picha

Dalili za ugonjwa wa ngiri

Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo mgonjwa wa ngiri anaweza kuzipata, kwa hiyo baada ya kusoma na kuelewa dalili hizi mgonjwa anapaswa kuwahi hospitali mapema kwa ajili ya kupata matibabu.

Dalili za ugonjwa wa ngiri.

1​​​​​​. Kwanza kabisa tunajua kuwa ugonjwa wa ngiri utokea pale ambapo misuli au kuta za tishu mwilini ambazo ushikilia au kubeba viungo fulani mwilini kupoteza uimara wake au kubwa na uwazi na kufanya viungo hivyo kutoshikilia vizuri katika sehemu inayostahili hali ambayo Usababisha mtu kuhisi maumivu na pengine kuwepo kwa uwazi  katika sehemu mbalimbali za mwili hali ambayo Usababisha nyama kuota na kuelekea kwenye sehemu hizo za uwazi. 

 

2.Kuna Dalili mbalimbali ambazo ujitokeza iwapo  mtu amepata tatizo hili na dalili hizi utofautiana kutoka kwa mtu mmoja na mwingine kwa sababu ugonjwa huu ushika sehemu tofauti kama vile kwenye kifua, kwenye kitovu na kwenye mshipa wa ngiri na pengine kwa sababu ya upasuaji kwa hiyo Dalili utofautiana kulingana na Ugonjwa umeshika sehemu ipi.

 

3. Mtu mwenye tatizo la ngiri anaweza kubanwa na tumbo hasa chini ya kitovu wakati wa baridi na pengine pale anapokuwa ameshiba au amekula vitu vitamu, hiyo huwa ni dalili ya ngiri ya kitovu kwa walio wengi.

 

4. Kupinga mingurumo tumboni.

Kwa kawaida ngiri nyingi ili kutokea uanzia kwenye tumbo ambapo sehemu ya utumbo inaota kuelekea kwenye uwazi fulani inawezekana kwenye kifua au na sehemu mbalimbali za mwili ambapo ngiri inaweza kutokea kwa hiyo hali hii usababisha mingurumo kutokea kwenye tumbo.

 

5. Kuhisi una haja kubwa na ukifika chooni unatoa gesi tu, kwa hiyo kama kuna tatizo hili la ngiri tumbo ukaa na  gesi sana ,hii ni kwa sababu ya hali ya tumbo kutokuwa kwenye hali yake ya kawaida.

 

6. Kukaa siku kadhaa bila kupata haja kubwa , inawezekana kwa siku kama mbili au zaidi bila kuwepo kwa choo, au ukibatiwa kupata choo ni kidogo sana na huwa kama choo ya mbuzi.

 

7. Pengine Mgonjwa anakwenda haja mara kwa mara, hasa anakuwa anahisi haja kubwa na akienda uko ni gesi na choo kidogo hali hiyo usumbua sana na kufikia kiasi cha mgonjwa kukaa karibu na choo na hatoi kitu cha maana.

 

8. Kupotea kwa nuru ya macho.

Mara nyingine kuna wagonjwa ambao nuru za macho upotea, ila hali hii utokea kwa mara chache sana na sio kupotea kwa nuru ni tatizo la ngiri kwa hiyo mgonjwa anapaswa kupima kwanza ili kujua tatizo ni nini.

 

9. Maumivu makubwa ya mgongo na kiuno.

Kuna wagonjwa wengine wanahisi kuwa na maumivu makali ya mgongo na kiuno na pengine hali inaweza kufikia kiasi kwamba Mgonjwa anashindwa kutembea, kwa hiyo ni vizuri kupima haraka na kugundua tatizo ni lipi.

 

10. Makende kuwa kwenye sehemu moja.

Kuna wakati mwingine makende yote yanakuwa kwenye sehemu moja kwa hiyo ni vizuri kujua Dalili hii ili kuweza kutibu na pengine mgonjwa anahisi maumivu makali sana kwenye sehemu za siri hasa kwa wanaume.

 

11.Pamoja na kujua Dalili zote za ngiri ni vizuri kabisa kujua kuwa sio Dalili zote ni za kuwepo kwa ngiri kwa hiyo vipimo ni lazima na kuwaona wataalamu wa afya ni jambo la muhimu sana ili kuweza kugundua kuwae ni tatizo gani kwa sababu kuna Magonjwa mbalimbali ambayo yana Dalili kama hizi.

 

12.Pia tunapaswa kutoa wito kwa jamii kuwa ugonjwa wa ngiri upo na unatibika kwa hiyo elimu inapaswa kutolewa kwa jamii ili kuepuka hali ya kuwaficha wagonjwa wakiwa na umani kuwa ni magonjwa ya zinaa na kuona kuwa ni aibu kwa familia na kuwatibu wagonjwa ki mila hali inayosababisha kuongezeka kwa maumivu na tatizo kubwa kubwa zaidi.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 6028

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Bongolite - Game zone - Play free game     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zinazofanana:

Ugonjwa wa upungufu wa maji mwilini.

Upungufu wa maji mwilini hutokea unapotumia au kupoteza Majimaji mengi zaidi ya unayonywa, na mwili wako hauna maji ya kutosha na Majimaji mengine ya kufanya kazi zake za kawaida. Usipochukua nafasi ya Vimiminika vilivyopotea, utapungukiwa na maji.

Soma Zaidi...
Dalili za Mgonjwa wa kisukari

Post hii inahusu dalili za mtu Mwenye ugonjwa wa kisukari, dalili hizi zinaweza kujitokeza Moja kwa Moja mtu akagundua kuwa ana Ugonjwa wa kisukari.zifuatazo ni dalili za ugonjwa wa kisukari.

Soma Zaidi...
Sababu za vidonda kwenye uume

Vidonda kwenye uume vinaweza kusababishwa na maambukizi ya magonjwa ya zinaa (STIs) kama kaswende na herpes, maambukizi ya fangasi au bakteria, majeraha madogo, mzio (allergy), au usafi duni. Uchunguzi wa kitabibu ni muhimu ili kutambua chanzo na kupata tiba sahihi.

Soma Zaidi...
Dalili za Saratani ya utumbo mdogo.

Posti hii inaonyesha ishara na dalili za Saratani ya utumbo mdogo

Soma Zaidi...
Nini hasa chanzo cha pumu, na je inarithiwa?

Ugonjwa wa pumu ni moja katika magonjwa hatari yanayoweza kutokea kwa ghafla, na endapo itacheleweshwa kudhibitiwa inaweza sababisha athari mbaya zaidi

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa macho.

Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa macho, ugonjwa huu kwa kawaida una dalili kuu tano kadri ya maambukizi yanavyoongezeka na madhara yake kwa hiyo tunapaswa kujua dalili hizo Kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...