Namna ya kutibu kuharisha kwa mtoto ukiwa nyumbani.
Post hii inahusu zaidi njia za kutibu kuharisha kwa watoto wakiwa nyumbani, kwa sababu mara nyingine mtoto anaweza kuharisha si kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi ila ni uchafu tu kwa hiyo njia muhimu zinazofaa kutibu mtoto ni pamoja na yafuatayo.
Njia za kutibu au kuzuia kuharisha wakiwa nyumbani,
1.Kwanza kabisa tunajua kuwa watoto wanaweza kupata matatizo mbalimbali ya kiafya hasa kuharisha ambapo wasipotibiwa mapema wanaweza kupoteza maji mwilini na kusababisha madhara makubwa kwa hiyo ikitokea mtoto akaanza kuharisha fanya yafuatayo.
2. Mpatie mtoto vitu mbalimbali vya majimaji.
Vitu vya majimaji kama vile kumnyonyesha mtoto mara kwa mara kumpatia mtoto Oral solution au unaweza kumpatia maji masafi, kumpatia vyakula vya majimaji kama supu, maji ya mchele, maziwa,na kama mtoto hajafikia wakati wa kula unampatia mda mwingi wa kunyonya.
3. Wakati wa kumlisha mtoto unapaswa kumpa kidogo kidogo kwenye kijiko na pia ukiona anatapika unapaswa kumpumzisha mpaka dakika kumi zipite na endelea kumpa vitu vya maji maji mpaka kuharisha kuishe ila hali ya kuharisha ikiendelea mpeleke mgonjwa hospitalini kwa matibabu zaidi.
4. Mpatie mtoto zink
Zink anapaswa kutumia mtoto mwenye umri wa kuanzia miezi miwili mpaka mwaka mmoja , mtoto wa miezi miwili mpaka miezi sita wanapaswa kutumia wanapaswa kutumia nusu ya kidonge mpaka siku kumi na nne na kuanzia miezi sita mpaka na kuendelea wanapaswa kutumia kidonge kimoja kwa siku kumi na nne.
5.Kwa hiyo pamoja na kutumia tiba hii ikifanikiwa utaendelea kuitumia isipofanikiwa basi mtoto anapaswa kupelekwa hospitalini na kupata matibabu kwa sababu mtoto akiishiwa maji mwilini ni shida na tunaweza kupata matatizo mengine makubwa
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Sababu za kupata hedhi zaidi ya mara moja kwa mwezi mmoja
Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa hedhi zaidi ya mara moja kwa mwezi mmoja, mara nyingi kuna Watu ambao huwa wanalalamika kwa sababu ya kupata hedhi za mara kwa mara kwa mwezi mmoja.
Soma Zaidi...Mke Wang Ana tatizo la tumbo kuuma chini upande wa kushoto akishika ni pagumu ,anapatwa na kichefuchef tumbo kujaa ges na kujiisi kusiba he mtanisaidije ili kuondoa tatizo Hilo Ila anaujauzito wa wiki mbili
Miongoni mwa changamoto za ujauzito ni maumivu ya tumbo. Maumivu haya yanawezakuwaya kawaida ama makali zaidi. Vyema kufika Kituo cha Afya endapoyatakuwa makali.
Soma Zaidi...Vyakula vinavyosaidia katika uzalishaji wa homoni ya testosterone
Posti hii inahusu zaidi vyakula ambavyo usaidia katika uzalishaji wa homoni ya testosterone.
Soma Zaidi...Maji ya Amniotic
Posti hii inahusu zaidi maji ya Amniotic ni maji ambayo uzunguka mtoto na kufanya kazi mbalimbali kama ifuayavyo.
Soma Zaidi...Uhusiano uliopo kati ya Mama Mjamzito na kibofu cha mkojo.
Posti hii inahusu zaidi uhusiano uliopo kati ya Mama Mjamzito na kibofu cha mkojo.ni mwingiliano unaokuwepo ambao usababisha Mama kukojoa sana wakati wa ujauzito.
Soma Zaidi...