picha

Dalili za kifua kikuu kwa watoto.

Posti hii inahusu zaidi dalili za kifua kikuu kwa watoto,ni Dalili ambazo ujitokeza kwa watoto pindi wanapopata Maambukizi ya kifua kikuu.

Dalili za kifua kikuu kwa watoto.

1.Kifua kikuu ni Ugonjwa unaowashambulia Watu wazima na watoto kwa hiyo Dalili uweza kupelekea a ila mtu mzima anaweza kujieleza wazi jinsi anavyojisikia kuliko mtoto kwa hiyo ili kujua Dalili za kifua kikuu kwa watoto tunapaswa kuangalia yafuatayo kwa watoto.

 

2. Mtoto kukosa raha au kulia lia.

Hii ni mojawapo ya Dalili ya kifua kikuu kwa watoto kwa sababu mtoto anakuwa anajisikia vibaya na hawezi kusema kwa hiyo ataonekana hana raha na kuanza kulia lia ingawa hii inaweza kuwa ni Dalili ya hata Magonjwa mengine lakini dalili hii ikiambatana na Dalili nyingine za kifua kikuu kama tutakavyoona ni kifua kikuu mtoto anapaswa kupelekwa hospitalini kwa uangalizi zaidi.

 

3.Kupungua uzito, au kutokuongezeka uzito.

Dalili nyingine ya kifua kikuu ni kupungua uzito kwa mtoto , tunajua wazi kubwa mtoto anapaswa kuongezeka uzito kila mwezi kama afya yake ni nzuri na hana ugonjwa ukiona uzito wa mtoto umeanza kupungua na hata kila mwezi haongezeki uzito hiyo ni Dalili ya kifua kikuu kwa mtoto kwa hiyo uchunguzi ni lazima.

 

4.Kikohozi kwa mda mrefu bila kupona.

Kuna kipindi ambapo watoto wanapata kikohozi lakini kikidumu kwa mda mrefu bila kupona na pakiwepo na dalili nyingine za kifua kikuu lazima mtoto apelekwe hospitali ili aweze kupimwa na kupata matibabu zaidi.

 

5.Homa kwa wiki mbili na zaidi.

Kuwepo kwa homa kwa wiki mbili na zaidi ni mojawapo ya Dalili ya kifua kikuu kwa mtoto kwa hiyo mama au mlezi baada ya kuona dalili kama hizi ya kuwepo kwa homa ambazo hazishi kwa mtoto ni lazima kumpeleka kwa mtoto kwa uangalizi zaidi.

 

6.Mtoto kudumaa au kutoonyesha maendeleo yoyote katika ukuaji na kubaki katika hali hiyo ikiongezea na kukonda 

Hii ni Dalili kubwa ya kifua kikuu ambapo mtoto uonekana kama mwenye mambukizi ya virus vya ukimwi na kukua hakui kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa ni Dalili mojawapo ya kifua kikuu kwa mtoto kwa hiyo matibabu ni lazima.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3724

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 ai web app     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Jinsi ya kujikinga na magonjwa ya zinaa (STIs).

Magonjwa ya zinaa, yanayojulikana pia kama STIs (Sexually Transmitted Infections), ni miongoni mwa changamoto kubwa za afya ya umma duniani. Kila mwaka, mamilioni ya watu hupata maambukizi mapya ya magonjwa haya, huku wengi wakikosa kutambua kuwa wameambukizwa kutokana na kutokuwa na dalili katika hatua za awali. Habari njema ni kwamba sehemu kubwa ya maambukizi ya magonjwa ya zinaa inaweza kuzuilika kwa kufuata mbinu sahihi za kinga na kufanya maamuzi salama kuhusu afya ya uzazi. Katika makala hii utajifunza maana ya magonjwa ya zinaa, namna yanavyoenea, sababu zinazoongeza hatari ya maambukizi, njia bora za kujikinga, umuhimu wa kupima afya mara kwa mara, pamoja na ukweli muhimu ambao kila mtu anapaswa kuufahamu kuhusu STIs.

Soma Zaidi...
Dalili za gonorrhea - gonoria

Jifunze dalili za gonorrhea na namna inavyoambukiza, zipi athari za gonori kwa wanawae na wanaume

Soma Zaidi...
Usingizi mzuri: Faida zake kiafya na jinsi ya kuupata.

Usingizi mzuri ni nguzo ya msingi ya afya ya binadamu, ikiwa na umuhimu sawa na lishe bora na mazoezi ya viungo. Katika ulimwengu wa sasa wenye shughuli nyingi, wengi wetu hupuuza umuhimu wa kupata usingizi wa kutosha. Makala haya yanachunguza faida za ajabu za usingizi kwa mwili na akili, pamoja na mbinu za kisayansi unazoweza kuzitumia ili kuhakikisha unapata mapumziko bora kila usiku.

Soma Zaidi...
Shinikizo la damu (High Blood Pressure): Sababu na vyakula vya kuepuka.

Shinikizo la damu (Hypertension) ni tatizo sugu la kiafya linaloathiri mamilioni ya watu duniani kote. Makala hii inachunguza kwa kina kiini cha shinikizo la damu, sababu zake kuu, na umuhimu wa lishe katika kudhibiti hali hii. Kwa kuelewa vyakula vya kuepuka na mabadiliko ya mtindo wa maisha, unaweza kulinda afya ya moyo wako na kuzuia madhara makubwa kama kiharusi na ugonjwa wa figo.

Soma Zaidi...
Pumu (Asthma): Dalili za mwanzo na jinsi ya kuepuka mashambulizi.

Pumu (Asthma) ni ugonjwa sugu wa njia ya hewa unaoathiri mamilioni ya watu duniani. Makala haya yanalenga kutoa ufahamu wa kina kuhusu dalili za mwanzo ambazo mara nyingi hupuuzwa, mazingira yanayochochea mashambulizi, na mikakati madhubuti ya kudhibiti ugonjwa huu. Kwa kufuata mwongozo huu, wagonjwa wanaweza kupunguza hatari ya mashambulizi ya ghafla na kuboresha ubora wa maisha yao.

Soma Zaidi...
je..! naweza kuambukizwa fangasi kwa kujamiiana na mtu mwenye fangasi?

Je ukifanya mapenz na mtu mweny aina hi ya fangasi na akawa anayo maambukizi ya ukimwi.

Soma Zaidi...