MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO

MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO

MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO.

Download Post hii hapa

MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO

MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO.


Maana ya Zakat



Kilugha: Katika lugha ya Kiarabu neno “zakat” lina maana ya utakaso (Purification). Neno “Zakat” limetumika katika Qur’an kwa maana hii katika aya zifuatazo:
“Bila shaka amefuzu aliyeitakasa (nafsi yake)” (91 :9).
“Hakika ameshafuzu aliyejitakasa (na mabaya)” (8 7:14).


Kisheria: Katika sheria ya Kiislamu “Zakat” ni sehemu ya mali ya tajiri (2.5% au 1/40) anayoitoa kwa kutekeleza amri ya Allah (s.w) na kuwapa wanaostahiki, baada ya kupindukia mwaka au baada ya mavuno iwapo mali hiyo imefikia Nisaab. Nisaab ni kima cha chini cha mali ambacho mtu akiwa nacho au zaidi yake analazimika kutoa Zakat.



Maana ya Sadaqa



Kilugha: Katika lugha ya Kiarabu neno “Sadaqa” linatokana na “Sidiq” lenye maana ya ukweli.
Kisheria: Katika sheria ya Kiislamu Sadaqat ni mali au huduma iinayotolewa au kupewa mtu yoyote anayehitajia kwa ihsani tu bila ya kutarajia malipo yoyote kutoka kwake. Maana ya “Sadaqat” inabainishwa vizuri katika Hadithi zifuatazo:



1.Jabir na Hudhaifa (r.a) wameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Kila kitendo kizuri ni Sadaqat”. (Bukhari na Muslim).



2.Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: Katika kila kiungo cha mtu kuna Sadaqat. Kuna Sadaqat katika kila mtu. Kufanya uadilifu kati ya watu wawili ni sadaqat; kumsaidia mtu kupanda mnyama wake anayesafiri naye au kumsaidia mtu kutwika mzigo wake ni sadaqat; neno zuri ni sadaqat na kila hatua mtu anayotembea kwenda kwenye swala ni sadaqat na kuondoa kitu kibaya njiani ni sadaqat”. (Bukhari na Muslim).



TOFAUTI YA ZAKA NA SADAKA


1. Zaka ni nguzo ya Uislamu na ni lazima, lakini dadaka si lazima


2. Zaka hutolewa kwa kiwango maalumu, lakini sadaka haina kiwango maalumu


3. Zaka hutolewa mali, lakini sadaka sio lazima iwe mali


4. Zaka hutolewa ndani ya muda maalumu, lakini sadaka haina muda maalumu


5. Zaka inatolewa kwa watu maalumu, lakini sadaka haijaelezewa watu maalumu wa kuwapatia.




                   


Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 3305

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Mafunzo ya swala
Mafunzo ya swala

Jifunze namna ya kuswali, zijuwe aina za swala na ujifunze masharti ya swala, kwa nini swala hazijibiwi? nini kifanyike?

Soma Zaidi...
Hadhi na haki za mwanamke katika jamii za Kigiriki hapo zamani
Hadhi na haki za mwanamke katika jamii za Kigiriki hapo zamani

(a) UgirikiTunajifunza katika historia ya Ulimwengu kuwa jamii ya Wagiriki ilikuwa miongoni mwa jamii zilizoanza kustarabika.

Soma Zaidi...
Mgogoro wa kuandama kwa mwezi, Je mwezi wa Kimataifa ama kila Mji na mwezi wake?
Mgogoro wa kuandama kwa mwezi, Je mwezi wa Kimataifa ama kila Mji na mwezi wake?

Mwezi ukionekana sehemu moja, Waislamu wote ulimwenguni watalazimika kufunga?

Soma Zaidi...
 Ubainifu kati ya halali na Haramu na kujiepusha na mambo yanayo tatiza
Ubainifu kati ya halali na Haramu na kujiepusha na mambo yanayo tatiza

عَنْ أَبِي عَبْدِ اللَّهِ النُّعْمَانِ بْنِ بَشِيرٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا، قَالَ: سَمِعْت رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم يَقُ?...

Soma Zaidi...
Yajuwe masharti ya udhu yaani yanayofanya udhu kukubalika
Yajuwe masharti ya udhu yaani yanayofanya udhu kukubalika

Posti hii itakufundisha masharti yanayohitajika kwa mwenye kutaka kutia udhu.

Soma Zaidi...
Wanaowajibika kuhijji
Wanaowajibika kuhijji

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Funga za Sunnah na umuhimu wake
Funga za Sunnah na umuhimu wake

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...