PHP - somo la 28: Maana ya constant kwenye php na kazi zake
Katika somo hili utajifunza kuhusu maana ya constanta pamoja na matumizi yake. Pia utazijuwa sheria za uandishi wa constant
PHP CONSTANTS
Je constants ni nini?
Constant ni jina ambalo hupewa thamani fulani ambayo haitabadilika kwenye script za php wakati zinapofanya kazi. Constants na variable hufanana ytofauti mkubwa ni kuwa, constants hazibadiliki lakini variable hubadilika.
Ni yapi matumizi yake:
Constant hutumika hasa kwa zile taarifa ambazo haziwezi kubadilika wakati wa code zinapofanya kazi. Kwa mfano tunatumia constant kwa ajili ya database configuration. Au login ambazo hazihitaji database. Ama unaweza kutumia constatnt popote bale kama mbadala wa variable.
Kanuni za kuandika constants:
Unapoandika constant ujuwe kuwa haianzi na alama ya dola $ kama ilivyo variable. Unaweza kuanza na herufi au underscode (_). Pia tunapoandika constants tunaanza na neno define likifuatiliwa na mabano ya kufunga na kufunguwa () mfano define()
Pia unaweza kusema kama constat hiyo inaangalia case-sensitivity, yaani kufuata kamaherufi ni kubwa iwe hivyohivyo na kamaherufi ni ndoo iwe hivyohivyo. Yaani hii ipo hivi, wakati wa kujakuitumia constants endapo hapo mwanzo uliiandika kwa herufi kubwa basi hata wakati wa kuitumia uandike hivyohivyo kwa herufi kubwa. Sasa jambo hili unaweza kuliset.
Ndani ya mabano kunakaa jina la constant, thamani ya conctanta, na case sensitivity. Hivyo basi kanuni ya kuandika constant inaweza kufupishwa hivi:-
define(jina, thamani, case-insensitive)
Mfano 1:
define("chakula", "ugali, nyama na soda");
echo chakula;
?>
Kama hapo juu jina la constant ni chakula kwa herufi ndogo. Na wakati wa kuitumia nimetumia hivyo hivyo herufi ndogo. Endapo ningetumia herufi kubwa ingeleta error. Sasa endapo unataka isijali herufi ziwe kubwa ama ndogo utaongeza parameta nyingine kwenye mabano kwa ajili ya kueleza case insensitive.
Case sensitivity ipo katika namna mbili eidha iwe true au false. Ukiacha bila ya kuipanga basi itakuwa ni case-sensitive ambayo hufuata hefufikubwa ni kubwa na ndogo i ndogo.
...Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 ai web app 👉5 web hosting 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Wajuwe wanasanyansi na lugha za kompyuta walizoanzisha
Hii ni list ya wataalamu wa kompyuta amba ni wagunduzi wa lugha zaidi ya 20 za kompyta.
Soma Zaidi...Ijuwe platform ya IndexNow
Je umeshawahi kuweka post yako kwenye blog halafu ikachukuwa mpaka siku 3 kuonekana kwenye search engine kama Google, Index ama Bing. Bsi project ya IndexNow imekuja kutatuwa tatizo hilo
Soma Zaidi...Njia ya haraka ku download video za Youtube
Katika post hii utakwenda kujifunza hatuwa kwa hatuwa za ku download video za Youtube kwa haraka.
Soma Zaidi...Utangulizi wa mvc na umuhimu wake
Katika somo hili, tutajifunza: Maana ya MVC (Model-View-Controller) Kila kipengele (Model, View, Controller) kinachofanya Faida za kutumia MVC Tatizo la PHP ya kawaida bila MVC
Soma Zaidi...Ifahamu Y2K yaani year 2000 bug
Moja katika changamoto iliyowahi kusumbuwa dunia kutokana na maendeleo ya tehama duniani.
Soma Zaidi...CSS Functions – calc(), clamp(), var(), min(), max() na Custom Functions
Katika somo hili, tutajifunza kuhusu CSS functions muhimu zinazotumika kufanya mahesabu, kuweka vipimo vya kisasa vinavyobadilika kulingana na hali ya kifaa, na kutumia variables. Tutazingatia functions kama: calc(), clamp(), var(), min(), max(), na mwishoni tutajifunza jinsi ya kutengeneza custom function kwa kutumia variables.
Soma Zaidi...