Kukaa Itiqaf
Kukaa Itiqaf katika kumi la mwisho la Ramadhani ni sunna iliyokokotezwa. Ki-lugha โItqafโ ina maana ya kukaa mahali. katika sheria ya Kiislamu โItiqafโ ni kukaa msikitini kwa ajili tu ya kumkumbuka na kumtukuza Allah (s.w) na kufanya ibada maalum kama vile kuswali, kusoma Qur-an na kufanya amali yoyote njema ambayo inaruhusiwa kufanyika msikitini nje ya shughuli za kawaida za kutafuta rizki. Kwa hiyo mahali pa kukalia โItiqafโ ni msikitini kama ilivyotajwa katika Qur-an:
โ... Wala msichanganyike nao, na hali mmekaa Itiqaf misikitini .... โ (2:187).
Misikiti inayokaliwa Itiqaf iwe ni ile inayoswaliwa jamaa na Ijumaa ili pasiwe na haja ya kutoka kwa swala za jamaa au kwa swala ya Ijumaa. Wanawake wanaruhusiwa kufanyia Itiqaf zao majumbani mwao katika sehemu zao za kusalia lakini baada ya kupata ruhusa kutoka kwa waume zao. Kwa muda wote mtu atapokuwa katika Itiqaf haruhusiwi kutokatoka msikitini ila kwa dharura kubwa sana kama vile kwenda haja au kwenda kula. Mtu akiwa katika Itiqaf hulazimika kujitenga na shughuli zote za kutafuta maslahi ya maisha na shughuli zote za kijamii kama vile kutembelea wagonjwa, kuhudhuria mazishi, na kadhalika. Mtu anapokuwa katika Itiqaf haruhusiwi kuchanganyika na mkewe.
โ ... Na w ala msichanganyike nao na hali mnakaa Itiqaf msikitini. (2:187).
Kwa ujumla katika muda huu wa kukaa Itiqaf, Muโtakif (Mwenye kukaa Itiqaf) anatakiwa ajihusishe tu na ibada maalum kama vile kuswali, kusoma Qur-an, kuleta tasbihi, tahmid, tahalili, takbir, istighfar na maombi mbali mbali.
Muโtakif anaruhusiwa kuja na matandiko yake msikitini na kuyaweka mahali pa uficho ambapo hayatawakarahisha watu wakati wa swala ya jamaa. Katika miezi mingine isiyokuwa Ramadhani mtu anaweza kukaa itiqaf kwa muda wowote ule, siku moja au masaa machache. Ni vyema mtu anapokuwa hana shughuli muhimu, anuie kukaa Itiqaf msikitini badala ya kujiingiza kwenye shughuli zisizo muhimu au shughuli za upuuzi zenye kumuingiza katika dhambi na kumpotezea muda ambao ni rasilimali pekee ya maisha yake. Katika mwezi wa Ramadhani Itiqaf imekokotezwa sana katika kumi la mwisho ili kumuwezesha Muumini kuudiriki usiku wa Lailatul-Qadr - akiwa katika hali ya kumkumbuka Allah (s.w). Mtume (s.a.w) alikuwa akikaa Itiqaf katika kumi hili la mwisho kama tunavyojifunza katika hadith zifu atazo:
Ames imulia Abdullah bin Umar (r.a) kuwa Mtume (s.a.w) alikuwa akikaa Itiqaf katika siku kumi za mwisho za mw ezi wa Ram adhani. (Bukhari na Muslim).
Aysha (r.a.) amesimulia kuwa Mtume wa Allah alikuwa akikaa Itiqaf katika siku kumi za mwisho za Ramadhani mpaka alipotawafu (Allah alipo mchukua).Kisha wakeze waliendelea kukaa Itiqaf baada yake. (Bukhari na Muslim).
Umeionaje Makala hii.. ?
Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga.
Soma Zaidi...Kwenye kipengele hichi tutajifinza vyanzo mbalimbali vya sheria ua kiislamu.
Soma Zaidi...Lengo la funga ni kuwa mchamungu sasa ni kwa nini wafungaji hawalifikii lengo hili na kuwa wachamungu.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza watu ambao ni halali kuwaoa na wale ambao ni haramu kuwaoa.
Soma Zaidi...Aina za Swala za Sunnah.
Soma Zaidi...Post hiibitakugundisha hekima ya kuruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja katika sheria za kiislamu.
Soma Zaidi...Posti hii itakwenda kukufunza utofauti kati ya uadilifu na usawa
Soma Zaidi...