picha

Dalili za kifua kikuu kwa watoto.

Posti hii inahusu zaidi dalili za kifua kikuu kwa watoto,ni Dalili ambazo ujitokeza kwa watoto pindi wanapopata Maambukizi ya kifua kikuu.

Dalili za kifua kikuu kwa watoto.

1.Kifua kikuu ni Ugonjwa unaowashambulia Watu wazima na watoto kwa hiyo Dalili uweza kupelekea a ila mtu mzima anaweza kujieleza wazi jinsi anavyojisikia kuliko mtoto kwa hiyo ili kujua Dalili za kifua kikuu kwa watoto tunapaswa kuangalia yafuatayo kwa watoto.

 

2. Mtoto kukosa raha au kulia lia.

Hii ni mojawapo ya Dalili ya kifua kikuu kwa watoto kwa sababu mtoto anakuwa anajisikia vibaya na hawezi kusema kwa hiyo ataonekana hana raha na kuanza kulia lia ingawa hii inaweza kuwa ni Dalili ya hata Magonjwa mengine lakini dalili hii ikiambatana na Dalili nyingine za kifua kikuu kama tutakavyoona ni kifua kikuu mtoto anapaswa kupelekwa hospitalini kwa uangalizi zaidi.

 

3.Kupungua uzito, au kutokuongezeka uzito.

Dalili nyingine ya kifua kikuu ni kupungua uzito kwa mtoto , tunajua wazi kubwa mtoto anapaswa kuongezeka uzito kila mwezi kama afya yake ni nzuri na hana ugonjwa ukiona uzito wa mtoto umeanza kupungua na hata kila mwezi haongezeki uzito hiyo ni Dalili ya kifua kikuu kwa mtoto kwa hiyo uchunguzi ni lazima.

 

4.Kikohozi kwa mda mrefu bila kupona.

Kuna kipindi ambapo watoto wanapata kikohozi lakini kikidumu kwa mda mrefu bila kupona na pakiwepo na dalili nyingine za kifua kikuu lazima mtoto apelekwe hospitali ili aweze kupimwa na kupata matibabu zaidi.

 

5.Homa kwa wiki mbili na zaidi.

Kuwepo kwa homa kwa wiki mbili na zaidi ni mojawapo ya Dalili ya kifua kikuu kwa mtoto kwa hiyo mama au mlezi baada ya kuona dalili kama hizi ya kuwepo kwa homa ambazo hazishi kwa mtoto ni lazima kumpeleka kwa mtoto kwa uangalizi zaidi.

 

6.Mtoto kudumaa au kutoonyesha maendeleo yoyote katika ukuaji na kubaki katika hali hiyo ikiongezea na kukonda 

Hii ni Dalili kubwa ya kifua kikuu ambapo mtoto uonekana kama mwenye mambukizi ya virus vya ukimwi na kukua hakui kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa ni Dalili mojawapo ya kifua kikuu kwa mtoto kwa hiyo matibabu ni lazima.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3618

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 ai web app     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 web hosting     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto wadogo.

Posti inahusu zaidi madhara ya kaswende kwa mama mjamzito na mtoto, Ni ugonjwa unaopatikana hasa kwa njia ya kujamiiana na utoka kwa mwenye Ugonjwa kwenda kwa mtu ambaye hana ugonjwa, kwa hiyo tunapaswa kujua madhara ya ugonjwa huu kwa mama mjamzito na mt

Soma Zaidi...
Dalili za Ugonjwa wa mapafu.

posti hii inahusu dalili za ugonjwa wa mapafu.ambapo kitaalamu hujulikana Kama Ugonjwa wa Acute Respiratory Distress Syndrome (ARDS) hutokea wakati Majimaji yanapojaa kwenye vifuko vidogo vya hewa nyororo (alveoli) kwenye mapafu yako. Majimaji mengi kw

Soma Zaidi...
Namna ya kufanya usafi wa sikio

Post hii inahusu zaidi namna ya kufanya usafi wa sikio, sikio ni mojawapo ya ogani ambayo usaidia kusikia,kwa hiyo sikio linapaswa kusafishwa kwa uangalifu kama tutakavyoona hapo chini.

Soma Zaidi...
Ni Nini husababisha kukosa choo? (Constipation)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na sababu zinazopelekea kukosa choo ,yaani kinyesi kuwa kigumu au kukosa kabisa choo.

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa upele

Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa upele, ni dalili au mwonekano wa mgonjwa wa upele.

Soma Zaidi...