Fahamu kuhusu Ugonjwa wa pre - eclampsia
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa pre- eclampsia ni Ugonjwa ambao uwapata wanawake wajawazito uwapata pale mimba inapofikisha umri wa wiki ishilini, utokea pale ambapo Mama mjamzito huwa na kiwango kikubwa cha shinikizo la damu na pia kuwepo kwa protini
Fahamu kuhusu Ugonjwa wa pre- eclampsia.
1.Kama tulivyoona hapo juu kwamba Ugonjwa huu usababishwa na kuwepo kwa shinikizo la damu pamoja na protini kwenye mkojo,kwa hiyo tunapaswa kufahamu kwamba Mama kabla hajabeba mimba anakuwa hana tatizo hili lakini akibeba mimba ndipo mabadiliko utokea kwa mjamzito kwa hiyo Mama mwenye Tatizo hili anapaswa kuangaliwa kwa karibu zaidi ili aweze kufikia wakati wa kujifungua kwa usalama, na walio wengi wakijifungua matatizo ya aina hii uisha kabisa.
2.Kwa hiyo kuna aina mbili ya ugonjwa huu wa eclampsia, kuna eclampsia ya kawaida na isiyo ya kawaida, tunaweza kuzitambua kwa kutumia vipimo vya shinikizo la damu na kuipima kiwango cha protini kwenye mkojo.
3. Pre - eclampsia ya kawaida utokea kwa kupima presha ya chini ambayo kwa kitaalamu huitwa dystolic presha, kwa kawaida presha ya chini ya kawaida inapaswa kuanzia sitini mpaka tisini, ila kwa mgonjwa wa pre-eclampsia presha ya chini uanzia tisini na haizidi mia na kumi, na pia kiwango cha protini kwenye mkojo ufika 2+ kwa hiyo aina hizi kwa mgonjwa uweza kuonekana za kawaida ila mama anapaswa kutunzwa kwa uangalizi zaidi.
4. Aina ya pili ya pre-eclampsia. Nia pale ambapo shinikizo la damu yaani presha ya juu na chini huwa juu, ambapo presha ya chini uanzia mia na kumi na ya juu ufika mia sitini na kuendelea, tunajua wazi kuwa presha ya juu uanzia mia ishirini na kuisha mua arobaini ikizidi hapo sio ya kawaida, kwa hiyo Mama wa hivi anapaswa kuwa na uangalizi wa karibu kutoka kwa wahudumu wa afya ili aweze kuepuka kuwepo kwa kifafa cha Mimba.
5.Kwa hiyo baada ya kujua hayo tunapaswa kuwahi kwenda kliniki mara tu ugunduapo uko mja mzito kwa sababu ya kuchukua vipimo mbalimbali ili kuweza kuokoa Maisha ya Mama na mtoto, na jamii inapaswa kuepukana mila na destory zinazoweza kufanya tatizo likawa kubwa kwa sababu ya kwenda kwa waganga na kusababisha madhara yasiyo tarajiwa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Hali ya wasiwasi (Anxiety): Dalili na jinsi ya kuishinda.
Hali ya wasiwasi (anxiety) ni sehemu ya maisha ya binadamu, lakini inapogeuka kuwa tatizo sugu, huathiri vibaya ustawi wa kimwili na kiakili. Makala hii inachunguza kwa kina maana ya wasiwasi, dalili zake za kimwili na kisaikolojia, sababu zake, na mikakati ya kisayansi ya kuishinda. Lengo ni kutoa mwongozo wa kitaalamu utakaomsaidia msomaji kutambua hali hii na kuchukua hatua za kimatibabu na kitabia ili kurejesha utulivu wa maisha.
Soma Zaidi...Sababu za Kutokwa Damu moja kwa moja bila kuganda (hemophilia).
Posti hii inaelezea kuhusiana na Damu kutokuganda ambalo hujulikana Kama Hemophilia, ni ugonjwa nadra ambapo damu yako haigandi kawaida kwa sababu haina protini za kutosha za kuganda. Ikiwa una tatizo la Damu kutokuganda, unaweza kuvuja damu kwa muda mre
Soma Zaidi...Je vvu inaweza sababisha mate kujaa mdomoni
Je kujaa kwa mate mdomoni ni dalili ya kuwa na VVU, na je ni zipi dalili za Virusi Vya Ukimwi (VVU) mdomoni?
Soma Zaidi...Dalili za macho kuwa makavu
posti hii inaelezea kuhusiana na dalilili na Mambo ya hatari ya Macho makavu hutokea wakati machozi yako hayawezi kutoa unyevu wa kutosha kwa macho yako. Machozi yanaweza kuwa duni kwa sababu nyingi. Kwa mfano, Macho makavu yanaweza ku
Soma Zaidi...Dalili za HIV kwa Mwanamke Mjamzito
Makala haya yanalenga kutoa uelewa muhimu kuhusu virusi vya UKIMWI (HIV) na ujauzito. Tutachunguza dalili zinazoweza kujitokeza, umuhimu wa upimaji wa mapema kwa afya ya mama na mtoto, na jinsi ya kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto (PMTCT).
Soma Zaidi...Watu walio hatarini kupata ugonjwa wa pumu
Kila mtu anaweza kupata ugonjwa wa pumu, hata hivyo kuna ambao wapo hatarini zaidi kupata pumu.
Soma Zaidi...