Mpangilio wa quran ni wa kipekee na uliotumia ujuzi mkubwa

Mpangilio wa quran ni wa kipekee na uliotumia ujuzi mkubwa

(vii)Mpangilio wa Qur-an:



Ukiuchunguza msahafu kwa kina utagundua kuwa si kitabu cha kawaida kama vile wanavyo vitunga wanaadamu. Qur-an pamoja na aya zake kufumwa na maneno ya Kiarabu, pametumika ujuzi usio na mfano katika uchaguzi na mpangilio wa maneno. Maneno yamechaguliwa na kupangiliwa kwa kiasi kwamba huwianisha habari zote zilizoelezwa ndani ya Kitabu na kuufikisha ujumbe kwa wepesi. Mifano michache ifuatayo itatupa picha ya mpangilio wa ajabu wa Qur-an:



Kwanza, kutokana na uchunguzi uliofanyika kwa kutumia kompyuta imedhihirika kuwa sura zile zilizoanza na herufi kama Qaf ( )zina idadi kubwa zaidi ya herufi hiyo ukilinganisha na herufi nyingine katika sura hizo.



Pili, Kuna sura 114 katika msahafu na kila sura imeanza kwa "Bismillahir-Rahmaanir-Rahiim" isipokuwa Suratut Tawba. Hi huifanya idadi ya "Bismillahir-Rahmaanir-Rahiim" kuwa 113. Lakini katika Suratun-Naml kuna "Bismillahir-Rahmaanir-Rahiim" iliyoletwa katikati ya sura.


Imetoka kwa Suleimani, nayo ni: Kwa jina la Mwenyezi Mungu,Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu." (2 7:30) Hivyo huifanya idadi ya "Bismillahir-Rahmaanir-Rahiim" kuwa 114 sawa na idadi ya sura zote katika msahafu. Je, hii imetokea kwa bahati tu au ni mpangilio wa Mjuzi, Mwenye Hikma.



Tatu, kutokana na uchunguzi imedhihirika kuwa maneno mbali mbali katika Qur-an yamerudiwa kwa kuzingatia idadi maalum. Kwa mfano neno "Sema" () limerudiwa mara 332 katika msahafu na neno "Alisema" () limerudiwa mara hizo hizo 332. Pia katika Qur-an zimetajwa "Mbingu Saba" ( ) na maneno haya yamerudiwa mara saba tu katika
msahafu mzima. Kuna miezi kumi na mbili katika mwaka mmoja na neno "Shahr"( )lenye maana ya mwezi limetajwa mara 12 katika Qur-an. Neno "Yaum" ( )katika Qur-an limetajwa mara 365 sawa na idadi ya siku za mwaka mmoja katika mwendo wa jua!



Nne, Qur-an inapofananisha jambo fulani na lingine, idadi ya utajo wa mambo hayo kitabuni humo pia huwiana. Kwa mfano katika sura ya 3 aya 59 Qur-an inasema: Bila shaka hali ya Issa mbele ya Allah ni kama ile ya Adam.Alimuumba kwa udongo, kisha akamwambia kuwa na akawa. (3:59).



Adam(a.s) ametajwa mara 25 katika Qur-an. Issa(a.s) vile vile ametajwa mara 25 katika Qur-an. Zaidi ya hivyo katika sura 3:59, Adam ametajwa kwa mara ya saba vivyo hivyo Issa nae ametajwa kwa mara ya saba katika aya hiyo.



Adam(a.s) ametajwa katika aya zifuatazo:
2:31, 2:33, 2:34, 2:35, 2:37, 3:33, 3:59 (mara ya saba), 5:27, 7:11, 7:26, 7:31, 7:35, 7:35, 7:172, .17:61, 17:70, 18:50, 19:58, 20:115, 20:116, 20:117, 20:120, 20:121, 36:60.



Issa(a.s) ametajwa katika aya zifuatazo:
2:87, 2:136, 2:253, 3:45, 3:52, 3:55, 3:59 (mara ya saba), 3:84, 4:157, 4:163, 4:171, 5:46, 5:78, 5:110, 5:112, 5:114, 5:116, 6:85, 19:34, 33:7, 42:13, 43:63, 57:27, 61:6 na 61:14.


Mfano mwingine ni ule wa sura ya 7 aya ya 176. Qur-an inawalinganisha watu wanaofuata matamanio ya nafsi zao kinyume na aya za Mwenyezi Mungu, kuwa hao ni sawa na mbwa (Kalb).


"Hali yao ni sawa na ile ya mbwa:


Tamko:"Wale wanaokanusha aya zetu( ) limerejewa mara 5 katika Qur-an, na neno "mbwa"() limetajwa mara 5:
Tamko:"Wale wanaokadhibisha aya zetu limetajwa katika aya zifuatazo:7:176 (mara ya kwanza),7:177,21:77, 25:36 na 62:5 (mara ya tano).


Neno mbwa (kalb) limetajwa katika aya zifuatazo: 7:176 (mara ya kwanza), 18:18, 18:22
Aidha Qur-an inaposema jambo au kitu hiki si kama kile idadi ya mambo au vitu hivyo haiwiani katika kutajwa kwake ndani ya Qur-an.2
Kutokana na mifano hii michache ni muhali mwanaadamu kuweza kuandika kitabu chenye mfumo wa maneno, aya na sura mithili ya Qur-an.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 1264

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

MAANA NA HUKUMU YA TAJWIDI

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
mafunzo ya TAJWID na imani ya dini ya kiislamu

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Maana ya qalqala na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid

Qalqala imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Qalqalatul qubra yaani qalqala kubwa na qalqalat as shughura yaani qalqala ndogo.

Soma Zaidi...
fadhila za sura kwenye quran

FADHILA ZA BAADHI YA SURA Umuhimu na ubora wa baadhi ya sura na aya.

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA IDGHAM

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Ni zipi hukumu za nuni yenye sakina au tanwin?

Hapa utajifunza usomaji wa Quran pindi utakapokuta nuni yenyebsakina au tanwin

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al-Fiyl

Al fiyl ni neno la Kiarabu lenye maana ya tembo. Sura hii inazungumziakisa cha jeshi lenye tembo. Jeshi hili lilikuwa na nia ya kuvunja al qaaba

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al adiyat

Sura hii iliposhuka ilikuwa kama imekuja kuwasuta Wanafiki waliokuwa wakizungumzahabari za uongo kuhusu jeshi alilolituma Mtume wa Allah.

Soma Zaidi...