Dalili za kifua kikuu kwa watoto.
Posti hii inahusu zaidi dalili za kifua kikuu kwa watoto,ni Dalili ambazo ujitokeza kwa watoto pindi wanapopata Maambukizi ya kifua kikuu.
Dalili za kifua kikuu kwa watoto.
1.Kifua kikuu ni Ugonjwa unaowashambulia Watu wazima na watoto kwa hiyo Dalili uweza kupelekea a ila mtu mzima anaweza kujieleza wazi jinsi anavyojisikia kuliko mtoto kwa hiyo ili kujua Dalili za kifua kikuu kwa watoto tunapaswa kuangalia yafuatayo kwa watoto.
2. Mtoto kukosa raha au kulia lia.
Hii ni mojawapo ya Dalili ya kifua kikuu kwa watoto kwa sababu mtoto anakuwa anajisikia vibaya na hawezi kusema kwa hiyo ataonekana hana raha na kuanza kulia lia ingawa hii inaweza kuwa ni Dalili ya hata Magonjwa mengine lakini dalili hii ikiambatana na Dalili nyingine za kifua kikuu kama tutakavyoona ni kifua kikuu mtoto anapaswa kupelekwa hospitalini kwa uangalizi zaidi.
3.Kupungua uzito, au kutokuongezeka uzito.
Dalili nyingine ya kifua kikuu ni kupungua uzito kwa mtoto , tunajua wazi kubwa mtoto anapaswa kuongezeka uzito kila mwezi kama afya yake ni nzuri na hana ugonjwa ukiona uzito wa mtoto umeanza kupungua na hata kila mwezi haongezeki uzito hiyo ni Dalili ya kifua kikuu kwa mtoto kwa hiyo uchunguzi ni lazima.
4.Kikohozi kwa mda mrefu bila kupona.
Kuna kipindi ambapo watoto wanapata kikohozi lakini kikidumu kwa mda mrefu bila kupona na pakiwepo na dalili nyingine za kifua kikuu lazima mtoto apelekwe hospitali ili aweze kupimwa na kupata matibabu zaidi.
5.Homa kwa wiki mbili na zaidi.
Kuwepo kwa homa kwa wiki mbili na zaidi ni mojawapo ya Dalili ya kifua kikuu kwa mtoto kwa hiyo mama au mlezi baada ya kuona dalili kama hizi ya kuwepo kwa homa ambazo hazishi kwa mtoto ni lazima kumpeleka kwa mtoto kwa uangalizi zaidi.
6.Mtoto kudumaa au kutoonyesha maendeleo yoyote katika ukuaji na kubaki katika hali hiyo ikiongezea na kukonda
Hii ni Dalili kubwa ya kifua kikuu ambapo mtoto uonekana kama mwenye mambukizi ya virus vya ukimwi na kukua hakui kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa ni Dalili mojawapo ya kifua kikuu kwa mtoto kwa hiyo matibabu ni lazima.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 web hosting 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Njia za maambukizi ya Homa ya inni
Posti hii inahusu zaidi njia za maambukizi ya Homa ya inni, Homa ya inni usababishwa na virusi viitwavyo Hepatitis B, huwapata watu wote hasa wale wenye umri chini ya miaka mitano.
Soma Zaidi...Dalili za minyoo na sababu zake
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za minyoo na sababu zake
Soma Zaidi...Je maumivu juu ya kitovu ni miongoni mwa dalili za mimba?
Kama unahisi maumivu ya tumbo huwenda umejiuliza swali hili ukiwa kama mwanamke "Je maumivu juu ya kitovu ni miongoni mwa dalili za mimba?". Post hii inakwenda kujibu swali hili
Soma Zaidi...Matibabu kwa mtu mwenye kiungulia
Posti hii inahusu zaidi matibabu kwa mtu mwenye kiungulia,ni tiba ambayo mtu anapaswa kutumia kama ana tatizo la kiungulia
Soma Zaidi...Dalili za maambukizi kwenye figo
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Maambukizi kwenye figo (pyelonephritis) ni aina mahususi ya maambukizi ya njia ya mkojo (UTI) ambayo kwa kawaida huanza kwenye urethra au kibofu chako na kusafiri hadi kwenye figo zako.
Soma Zaidi...Msaada kwa Mgonjwa aliyeshindwa kupitisha mkojo.
Posti hii utokea huduma ya kwanza kwa mtu aliye na shida ya kushindwa kupitisha mkojo kutoka kwenye kibofu Cha mkojo,
Soma Zaidi...