Makatazo ya kujiepusha nayo

Makatazo ya kujiepusha nayo

(2) Makatazo ya kujiepusha nayo



Yale waumini wanayowajibika kujiepusha nayo kwa mnasaba wa aya tulizozipitia (17:23-40) ni haya yafuatayo:



(a) Kujiepusha na kumshirikisha Allah (s.w)
Kumshirikisha Allah (s.w) ni kujaalia kuwa Allah (s.w) anao washirika wake wanaomsaidia katika kuendesha masuala mbali mbali katika mchakato mzima wa maisha ya dunia. Allah (s.w) hushirkishwa kinadharia na kiutendaji.



Allah (s.w) hushikirishwa kinadharia kwa kujaalia kiumbe kisicho na uwezo wowote, kama vile sanamu, jiwe kubwa, mti mkubwa, majini, malaika, n.k.; kuwa ni mungu na kukielekea kwa maombi na kukitegemea kama apasavyo kuombwa na kutegemewa Allah (s.w). Hii ni shiriki katika Dhati ya Allah (s.w). Pia Allah (s.w) hushirikishwa kinadharia, kwa kumnasibisha na kiumbe au kukipachika kiumbe sifa anazostahiki kusifiwa kwazo. Hii ni shiriki katika sifa za Allah (s.w).


Allah (s.w) hushirikishwa kiutendaji kwa kutiiwa kanuni na sharia na kufuatwa miongozo ya maisha iliyotungwa na watu kinyume na mwongozo wa maisha wa Allah (s.w) kupitia kwa Mitume wake na Vitabu vyake. Kumtii yeyote kinyume na kanuni na sharia za Allah (s.w) ni kumshirikisha Allah (s.w) katika Mamlaka yake. Na kupitisha hukumu yoyote kinyume na alivyohukumu Allah (s.w) ni kumshirikisha katika Hukumu zake. Shirk ndio kiini na chanzo kikuu cha maovu yote duniani na ndio msingi mkuu wa dhuluma (rejea Qur-an 31:13)




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 953

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Kuwa wenye shukurani mbele ya Allah (s.w)

Mwanaadamu ametunukiwa neema mbali mbali na Mola wake kuliko viumbe wengine wote kama tuanvyojifunza katika aya mbali mbali za Qur'an.

Soma Zaidi...
Kujiepusha na maringo na majivuno

Maringo, majivuno, majigambo, dharau ni vipengele vya kibri.

Soma Zaidi...
Haki za kielimu za mwanamke katika uislamu

Haki ya ElimuKatika Uislamu kujielimisha ni faradhi inayowahusu Waislamu wote, wanaume na wanawake: "Soma kwa jina ?

Soma Zaidi...
Makemeo juu ya Zinaa na Hukumu kwa Wazinifu.

Tendo la zinaa ni tendo chafu kimaadili na Allah (s.

Soma Zaidi...
Elimu yenye manufaa

Elimu yenye manufaa Ni ipi? (EDK form 1:elimu yenye manufaa)

Soma Zaidi...
Kwa nini Uislamu ndio dini pekee inayostahiki kufuatwa

Kwa nini uislamu ndio dini pekee ya haki ambayo watu wanatakiwa waifuate.

Soma Zaidi...
Kwa nini hakuna haja ya Mtume mwingine baada ya Muhammad

Na tukiutafiti Uislamu kwa makini kama mfumo kamili wa maisha tunaona unadhihiri ukweli wa aya hii ya Qur-an.

Soma Zaidi...
Kuamini Qadar ya Mwenyezi Mungu

Nguzo za imani (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu

Soma Zaidi...