MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO.
MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO.
Maana ya Zakat
Kilugha: Katika lugha ya Kiarabu neno “zakat” lina maana ya utakaso (Purification). Neno “Zakat” limetumika katika Qur’an kwa maana hii katika aya zifuatazo:
“Bila shaka amefuzu aliyeitakasa (nafsi yake)” (91 :9).
“Hakika ameshafuzu aliyejitakasa (na mabaya)” (8 7:14).
Kisheria: Katika sheria ya Kiislamu “Zakat” ni sehemu ya mali ya tajiri (2.5% au 1/40) anayoitoa kwa kutekeleza amri ya Allah (s.w) na kuwapa wanaostahiki, baada ya kupindukia mwaka au baada ya mavuno iwapo mali hiyo imefikia Nisaab. Nisaab ni kima cha chini cha mali ambacho mtu akiwa nacho au zaidi yake analazimika kutoa Zakat.
Maana ya Sadaqa
Kilugha: Katika lugha ya Kiarabu neno “Sadaqa” linatokana na “Sidiq” lenye maana ya ukweli.
Kisheria: Katika sheria ya Kiislamu Sadaqat ni mali au huduma iinayotolewa au kupewa mtu yoyote anayehitajia kwa ihsani tu bila ya kutarajia malipo yoyote kutoka kwake. Maana ya “Sadaqat” inabainishwa vizuri katika Hadithi zifuatazo:
1.Jabir na Hudhaifa (r.a) wameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Kila kitendo kizuri ni Sadaqat”. (Bukhari na Muslim).
2.Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: Katika kila kiungo cha mtu kuna Sadaqat. Kuna Sadaqat katika kila mtu. Kufanya uadilifu kati ya watu wawili ni sadaqat; kumsaidia mtu kupanda mnyama wake anayesafiri naye au kumsaidia mtu kutwika mzigo wake ni sadaqat; neno zuri ni sadaqat na kila hatua mtu anayotembea kwenda kwenye swala ni sadaqat na kuondoa kitu kibaya njiani ni sadaqat”. (Bukhari na Muslim).
TOFAUTI YA ZAKA NA SADAKA
1. Zaka ni nguzo ya Uislamu na ni lazima, lakini dadaka si lazima
2. Zaka hutolewa kwa kiwango maalumu, lakini sadaka haina kiwango maalumu
3. Zaka hutolewa mali, lakini sadaka sio lazima iwe mali
4. Zaka hutolewa ndani ya muda maalumu, lakini sadaka haina muda maalumu
5. Zaka inatolewa kwa watu maalumu, lakini sadaka haijaelezewa watu maalumu wa kuwapatia.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu
Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh
Main: Post
File: Download PDF
Share On
Facebook
or
Whatsapp
Views 2383
Sponsored links
👉1
Kitabu cha Afya
👉2
kitabu cha Simulizi
👉3
Madrasa kiganjani
👉4
Simulizi za Hadithi Audio
👉5
Kitau cha Fiqh
👉6
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Mambo yenye kufunguza swaumu (funga)
Soma Zaidi...
Yajuwe mandalizi ya Ibada ya hija
Soma Zaidi...
.Mazingatio muhimu katika uchumi wa Kiislamu
3. Soma Zaidi...
Faida za funga
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Zoezi la 6 kusimamisha swala
Zoezi hili linamaswali mbalimbali kuhusiana na swala na masharti ya swala. Soma Zaidi...
Zaka katika mapambo, mali ya biashara na mali iliyofukuliwa ardhini
Soma Zaidi...
Nguzo za swala ya maiti
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Yaliyo haramu kwa mwenye hadathi kubwa.
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ya haramu kwa mwenye hadathi kubwa Soma Zaidi...
Maana ya Swaumu na Lengo la kufunga
Soma Zaidi...
Kuandama kwa Mwezi na Kufunga ama kufungua ramadhani, sheria na hukumu za kuangalia mwezi
Soma Zaidi...