Dalili za kifua kikuu kwa watoto.
Posti hii inahusu zaidi dalili za kifua kikuu kwa watoto,ni Dalili ambazo ujitokeza kwa watoto pindi wanapopata Maambukizi ya kifua kikuu.
Dalili za kifua kikuu kwa watoto.
1.Kifua kikuu ni Ugonjwa unaowashambulia Watu wazima na watoto kwa hiyo Dalili uweza kupelekea a ila mtu mzima anaweza kujieleza wazi jinsi anavyojisikia kuliko mtoto kwa hiyo ili kujua Dalili za kifua kikuu kwa watoto tunapaswa kuangalia yafuatayo kwa watoto.
2. Mtoto kukosa raha au kulia lia.
Hii ni mojawapo ya Dalili ya kifua kikuu kwa watoto kwa sababu mtoto anakuwa anajisikia vibaya na hawezi kusema kwa hiyo ataonekana hana raha na kuanza kulia lia ingawa hii inaweza kuwa ni Dalili ya hata Magonjwa mengine lakini dalili hii ikiambatana na Dalili nyingine za kifua kikuu kama tutakavyoona ni kifua kikuu mtoto anapaswa kupelekwa hospitalini kwa uangalizi zaidi.
3.Kupungua uzito, au kutokuongezeka uzito.
Dalili nyingine ya kifua kikuu ni kupungua uzito kwa mtoto , tunajua wazi kubwa mtoto anapaswa kuongezeka uzito kila mwezi kama afya yake ni nzuri na hana ugonjwa ukiona uzito wa mtoto umeanza kupungua na hata kila mwezi haongezeki uzito hiyo ni Dalili ya kifua kikuu kwa mtoto kwa hiyo uchunguzi ni lazima.
4.Kikohozi kwa mda mrefu bila kupona.
Kuna kipindi ambapo watoto wanapata kikohozi lakini kikidumu kwa mda mrefu bila kupona na pakiwepo na dalili nyingine za kifua kikuu lazima mtoto apelekwe hospitali ili aweze kupimwa na kupata matibabu zaidi.
5.Homa kwa wiki mbili na zaidi.
Kuwepo kwa homa kwa wiki mbili na zaidi ni mojawapo ya Dalili ya kifua kikuu kwa mtoto kwa hiyo mama au mlezi baada ya kuona dalili kama hizi ya kuwepo kwa homa ambazo hazishi kwa mtoto ni lazima kumpeleka kwa mtoto kwa uangalizi zaidi.
6.Mtoto kudumaa au kutoonyesha maendeleo yoyote katika ukuaji na kubaki katika hali hiyo ikiongezea na kukonda
Hii ni Dalili kubwa ya kifua kikuu ambapo mtoto uonekana kama mwenye mambukizi ya virus vya ukimwi na kukua hakui kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa ni Dalili mojawapo ya kifua kikuu kwa mtoto kwa hiyo matibabu ni lazima.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 web hosting 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 ai web app 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Sababu za kuwepo kwa saratani ya inni.
Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali za kuwepo kwa saratani ya ini, saratani hii imekuwa tishio kwa wengi ila ni vizuri kujua baadhi ya sababu ambazo uchangia sana kuwepo kwa tatizo hili la saratani ya inni.
Soma Zaidi...Namna ya kujikinga na VVU/UKIMWI
Somo hili linakwenda kukueleza namna mbalimbali za kujikinga na VVU/UKIMWI
Soma Zaidi...Je utaweza kuambukiza HIV ukiwa unatumia PrEP?
Swali hili limeulizwa na mdau mmoja. Kuwa endapo mtu atafanya ngono zembe na akapata virusi je ataweza kuambukiza.
Soma Zaidi...Fangasi watambulikao kama invasive candidiasis
Hawa huweza kuingia kwenye mfumo wa damu na kuenda maeneo mengine nyeti sana ya mwili.
Soma Zaidi...MALARIA NI NINI? NI WATU WANGAPI WANAKUFA KWA MALARIA DUNIANI
Malaria ni katika maradhi yanayosumbua sana na kusababisha maradhi ya watu wengi sana duniani.
Soma Zaidi...Dalili za UTI upande wa wanawake
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za UTI upande wa wanawake
Soma Zaidi...