Adabu ya kukaa na kula katika nyumba za watu

Adabu ya kukaa na kula katika nyumba za watu

"Si vibaya kwa kipofu, wala si vibaya kwa kiguru, wala si vibaya kwa mgonjwa, wala kwenu, kama mkila katika nyumba zenu, au nyumba za baba zenu, au nyumba za mama zenu, au nyumba za ndugu zenu, au nyumba za dada zenu, au nyumba za ami zenu, au nyumba za s

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Adabu ya kukaa na kula katika nyumba za watu

(g) Adabu ya kukaa na kula katika nyumba za watu.


"Si vibaya kwa kipofu, wala si vibaya kwa kiguru, wala si vibaya kwa mgonjwa, wala kwenu, kama mkila katika nyumba zenu, au nyumba za baba zenu, au nyumba za mama zenu, au nyumba za ndugu zenu, au nyumba za dada zenu, au nyumba za ami zenu, au nyumba za shangazi zenu, au nyumba za wajomba zenu, au nyumba za dada wa mama zenu, au za wale mliowashikia funguo zao, au rafiki zenu. Si vibaya juu yenu kama mkila pamoja au mbali mbali. Na mnapoingia katika majumba toleaneni salamu; (maamkio haya) ni zawadi itokayo kwa Mwenyezi Mungu, yenye baraka, na mema. Hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu Anavyokubainishieni Aya (zake) ili mpate kufahamu." (24:61)



"Enyi mlioamini! Msiingie nyumba za Mtume ila mpewe ruhusa kwenda kula, pasipo (kwenda kukaa) kungojea kiivie. Lakini mtakkapoitwa ingieni, na mnapokwisha kula tawanyikeni. Wala msiweke mazungumzo, maana jambo hili linamuudhi Mtume, naye anakuoneeni haya; lakini Mwenyezi Mungu Haoni haya kusema haki. Nanyi mnapowauliza (wakeze) waulizeni nyuma ya pazia. Kufanya haya kutasafisha nyoyo zenu na nyoyo zao. Wala haikupasieni (haitakikani) kumuudhi Mtume wa Mwenyezi Mungu. Wala kuwaoa wake zake baada yake; kabisa. Hakika jambo hilo ni (dhambi) kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu. (33:53)
Tukizingatia aya hizi tunapata maelekezo ya kimaadili yafuatayo:



(i) Pamoja na kwamba Uislamu unahimiza ukarimu, haumuhusu kwa pande mmoja, kuingia na kula katika nyumba za watu pasi na mwaliko rasmi. Kuvamia chakula katika nyumba za watu ni kuvuruga utaratibu wa familia na kuleta kero, jambo ambalo halikubaliki katika Uislamu. Kwa upande mwingine, katika mafundisho ya Uislamu, akija mgeni asiyerami (mgeni wa kupita) asitoke bila ya kumkirimu chochote, angalau maji ya kunywa; naye apokee lakini ahakikishe kuwa hawakalifishi wenyeji wake.



(ii)Wanaoruhusika kula chakula watakacho kikuta ni wanafamilia wenyewe na jamaa wa karibu kama walivyotajwa katika aya (24:61). Marafiki walioainishwa katika aya hii ni wale marafiki wa ndani walioshibana na familia (rafiki ndugu).



(iii)Wengine wanaoruhusika kula chakula katika nyumba za watu bila mwaliko rasmi ni wagonjwa, vilema, na wengine walioathirika kiuchumi wanaotambulika kisheria na wanaohitajia msaada wa Waislamu.



(iv)Waislamu watakapopata mwaliko wa kwenda kula katika nyumba za watu, waje pale kwa wakati uliopangwa na baada ya kula waombe ruhusa ya kuondoka ili kuwapa wenyeji wao uhuru wa kufanya mambo yao mengine ya faragha (yanayohusu familia).




                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 960

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Sura za kujikinga na Uchawi na mashetani
Sura za kujikinga na Uchawi na mashetani

Post hii itakwenda kukufundisha sura katika Quran ambazo ni kinga dhidi ya Wachawi, uchawi na Masheitwani.

Soma Zaidi...
Haki za Muislamu kwa Muislamu mwenzie
Haki za Muislamu kwa Muislamu mwenzie

Katika makala hii utakwenda kujifunza kuhusu haki za Muislamu kwa Muislamu mwenzie

Soma Zaidi...
Dua sehemu 03
Dua sehemu 03

Zijuwe njia ambazo Allah hujibu Dua yako. Tambua kama umejibiwa dua yako au bodo, soma darsa za dua hapa.

Soma Zaidi...
Hadithi Ya 32: Kusiwe Na Kudhuriana Wala Kulipiza Dhara
Hadithi Ya 32: Kusiwe Na Kudhuriana Wala Kulipiza Dhara

الحديث الثاني والثلاثون "لا ضرر ولا ضرار" عَنْ أَبىِ سَعيدٍ سَعْدِ بْن مَالكِ بْن سِنَانٍ الْخُدريِّ رضي الله عنه  أَنَّ رَسُولَ اللّ?...

Soma Zaidi...
Dua Sehemu ya 02
Dua Sehemu ya 02

Zijuwe nyakati ambazo dua inakubaliwa kwa haraka zaidi. Zijuwe nyakati ambazo ukiomba dua hitakubaliwa.

Soma Zaidi...
DUA 113 - 126
DUA 113 - 126

DUA ZA WAKATI WA SHIDA Dua ya wakati wa taabu “LAA ILAAHA ILLA-LLAHUL-’ADHIMUL-HALIIMU.

Soma Zaidi...
UHAKIKI WA HADITHI
UHAKIKI WA HADITHI

Uhakiki wa Hadith za Mtume (s.

Soma Zaidi...