-swadiq - Mkweli.
Ndani ya Qur-an yenyewe yamezungumzwa mambo yake ya ndani lakini bado hakuyaficha bali aliyadhihirisha kama yalivyo.
(b)Hangelifundisha imani iliyo tofautiana sana na Ukristo na Uyahudi hasa kuhusu misingi ya dini hizo. Lakini imani ya Kiislamu ni mbali na ni kinyume kabisa na imani ya Kikristo na Kiyahudi.
(c)Yeyote yule aliyemfundisha angeliweza kuandika kitabu mfano wa Qur-an angalau sura moja. Lakini hakutokea mtu yeyote mwenye uwezo huo.
(d)Mayahudi ambao katika Qur-an wameitwa "Ahlul-Kitaabi" au wana wa Israil (Bani Israil) wamekuwa katika muda wote wa utume wake wakimhoji-hoji Mtume Muhammad (s.a.w) na kumcheza shere na walikuwa wakimficha Mtume vitabu vyao. Kunawezekanaje watu hawa kama ndio waliomfundisha Mtume Qur-an wawe wanamhoji hoji tena juu ya Qur-an? Kama wangalikuwa wamemfundisha Mtume chochote, kwa nini wasingelikuwa watu wa kwanza kutangaza kwa watu kuwa wao ndio waliomfundisha ili kuonesha uongo wa utume wake?
(e)Mtume Muhammad (s.a.w) asingelikuwa mkweli katika utume wake na mwaminifu katika kutoa ujumbe aliotumwa autowe kwa watu, wafuasi wake wasingelikuwa wanyenyekevu kwake kiasi hicho na wasingelijizatiti katika kusimamisha mafundisho yake kiasi hicho katika mazingira magumu ya kufa na kupona. Historia inaonesha kuwa Waumini waliomfuata hawakumsaliti hata chembe.
Qur-an Inasadikisha Ukweli:
Sifa ya Qur-an ni kuwa inasadikisha yaliyo ya kweli katika vitabu vilivyopita. Hivyo Muislamu anaweza kujua kwa urahisi kabisa lipi ni sahihi katika Biblia na lipi si sahihi. Lolote lililomo katika vitabu vilivyotangulia ambalo linawafikiana na Qur-an ni sahihi. Na lolote linalokwenda kinyume na Qur-an ni batili.
Jambo la kusisitiza hapa ni kuwa kuhusu vitabu vilivyotangulia Qur-an imevitaja kuwa ni Suhf, Zabur, Taurat na Injili. Muislamu anayevikana vitabu hivi katika asili yake anakoma kuwa Muislamu.
Kama tulivyokwishasema Biblia inavyo kwa uchache vitabu 66. Agano la Kale lina vitabu 39 na Jipya inavyo 27. Katika vile 39 vya Agano la Kale ni vitano tu ndivyo vinavyoitwa Taurati ya Musa.
Qur-an inapotaja Taurati haikusudii Biblia au vitabu 39 vya Agano la Kale wala hivyo vitano vinavyodaiwa kuwa viliandikwa na Musa. Qur-an imeitaja Taurati kama ni ufunuo kutoka kwa Allah. Lakini tunaona kitabu cha Mwanzo ambacho kina taarifa za zamani sana kabla ya yeye (Musa) kuzaliwa. Hatuna uhakika kama kitabu hicho cha Mwanzo ilikuwa ni sehemu ya ufunuo alioupata kwenye mlima Sinai.
Isitoshe nusu ya kitabu cha Kutoka inazungumzia habari za kutoka kwa Wayahudi Misri. Hayo pia yalitokea kabla ya Musa kupata Taurati. Kitabu cha Kumbukumbu la Torati ambacho inadaiwa kiliandikwa na Musa kimeandikwa pia habari za kufariki kwa Musa:
Basi Musa, mtumishi wa BWANA, akafa huko, katika nchi ya Moabu, kukabili Beth-peori; lakini hapana mtu ajuaye kaburi lake hata leo. Musa alikuwa mtu wa miaka mia na ishirini alipokufa; jicho lake halikupofuka, wala nguvu za mwili wake hazikupunguka. Wana wa Israeli wakamwombolezea Musa katika uwanda wa Moabu siku thelathini; basi siku za maombolezo ya matanga ya Musa zikaisha. (Kumbukumbu la Torati 34:4-1 2)
Ni dhahiri kuwa upo wasiwasi kama Nabii Musa (a.s) ndiye mwandishi wa kitabu hiki kwa sababu asingeweza kusimulia habari ya kifo chake na matanga yake mwenyewe.
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Quran Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1084
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi
👉2 Simulizi za Hadithi Audio
👉3 Kitau cha Fiqh
👉4 Kitabu cha Afya
👉5 Madrasa kiganjani
👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Sababu za kushukasurat an Nasr
Sura hii ni katika sura za mwisho kushuka, huwendakuwa ndio ya mwisho kabisa. Masahaba waliamini kuwa sura hii imetabiri kifo cha Mtume S.A.W Soma Zaidi...
Quran na sayansi
3; Mchujo wa maji dhaliliKatika aya nyingine tunakuja kupata funzo kuwa maji aliyoumbiwa mwanadamu licha yakuwa na sifa zilizotajwa katika kurasa zilizopita ila pia maji haya yanasifa kuwa ni madhalilina pia na yamechujwa kama tunavyoelezwa katika quran?? Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al Fatiha
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu srat al fatiha, faida zake na maudhui zake Soma Zaidi...
Nini maana ya Iqlab katika hukumu za tajwid
Hapa utajifunza maana ya iqlab katika usomaji wa Quran kwa tajwid Soma Zaidi...
Hukumu za Idh-har na id-gham katika laam al-maarifa
Laam al- maarifa inaweza kusomwa kwa idgham au idh-har pindibitakapokutana na herufi za shamsiya au qamariya. Soma Zaidi...
quran na sayansi
YALIYOMONENO LA AWALI1. Soma Zaidi...
Naman ya kuiendea quran na kuifanyia kazi baada ya kuisoma
Soma Zaidi...
Sababu za kushuka Surat al Kafirun
Sura hii imekuja kukata rai ya Makafiri wa Makka kuhusu ibada ya ushirika. Hivi leo tungesema kuhusu dini mseto. Soma Zaidi...
quran na sayansi
2:UUMBWAJI KWA MAJI YA UZAZIUumbwaji wa mwanadamu umepitia hatua mbalimbali na haya yote yamefanywa kwa sababumaalumu ili tipate mazingatio. Soma Zaidi...
Hukumu za waqfu na Ibtida
waqfu ni misimamo ambapo msomaji wa Quran anaruhusiwa kusimama, kuhema au kumeza mate. Na ibtidai ni kuanza baada ya kutoka kwenye waqf Soma Zaidi...
namna quran inavyogawanya mirathi na wanaorithi pamoja na mafungu yao
Qur-an inavyogawa MirathiMgawanyo wa mirathi umebainishwa katika Qur-an kama ifuatavyo:Mwenyezi Mungu anakuusieni juu ya watoto wenu: Mwanamume apate sawa na sehemu ya wanawake wawili. Soma Zaidi...
Tofauti kati ya sura za makkah na madinah
Quran (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...