Makatazo ya kujiepusha nayo

Makatazo ya kujiepusha nayo

(2) Makatazo ya kujiepusha nayo



Yale waumini wanayowajibika kujiepusha nayo kwa mnasaba wa aya tulizozipitia (17:23-40) ni haya yafuatayo:



(a) Kujiepusha na kumshirikisha Allah (s.w)
Kumshirikisha Allah (s.w) ni kujaalia kuwa Allah (s.w) anao washirika wake wanaomsaidia katika kuendesha masuala mbali mbali katika mchakato mzima wa maisha ya dunia. Allah (s.w) hushirkishwa kinadharia na kiutendaji.



Allah (s.w) hushikirishwa kinadharia kwa kujaalia kiumbe kisicho na uwezo wowote, kama vile sanamu, jiwe kubwa, mti mkubwa, majini, malaika, n.k.; kuwa ni mungu na kukielekea kwa maombi na kukitegemea kama apasavyo kuombwa na kutegemewa Allah (s.w). Hii ni shiriki katika Dhati ya Allah (s.w). Pia Allah (s.w) hushirikishwa kinadharia, kwa kumnasibisha na kiumbe au kukipachika kiumbe sifa anazostahiki kusifiwa kwazo. Hii ni shiriki katika sifa za Allah (s.w).


Allah (s.w) hushirikishwa kiutendaji kwa kutiiwa kanuni na sharia na kufuatwa miongozo ya maisha iliyotungwa na watu kinyume na mwongozo wa maisha wa Allah (s.w) kupitia kwa Mitume wake na Vitabu vyake. Kumtii yeyote kinyume na kanuni na sharia za Allah (s.w) ni kumshirikisha Allah (s.w) katika Mamlaka yake. Na kupitisha hukumu yoyote kinyume na alivyohukumu Allah (s.w) ni kumshirikisha katika Hukumu zake. Shirk ndio kiini na chanzo kikuu cha maovu yote duniani na ndio msingi mkuu wa dhuluma (rejea Qur-an 31:13)




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1075

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰2 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    πŸ‘‰4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰5 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Maana ya kumuamini mwenyezi Mungu (s.w) katika maisha ya kila siku

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
KUAMINI MALAIKA

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

Soma Zaidi...
Kujiepusha na kukaribia zinaa

Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa.

Soma Zaidi...
Lengo la ibada maalumu

Lengo la ibada maalumu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kujiepusha na kukaribia zinaa

Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa.

Soma Zaidi...