Epuka kukata tamaa, na yajuwe madhara ya kukata tamaa

37.

Epuka kukata tamaa, na yajuwe madhara ya kukata tamaa

37. Kuepukana na Kukata Tamaa



Pia Muislamu hatakiwi kukata tamaa na Rehema za Mwenyezi Mungu (s.w). Hakuna kinachoshindikana kwa Mwenyezi Mungu. Muislamu hana budi kufanya jitihada katika kufanikisha jambo muhimu la maisha kwa kufuata njia za halali anazoziridhia Mwenyezi Mungu (s.w). Kama jambo hilo lina kheri na yeye, basi Mwenyezi Mungu (s.w) atalifanikisha. Mzee Yaquub (a.s) akiwausia wanawe wasichoke kumtafuta Yusuf na ndugu yake aliwaambia:



โ€œEnyi wanangu! Nendeni mkamtafute Yusuf na nduguye, w ala msikate tamaa na Rehema ya Mwenyezi Mungu. Hawakati tamaa na Rehema ya Mw enyezi Mungu isipokuw a w atu makafiriโ€. (12:87).



Pia iwapo baada ya Muislamu kufanya juhudi na kutumia uwezo wake wote, hakupata mafanikio aliyotarajia, asikate tamaa bali aridhike kuwa matokeo hayo ndiyo yenye kheri kwake kwa kuzingatia Qur-an:


โ€œ... Lakini huenda mkachukia kitu nacho ni kheri kwenu. Na huenda mkapenda kitu nacho ni shari kwenu. Na Mwenyezi Mugu ndiye anayejua, (lakini) nyinyi hamjuiโ€. (2:216).




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Dini File: Download PDF Views 1279

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰3 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰5 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Kushika mwenendo wa kati "Na ushike mwenendo wa katiโ€ฆ." (31:19)

Mwenendo wa kati ni mwenendo ulioepukana na kibri na majivuno kwa upande mmoja na ulioepukkana na udhalili na unyonge kwa upande mwingine.

Soma Zaidi...
Fadhila za kujenga msikiti

Kuna malipo makubwa kwa ambaye amejenga msikiti kwa ajili ya kuoatavradhi za Allah.

Soma Zaidi...
sura ya 02

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...