picha

Namna ya kutibu kuharisha kwa mtoto ukiwa nyumbani.

Post hii inahusu zaidi njia za kutibu kuharisha kwa watoto wakiwa nyumbani, kwa sababu mara nyingine mtoto anaweza kuharisha si kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi ila ni uchafu tu kwa hiyo njia muhimu zinazofaa kutibu mtoto ni pamoja na yafuatayo.

Njia za kutibu au kuzuia kuharisha wakiwa nyumbani,

1.Kwanza kabisa tunajua kuwa watoto wanaweza kupata matatizo mbalimbali ya kiafya hasa kuharisha ambapo wasipotibiwa mapema wanaweza kupoteza maji mwilini na kusababisha madhara makubwa kwa hiyo ikitokea mtoto akaanza kuharisha fanya yafuatayo.

 

2. Mpatie mtoto vitu mbalimbali vya majimaji.

Vitu vya majimaji kama vile kumnyonyesha mtoto mara kwa mara kumpatia mtoto Oral solution au unaweza kumpatia maji masafi, kumpatia vyakula vya majimaji kama supu, maji ya mchele, maziwa,na kama mtoto hajafikia wakati wa kula unampatia mda mwingi wa kunyonya.

 

3. Wakati wa kumlisha mtoto unapaswa kumpa kidogo kidogo kwenye kijiko na pia ukiona anatapika unapaswa kumpumzisha mpaka dakika kumi zipite na endelea kumpa vitu vya maji maji mpaka kuharisha kuishe ila hali ya kuharisha ikiendelea mpeleke mgonjwa hospitalini kwa matibabu zaidi.

 

4. Mpatie mtoto zink 

Zink anapaswa kutumia mtoto mwenye umri wa kuanzia miezi miwili mpaka mwaka mmoja , mtoto wa miezi miwili mpaka miezi sita wanapaswa kutumia wanapaswa kutumia nusu ya kidonge mpaka siku kumi na nne na kuanzia miezi sita mpaka na kuendelea wanapaswa kutumia kidonge kimoja kwa siku kumi na nne.

 

5.Kwa hiyo pamoja na kutumia tiba hii ikifanikiwa utaendelea kuitumia isipofanikiwa basi mtoto anapaswa kupelekwa hospitalini na kupata matibabu kwa sababu mtoto akiishiwa maji mwilini ni shida na tunaweza kupata matatizo mengine makubwa

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 18491

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Bongolite - Game zone - Play free game     πŸ‘‰2 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰5 ai web app     πŸ‘‰6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Njia za uzazi wa mpango kwa akina Mama kuanzia miezi sita baada ya kujifungua mpaka mwaka mmoja

Posti hii inahusu zaidi njia za uzazi wa mpango kwa mama aliyejifungua kuanzia miezi sita mpaka mwaka mmoja.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusiana na kubalehe kwa msichana na mvulana.

Kubalehe ni wakati mwili wa mtoto unapoanza kubadilika na kuwa wa mtu mzima (balehe) hivi karibuni. Kubalehe ambao huanza kabla ya umri wa miaka 8 kwa wasichana na kabla ya umri wa miaka 9 kwa wavulana.

Soma Zaidi...
Kuwepo kwa mabonge ya damu wakati wa hedhi

Posti hii inahusu zaidi kuwepo kwa mabonge ya damu wakati wa hedhi, tunajua kabisa wakati wa hedhi damu inapaswa kuwa nyepesi na ya kawaida ila kuna wakati mwingine inakuwa na mabonge zifuatazo ni sababu za kuwepo kwa mabonge ya damu wakati wa hedhi.

Soma Zaidi...
Dalili za mimba ya mtoto wa kiume ama mtoto wa kike

Posti hii inakwenda kukueleza jinsi ya kuwjuwa kama mtoto ni wa kike ama wa kiume.

Soma Zaidi...
mambo ambayo utaulizwa mama mjamzito ukifika kituo cha afya unatakiwa utoe majibu sahihi.

Posti hii inahusu zaidi mambo ambayo Mama mjamzito anaweza kuulizwa pindi anapokuja kwenye kliniki ya uzazi ,ni mambo muhimu na ya lazima yanayopaswa kuongea na Mama mjamzito ili kuweza kuona maendeleo yake kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...