picha

Namna ya kutibu kuharisha kwa mtoto ukiwa nyumbani.

Post hii inahusu zaidi njia za kutibu kuharisha kwa watoto wakiwa nyumbani, kwa sababu mara nyingine mtoto anaweza kuharisha si kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi ila ni uchafu tu kwa hiyo njia muhimu zinazofaa kutibu mtoto ni pamoja na yafuatayo.

Njia za kutibu au kuzuia kuharisha wakiwa nyumbani,

1.Kwanza kabisa tunajua kuwa watoto wanaweza kupata matatizo mbalimbali ya kiafya hasa kuharisha ambapo wasipotibiwa mapema wanaweza kupoteza maji mwilini na kusababisha madhara makubwa kwa hiyo ikitokea mtoto akaanza kuharisha fanya yafuatayo.

 

2. Mpatie mtoto vitu mbalimbali vya majimaji.

Vitu vya majimaji kama vile kumnyonyesha mtoto mara kwa mara kumpatia mtoto Oral solution au unaweza kumpatia maji masafi, kumpatia vyakula vya majimaji kama supu, maji ya mchele, maziwa,na kama mtoto hajafikia wakati wa kula unampatia mda mwingi wa kunyonya.

 

3. Wakati wa kumlisha mtoto unapaswa kumpa kidogo kidogo kwenye kijiko na pia ukiona anatapika unapaswa kumpumzisha mpaka dakika kumi zipite na endelea kumpa vitu vya maji maji mpaka kuharisha kuishe ila hali ya kuharisha ikiendelea mpeleke mgonjwa hospitalini kwa matibabu zaidi.

 

4. Mpatie mtoto zink 

Zink anapaswa kutumia mtoto mwenye umri wa kuanzia miezi miwili mpaka mwaka mmoja , mtoto wa miezi miwili mpaka miezi sita wanapaswa kutumia wanapaswa kutumia nusu ya kidonge mpaka siku kumi na nne na kuanzia miezi sita mpaka na kuendelea wanapaswa kutumia kidonge kimoja kwa siku kumi na nne.

 

5.Kwa hiyo pamoja na kutumia tiba hii ikifanikiwa utaendelea kuitumia isipofanikiwa basi mtoto anapaswa kupelekwa hospitalini na kupata matibabu kwa sababu mtoto akiishiwa maji mwilini ni shida na tunaweza kupata matatizo mengine makubwa

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 18922

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 ai web app     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

tuseme nilifanya ngono jana na leo nipata period,je kuna uwezekano wa kupata mimba

Mimba inatungwa katika siku maalumu na hazizidi 10. Sio kila ukishiriki tendo unaweza pata mimba. Je unaweza kupata mimba baada ya kushiriki tendo wiki moja kabla ya kuingia hedhi?

Soma Zaidi...
Sababu za mama kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua.

Posti hii inahusu zaidi sababu za mama kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua, hili ni tatizo ambalo uwapata akina Mama wengi wanapomaliza kujifungua kwa hiyo tutaweza kuziona sababu zinazosababishwa na tatizo hili.

Soma Zaidi...
Je mwanamke anaweza pata mimba ikiwa wakati watendo la ndoa hakukojoa Wala kusikia raha yoyote ya sex wakati watendo landoa

Je wewe ni mwanmake unayepata shida kufika kileleni? (Kukojoa wakati wa tendo lwa ndoa). Post hii itakujibu baadhi ya maswali yako.

Soma Zaidi...
Huduma kwa mama ambaye mimba imetoka moja kwa moja.

Post hii inahusu zaidi huduma kwa mama ambaye mimba imetoka moja kwa moja, aina hiyo ya mimba kwa kitaalamu huitwa complete abortion.

Soma Zaidi...
Mabadiliko ya mzunguko wa damu kwa wajawazito.

Posti hii inahusu zaidi mabadiliko ya mzunguko wa damu kwa wajawazito, tunajua wazi kuwa wajawazito pindi ujauzito ukiingia tu, kila kitu kwenye mwili ubadilika vile vile na mzunguko wa damu ubadilika.

Soma Zaidi...