picha

kuwa na kauli njema, na faida zake katika jamii

11.

kuwa na kauli njema, na faida zake katika jamii

11. Kuwa na Kauli Njema


Muislamu anatakiwa kila mara azungumze mambo ya maana na ya kheri. Ulimi utumike kusema ukweli, kuamrisha mema, kukataza maovu, kuwashauri wengine juu ya mambo ya kheri, kupatanisha waliogombana, kumsabihi Allah, kutoa elimu yenye kunufaisha watu na katika mazungumzo mengine ya kheri.


“Na ni nani asemaye kauli bora kuliko (yule) aitaye (watu) kwa Allah na (mwenyewe) akafanya vitendo vizuri na kusema (kwa maneno yake na vitendo vyake): “Hakika mimi ni miongoni mw a Waislamu ”. (41:33).
Allah (s.w) anatuamrisha kusema maneno mazuri katika aya ifu atayo:

“Na waambie waja wangu waseme daima maneno yaliyo mazuri. Maana Shetani huchochea ugomvi baina yao. Hakika shetani kwa wanaadamu ni adui aliye dhahiri”. (17:53)
Hivyo Muislamu hana budi kuzungumza na watu kwa maneno mazuri ya heshima. Maneno mazuri ya heshima yanajenga na kuzidisha upendo kati ya watu. Maneno mazuri ya heshima ni ngao ya kumzuilia shetani asiingilie kati na kuleta migongano na kutoelewana. Ni katika msingi huu tunaamrishwa tuulinganie Uislamu kwa hekima na kwa mawaidha mazuri:

“Walinganie (watu) katika njia ya Mola wako kwa hekima na mawaidha m em a, na ujadiliane nao kw a namna iliyo bora. Hakika Mola w ako ndiye anayemjua aliyepotea katika njia yake naye ndiye anayewajua walioongoka ”. (16:125).
Kauli njema ni yenye kumuongoza mja kwenda Peponi na kauli mbaya humuongoza mja kwenda Motoni kama tunavyojifunza katika Hadithi zifuatazo:
Sahl bin Sa ’d(r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “Atakayeweza kuchunga kilichopo kati kati ya taya zake (ulimi) na kilichopo katikati ya miguu yake miwili (utupu) ninaw eza kumhakikishia Pepo.” (Bukhari).

Abu Hurairah(r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: “Mja atatamka neno lenye kumfurahisha Allah bila ya kuona uzito wake, bado Allah (s.w) humlipa malipo makubwa kutokana na neno hilo. Na mja atatamka neno lenye kumuudhi Allah bila ya kuona uzito wake, na bado linakuw a ndio mw anzo w a kumuingiza Motoni. (Bukhari).



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 2061

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Dua za Mitume na Manabii    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Maana ya Hadith al Quds na Hadith an-Nabawiy

Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya hadithi al Quds na Hadith an-Nabawiy

Soma Zaidi...
BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU

BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU.

Soma Zaidi...
DUA 113 - 126

DUA ZA WAKATI WA SHIDA Dua ya wakati wa taabu “LAA ILAAHA ILLA-LLAHUL-’ADHIMUL-HALIIMU.

Soma Zaidi...
Faida za swala ya Mtume

Hapa utajifunza fadhila za kumswalia Mtume (s.a.w)

Soma Zaidi...
NAMNA AMBAZO DUA HUJIBIWA

NAMNA AMBAYO ALLAH HUJIBU DUA.

Soma Zaidi...
Dua 10 ambazo ni muhimu kuziomba kwa kila siku.

Posti hii inakwenda kukupa orodha ya dua 10 ambazo unaweza kuziomba kila siku.

Soma Zaidi...
Sura za kujikinga na Uchawi na mashetani

Post hii itakwenda kukufundisha sura katika Quran ambazo ni kinga dhidi ya Wachawi, uchawi na Masheitwani.

Soma Zaidi...
Hadithi ya tatu:ukarimu na kusaidiana

Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...