picha

Yajue magonjwa nyemelezi.

Posti hii inahusu zaidi magonjwa nyemelezi ambayo kwa kawaida utokea pale ambapo kinga ya mwili inashuka.

Magonjwa nyemelezi

1.Ugonjwa wa kifua kikuu

 Ni mojawapo ya magonjwa nyemelezi kwa kawaida utokea pale ambapo kinga ya mwili ikishuka huu ugonjwa unaweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya hewa au endapo mgonjwa hajaanza kutumia dawa na pengine uambukizwa pale mtu akishika makohozi ya mgonjwa wa kifua kikuu na kama hajanawa mikono anaweza kushika kitu chochote Cha kula akajiambukiza, zifuatazo ni dalili za ugonjwa wa kifua kikuu.

_ kukohoa ndani ya wiki mbili na zaidi

_ kupungua uzito

_ kuwa na joto hasa wakati wa usiku

_ Homa za mara kwa mara

_ makohozi kuwa na damu

 

2. Magonjwa ya ngozi

Huu ni ugonjwa ambao pia ni nyemelezi kwa mtu ambaye kinga yake Iko chini, ambapo ngozi ya mgonjwa ushambulia sana na bakteria na kufanya mwili uwe na maupele upele ambayo hayaponi au uchukua mda mrefu kupona na pengine vidonda uweza kusababisha maambukizi mengine kama vile Homa kupanda zaidi na kusababisha madhara makubwa hasa kwa watoto kama vile degedege kwa hiyo tunapaswa kuwa macho iwapo kinga ya mwili ikishuka na kutafuta njia ya kuipandisha.

 

3.Kandidiasisi

Ni ugonjwa nyemelezi ambao utokea ikiwa kinga ya mwili ikishuka na hasahasa ushambulia sehemu za Siri na kusababisha maupele na kumfanya mtu aanze kujikinga , huu ugonjwa usababishwa na fangasi ambazo ushambulia sehemu za Siri,kwahiyo unaweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kujamiiana kwa mtu Mwenye ugonjwa na ambaye Hana,kwa hiyo mtu akiwa na huu ugonjwa anapaswa kwenda hospitalini Ili akapatiwe dawa maana ugonjwa huu upo na unatibika

 

4. Mkanda wa jeshi.

Huu ni ugonjwa ambao utokea Baada ya kinga ya mwili kushuka, ugonjwa huu usababishwa na virusi ambaye ushambulia kulingana na sehemu ya nevu zinapopita kwa hiyo maambukizi uendana na nevu ya sehemu ndo maana utakuta mtu amishambuliwa sehemu fulani, Dalili za ugonjwa huu ni pamoja na Homa kutokea, maumivu kwenye sehemu ya maambukizi. Mgonjwa wa mkanda wa jeshi anaweza kupatiwa dawa kwa kufuata nadalili na hali ya maumivu na vidonda vilivyopo.

 

Magonjwa nyemelezi yakitokea ni lazima mgonjwa apelekwe hospitali mara moja Ili kuepuka madhara makubwa yanayoweza kujitokeza kwa sababu iwapo kinga imeshuka sana magonjwa zaidi ya mawili yanaweza kutokea kwa wakati mmoja, kwa hiyo tuwe makini kulinda afya nzetu na kutumia dawa zinazohitajika .

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3114

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰2 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰5 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Dalili za maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo

Posti hii inahusu zaidi maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo,ni dalili ambazo ujionesha kwa mtu akiwa na shida kwenye utumbo mdogo na tumbo la kawaida.

Soma Zaidi...
Matatizo ya unene kwa watoto (childhood obesity)

post Ina onyesha madhara na matatizo ya Unene Utoto ni hali mbaya ya kiafya inayoathiri watoto na vijana. Inatokea wakati mtoto yuko juu ya uzito wa kawaida kwa umri na urefu wake

Soma Zaidi...
Vyakula Vinavyoongeza Kinga ya Mwili.

​Blogu hii inaangazia umuhimu wa lishe bora katika kuimarisha mfumo wa kinga ya mwili. Tutajadili vyakula mahususi vyenye virutubisho muhimu, umuhimu wa vitamini na madini, pamoja na ukweli wa kisayansi kuhusu jinsi lishe inavyochangia afya yako kwa ujumla.

Soma Zaidi...
Tabia za kujikosoa kupita kiasi na jinsi ya kujenga upendo

​Katika ulimwengu wa kisasa, shinikizo la kuwa "mkamilifu" mara nyingi husababisha watu wengi kuangukia katika mtego wa kujikosoa kupita kiasi. Makala haya yanachunguza asili ya sauti hii ya ndani (inner critic), madhara yake katika afya ya akili, na kutoa mwongozo wa hatua kwa hatua wa jinsi ya kugeuza mtazamo huo kuwa upendo na huruma kwa nafsi yako (self-compassion).

Soma Zaidi...