Yajue magonjwa nyemelezi.
Posti hii inahusu zaidi magonjwa nyemelezi ambayo kwa kawaida utokea pale ambapo kinga ya mwili inashuka.
Magonjwa nyemelezi
1.Ugonjwa wa kifua kikuu
Ni mojawapo ya magonjwa nyemelezi kwa kawaida utokea pale ambapo kinga ya mwili ikishuka huu ugonjwa unaweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya hewa au endapo mgonjwa hajaanza kutumia dawa na pengine uambukizwa pale mtu akishika makohozi ya mgonjwa wa kifua kikuu na kama hajanawa mikono anaweza kushika kitu chochote Cha kula akajiambukiza, zifuatazo ni dalili za ugonjwa wa kifua kikuu.
_ kukohoa ndani ya wiki mbili na zaidi
_ kupungua uzito
_ kuwa na joto hasa wakati wa usiku
_ Homa za mara kwa mara
_ makohozi kuwa na damu
2. Magonjwa ya ngozi
Huu ni ugonjwa ambao pia ni nyemelezi kwa mtu ambaye kinga yake Iko chini, ambapo ngozi ya mgonjwa ushambulia sana na bakteria na kufanya mwili uwe na maupele upele ambayo hayaponi au uchukua mda mrefu kupona na pengine vidonda uweza kusababisha maambukizi mengine kama vile Homa kupanda zaidi na kusababisha madhara makubwa hasa kwa watoto kama vile degedege kwa hiyo tunapaswa kuwa macho iwapo kinga ya mwili ikishuka na kutafuta njia ya kuipandisha.
3.Kandidiasisi
Ni ugonjwa nyemelezi ambao utokea ikiwa kinga ya mwili ikishuka na hasahasa ushambulia sehemu za Siri na kusababisha maupele na kumfanya mtu aanze kujikinga , huu ugonjwa usababishwa na fangasi ambazo ushambulia sehemu za Siri,kwahiyo unaweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kujamiiana kwa mtu Mwenye ugonjwa na ambaye Hana,kwa hiyo mtu akiwa na huu ugonjwa anapaswa kwenda hospitalini Ili akapatiwe dawa maana ugonjwa huu upo na unatibika
4. Mkanda wa jeshi.
Huu ni ugonjwa ambao utokea Baada ya kinga ya mwili kushuka, ugonjwa huu usababishwa na virusi ambaye ushambulia kulingana na sehemu ya nevu zinapopita kwa hiyo maambukizi uendana na nevu ya sehemu ndo maana utakuta mtu amishambuliwa sehemu fulani, Dalili za ugonjwa huu ni pamoja na Homa kutokea, maumivu kwenye sehemu ya maambukizi. Mgonjwa wa mkanda wa jeshi anaweza kupatiwa dawa kwa kufuata nadalili na hali ya maumivu na vidonda vilivyopo.
Magonjwa nyemelezi yakitokea ni lazima mgonjwa apelekwe hospitali mara moja Ili kuepuka madhara makubwa yanayoweza kujitokeza kwa sababu iwapo kinga imeshuka sana magonjwa zaidi ya mawili yanaweza kutokea kwa wakati mmoja, kwa hiyo tuwe makini kulinda afya nzetu na kutumia dawa zinazohitajika .
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 ai web app π2 Kitabu cha Afya π3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π4 web hosting π5 Madrasa kiganjani π6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Kutetemeka kwa mikono au mwili bila sababu.
Kutetemeka (tremor) ni miondoko isiyo ya hiari ya sehemu yoyote ya mwili, kwa kawaida mikono, kichwa, au sauti, inayotokana na mikazo ya misuli ya mara kwa mara. Ingawa wengi huhisi ni tatizo la wazee pekee, linaweza kutokea kwa mtu yeyote na kwa sababu mbalimbali. Makala haya yanafafanua sababu za kutetemeka, kuanzia hali za kawaida za muda mfupi hadi changamoto za neva zinazohitaji matibabu.
Soma Zaidi...Tabia za kujidhuru (Self-harm): Nini cha kufanya?
Tabia ya kujidhuru kimakusudi ni ishara ya wazi ya maumivu makali ya ndani ya kihisia ambayo mtu anashindwa kuyastahimili. Makala haya yanachambua kwa nini hali hii hutokea, jinsi ya kuacha unyanyapaa, na hatua za vitendo unazoweza kuchukua ikiwa wewe mwenyewe au mtu unayemjali anapitia changamoto hii.
Soma Zaidi...Sababu za Kuchoka Sana Mwilini
βUchovu wa mwili (fatigue) ni hisia ya kukosa nguvu, kutaka kulala mara kwa mara, na kuhisi mwili ni mzito, hali ambayo haiishi hata baada ya kupata mapumziko. Ingawa mara nyingi ni matokeo ya mtindo wa maisha, wakati mwingine inaweza kuwa ishara ya tatizo la kiafya linalohitaji uangalizi. Makala hii inaangazia sababu kuu za uchovu huu na hatua za kurejesha nguvu zako.
Soma Zaidi...Dalili za madonda ya koo
Posti hii inahusu zaidi magonjwa ya koo, ni ugonjwa unaoshambulia sana sehemu ya koo la hewa, na na huwa na dalili zake kama ifuayavyo.
Soma Zaidi...Ni bakteria gani husababisha ugonjwa wa pumu
Post hii inakwenda kujibu swali linalosema je ni bakteria aina gani husababisha igonjwa wa pumu.
Soma Zaidi...