Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo mgonjwa wa ngiri anaweza kuzipata, kwa hiyo baada ya kusoma na kuelewa dalili hizi mgonjwa anapaswa kuwahi hospitali mapema kwa ajili ya kupata matibabu.
1​​​​​​. Kwanza kabisa tunajua kuwa ugonjwa wa ngiri utokea pale ambapo misuli au kuta za tishu mwilini ambazo ushikilia au kubeba viungo fulani mwilini kupoteza uimara wake au kubwa na uwazi na kufanya viungo hivyo kutoshikilia vizuri katika sehemu inayostahili hali ambayo Usababisha mtu kuhisi maumivu na pengine kuwepo kwa uwazi katika sehemu mbalimbali za mwili hali ambayo Usababisha nyama kuota na kuelekea kwenye sehemu hizo za uwazi.
2.Kuna Dalili mbalimbali ambazo ujitokeza iwapo mtu amepata tatizo hili na dalili hizi utofautiana kutoka kwa mtu mmoja na mwingine kwa sababu ugonjwa huu ushika sehemu tofauti kama vile kwenye kifua, kwenye kitovu na kwenye mshipa wa ngiri na pengine kwa sababu ya upasuaji kwa hiyo Dalili utofautiana kulingana na Ugonjwa umeshika sehemu ipi.
3. Mtu mwenye tatizo la ngiri anaweza kubanwa na tumbo hasa chini ya kitovu wakati wa baridi na pengine pale anapokuwa ameshiba au amekula vitu vitamu, hiyo huwa ni dalili ya ngiri ya kitovu kwa walio wengi.
4. Kupinga mingurumo tumboni.
Kwa kawaida ngiri nyingi ili kutokea uanzia kwenye tumbo ambapo sehemu ya utumbo inaota kuelekea kwenye uwazi fulani inawezekana kwenye kifua au na sehemu mbalimbali za mwili ambapo ngiri inaweza kutokea kwa hiyo hali hii usababisha mingurumo kutokea kwenye tumbo.
5. Kuhisi una haja kubwa na ukifika chooni unatoa gesi tu, kwa hiyo kama kuna tatizo hili la ngiri tumbo ukaa na gesi sana ,hii ni kwa sababu ya hali ya tumbo kutokuwa kwenye hali yake ya kawaida.
6. Kukaa siku kadhaa bila kupata haja kubwa , inawezekana kwa siku kama mbili au zaidi bila kuwepo kwa choo, au ukibatiwa kupata choo ni kidogo sana na huwa kama choo ya mbuzi.
7. Pengine Mgonjwa anakwenda haja mara kwa mara, hasa anakuwa anahisi haja kubwa na akienda uko ni gesi na choo kidogo hali hiyo usumbua sana na kufikia kiasi cha mgonjwa kukaa karibu na choo na hatoi kitu cha maana.
8. Kupotea kwa nuru ya macho.
Mara nyingine kuna wagonjwa ambao nuru za macho upotea, ila hali hii utokea kwa mara chache sana na sio kupotea kwa nuru ni tatizo la ngiri kwa hiyo mgonjwa anapaswa kupima kwanza ili kujua tatizo ni nini.
9. Maumivu makubwa ya mgongo na kiuno.
Kuna wagonjwa wengine wanahisi kuwa na maumivu makali ya mgongo na kiuno na pengine hali inaweza kufikia kiasi kwamba Mgonjwa anashindwa kutembea, kwa hiyo ni vizuri kupima haraka na kugundua tatizo ni lipi.
10. Makende kuwa kwenye sehemu moja.
Kuna wakati mwingine makende yote yanakuwa kwenye sehemu moja kwa hiyo ni vizuri kujua Dalili hii ili kuweza kutibu na pengine mgonjwa anahisi maumivu makali sana kwenye sehemu za siri hasa kwa wanaume.
11.Pamoja na kujua Dalili zote za ngiri ni vizuri kabisa kujua kuwa sio Dalili zote ni za kuwepo kwa ngiri kwa hiyo vipimo ni lazima na kuwaona wataalamu wa afya ni jambo la muhimu sana ili kuweza kugundua kuwae ni tatizo gani kwa sababu kuna Magonjwa mbalimbali ambayo yana Dalili kama hizi.
12.Pia tunapaswa kutoa wito kwa jamii kuwa ugonjwa wa ngiri upo na unatibika kwa hiyo elimu inapaswa kutolewa kwa jamii ili kuepuka hali ya kuwaficha wagonjwa wakiwa na umani kuwa ni magonjwa ya zinaa na kuona kuwa ni aibu kwa familia na kuwatibu wagonjwa ki mila hali inayosababisha kuongezeka kwa maumivu na tatizo kubwa kubwa zaidi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
sukari kupungua mwilini (Hypoglycemia) huhusishwa kwa kawaida na matibabu ya Kisukari. Hata hivyo, hali mbalimbali, nyingi zikiwa nadra, zinaweza kusababisha sukari ya chini ya damu kwa watu wasio na Kisukari. Kama vile Homa, Hy
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi namna ya magonjwa ya koo yanavyosambaa, magonjwa haya usambaa kutoka sehemu Moja kwenda nyingine kwa njia tofauti kama ifuayavyo
Soma Zaidi...Coma ni hali ya kupoteza fahamu kwa muda mrefu ambayo inaweza kusababishwa na matatizo mbalimbali Jeraha la Kichwa, Kiharusi, Uvimbe kwenye ubongo, ulevi wa dawa za kulevya au pombe, au hata ugonjwa wa msingi,
Soma Zaidi...Hapa utajifunza sababu zinzopelekea mdomo kubadilika ladha na kuwa mchungu, ama mchachu.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa upele na matatibabu yake, ni ugonjwa unaosabavishwa na mdudu kwa kitaalamu huitwa mites sarcoptes scrabie mdudu huyu usababisha miwasho kwenye ngozi.
Soma Zaidi...Je kujaa kwa mate mdomoni ni dalili ya kuwa na VVU, na je ni zipi dalili za Virusi Vya Ukimwi (VVU) mdomoni?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili za Dengue,ni Dalili ambazo huwa kwenye makundi matatu na kuwepo kwa makundi hayautegemea kuongezeka kwa tatizo kwa sababu tatizo likiongezeka bila kutibiwa na dalili uongezeka na kufikia kwenye sehemu isiyo ya kawaida kwa mg
Soma Zaidi...Katika post hii utajifunza kuhusu ugonjwa wa vitiligo, chanzo chake, dalili zake na matibabu yaje
Soma Zaidi...