Namna ya kutibu kuharisha kwa mtoto ukiwa nyumbani.
Post hii inahusu zaidi njia za kutibu kuharisha kwa watoto wakiwa nyumbani, kwa sababu mara nyingine mtoto anaweza kuharisha si kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi ila ni uchafu tu kwa hiyo njia muhimu zinazofaa kutibu mtoto ni pamoja na yafuatayo.
Njia za kutibu au kuzuia kuharisha wakiwa nyumbani,
1.Kwanza kabisa tunajua kuwa watoto wanaweza kupata matatizo mbalimbali ya kiafya hasa kuharisha ambapo wasipotibiwa mapema wanaweza kupoteza maji mwilini na kusababisha madhara makubwa kwa hiyo ikitokea mtoto akaanza kuharisha fanya yafuatayo.
2. Mpatie mtoto vitu mbalimbali vya majimaji.
Vitu vya majimaji kama vile kumnyonyesha mtoto mara kwa mara kumpatia mtoto Oral solution au unaweza kumpatia maji masafi, kumpatia vyakula vya majimaji kama supu, maji ya mchele, maziwa,na kama mtoto hajafikia wakati wa kula unampatia mda mwingi wa kunyonya.
3. Wakati wa kumlisha mtoto unapaswa kumpa kidogo kidogo kwenye kijiko na pia ukiona anatapika unapaswa kumpumzisha mpaka dakika kumi zipite na endelea kumpa vitu vya maji maji mpaka kuharisha kuishe ila hali ya kuharisha ikiendelea mpeleke mgonjwa hospitalini kwa matibabu zaidi.
4. Mpatie mtoto zink
Zink anapaswa kutumia mtoto mwenye umri wa kuanzia miezi miwili mpaka mwaka mmoja , mtoto wa miezi miwili mpaka miezi sita wanapaswa kutumia wanapaswa kutumia nusu ya kidonge mpaka siku kumi na nne na kuanzia miezi sita mpaka na kuendelea wanapaswa kutumia kidonge kimoja kwa siku kumi na nne.
5.Kwa hiyo pamoja na kutumia tiba hii ikifanikiwa utaendelea kuitumia isipofanikiwa basi mtoto anapaswa kupelekwa hospitalini na kupata matibabu kwa sababu mtoto akiishiwa maji mwilini ni shida na tunaweza kupata matatizo mengine makubwa
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 web hosting 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Mwanamke mwenye HIV akiwa mjamzito ama ananyonyesha
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mwanamke mwenye HIV akiwa mjamzito ama anaenyonyesha
Soma Zaidi...Je? Naomba kuuliza mkewangu ali ingiya kwenye hezi siku tatu damu ikakata nikakutana nae siku ya nane je? Anaweza pata ujauzito
Idadi ya siku hatari za kupata mimba hutofautiana kutoka kwa mwanamke mmoja namwinhine. Kinda ambao idadivyavsikuvzao za hatari ni nyingi kuliko wengine.
Soma Zaidi...Fahamu madhara ya Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke PID
Posti hii inazungumzia kuhusiana na mathara yanayosababisha Ugonjwa wa Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke
Soma Zaidi...Dalili za mimba changa
Zijuwe dalili 17 za mimba na mimba changa, kuanzia siku ya kwanza mpaka mwezi mmoja
Soma Zaidi...Fahamu mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa
Posti hii inahusu zaidi mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa, kwa kawaida tunajua kwamba mtoto wakati wa kuzaliwa ni lazima atangulize kichwa ila Kuna kipindi mtoto anatanguliza matako, kuna aina nne za mtoto kutanguliza matako.
Soma Zaidi...