picha

Dalili za ugonjwa wa ngiri

Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo mgonjwa wa ngiri anaweza kuzipata, kwa hiyo baada ya kusoma na kuelewa dalili hizi mgonjwa anapaswa kuwahi hospitali mapema kwa ajili ya kupata matibabu.

Dalili za ugonjwa wa ngiri.

1​​​​​​. Kwanza kabisa tunajua kuwa ugonjwa wa ngiri utokea pale ambapo misuli au kuta za tishu mwilini ambazo ushikilia au kubeba viungo fulani mwilini kupoteza uimara wake au kubwa na uwazi na kufanya viungo hivyo kutoshikilia vizuri katika sehemu inayostahili hali ambayo Usababisha mtu kuhisi maumivu na pengine kuwepo kwa uwazi  katika sehemu mbalimbali za mwili hali ambayo Usababisha nyama kuota na kuelekea kwenye sehemu hizo za uwazi. 

 

2.Kuna Dalili mbalimbali ambazo ujitokeza iwapo  mtu amepata tatizo hili na dalili hizi utofautiana kutoka kwa mtu mmoja na mwingine kwa sababu ugonjwa huu ushika sehemu tofauti kama vile kwenye kifua, kwenye kitovu na kwenye mshipa wa ngiri na pengine kwa sababu ya upasuaji kwa hiyo Dalili utofautiana kulingana na Ugonjwa umeshika sehemu ipi.

 

3. Mtu mwenye tatizo la ngiri anaweza kubanwa na tumbo hasa chini ya kitovu wakati wa baridi na pengine pale anapokuwa ameshiba au amekula vitu vitamu, hiyo huwa ni dalili ya ngiri ya kitovu kwa walio wengi.

 

4. Kupinga mingurumo tumboni.

Kwa kawaida ngiri nyingi ili kutokea uanzia kwenye tumbo ambapo sehemu ya utumbo inaota kuelekea kwenye uwazi fulani inawezekana kwenye kifua au na sehemu mbalimbali za mwili ambapo ngiri inaweza kutokea kwa hiyo hali hii usababisha mingurumo kutokea kwenye tumbo.

 

5. Kuhisi una haja kubwa na ukifika chooni unatoa gesi tu, kwa hiyo kama kuna tatizo hili la ngiri tumbo ukaa na  gesi sana ,hii ni kwa sababu ya hali ya tumbo kutokuwa kwenye hali yake ya kawaida.

 

6. Kukaa siku kadhaa bila kupata haja kubwa , inawezekana kwa siku kama mbili au zaidi bila kuwepo kwa choo, au ukibatiwa kupata choo ni kidogo sana na huwa kama choo ya mbuzi.

 

7. Pengine Mgonjwa anakwenda haja mara kwa mara, hasa anakuwa anahisi haja kubwa na akienda uko ni gesi na choo kidogo hali hiyo usumbua sana na kufikia kiasi cha mgonjwa kukaa karibu na choo na hatoi kitu cha maana.

 

8. Kupotea kwa nuru ya macho.

Mara nyingine kuna wagonjwa ambao nuru za macho upotea, ila hali hii utokea kwa mara chache sana na sio kupotea kwa nuru ni tatizo la ngiri kwa hiyo mgonjwa anapaswa kupima kwanza ili kujua tatizo ni nini.

 

9. Maumivu makubwa ya mgongo na kiuno.

Kuna wagonjwa wengine wanahisi kuwa na maumivu makali ya mgongo na kiuno na pengine hali inaweza kufikia kiasi kwamba Mgonjwa anashindwa kutembea, kwa hiyo ni vizuri kupima haraka na kugundua tatizo ni lipi.

 

10. Makende kuwa kwenye sehemu moja.

Kuna wakati mwingine makende yote yanakuwa kwenye sehemu moja kwa hiyo ni vizuri kujua Dalili hii ili kuweza kutibu na pengine mgonjwa anahisi maumivu makali sana kwenye sehemu za siri hasa kwa wanaume.

 

11.Pamoja na kujua Dalili zote za ngiri ni vizuri kabisa kujua kuwa sio Dalili zote ni za kuwepo kwa ngiri kwa hiyo vipimo ni lazima na kuwaona wataalamu wa afya ni jambo la muhimu sana ili kuweza kugundua kuwae ni tatizo gani kwa sababu kuna Magonjwa mbalimbali ambayo yana Dalili kama hizi.

 

12.Pia tunapaswa kutoa wito kwa jamii kuwa ugonjwa wa ngiri upo na unatibika kwa hiyo elimu inapaswa kutolewa kwa jamii ili kuepuka hali ya kuwaficha wagonjwa wakiwa na umani kuwa ni magonjwa ya zinaa na kuona kuwa ni aibu kwa familia na kuwatibu wagonjwa ki mila hali inayosababisha kuongezeka kwa maumivu na tatizo kubwa kubwa zaidi.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 5830

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 web hosting     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Je unazijuwa dalili za Ukimwi na HIV?

Huwenda ukawa ni moja kati ya watu wanaotaka kujuwa juu ya dalili za ukimwi. Kama wewe ni katika watu hawa tambuwa kuwa kuna dalili za VVU (hiv) na dalili za ukimwi. Makala hii itakwenda kukuletea dalili kuu za mwanzo za VVU na HIV kuanzia wiki tatu za mw

Soma Zaidi...
Ishara na dalilili za Mtoto mwenye kuhara

postii hii inazungumzia dalilili za Mtoto mwenye Kuhara. Kuhara maana yake ni kutokwa na kinyesi chenye maji matatu au zaidi, pamoja na au bila damu ndani ya masaa 24. Kuhara kunaweza kusababishwa na maambukizo ya bakteria na virusi, ugonjwa wa matumb

Soma Zaidi...
Presha ya kushuka na matibabu yake

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu presha ya kushuka na matibabu yake

Soma Zaidi...
Yajue magonjwa ya jicho

Posti hii inahusu zaidi Magonjwa ya jicho,ni Magonjwa ambayo ushambulia sehemu mbalimbali za jicho kwa mfano kwenye retina,kuaribu mishipa ya retina ,macho kuwa makavu na pia mtoto wa jicho, hali hii ya magonjwa ya macho Usababisha madhara mbalimbali kama

Soma Zaidi...
Njia za kupunguza ugonjwa wa zinaa

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo zinaweza kutumika Ili kuweza kupunguza kuwepo kwa magonjwa ya zinaa

Soma Zaidi...
Aina za ajali kwenye kifua,

Post hii inahusu Zaidi aina za ajali kwenye kifua,pamoja na kifua kuwa na sehemu mbalimbali na pia na ajali ambazo utokea Huwa za aina mbalimbali kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...