Yajue magonjwa nyemelezi.

Posti hii inahusu zaidi magonjwa nyemelezi ambayo kwa kawaida utokea pale ambapo kinga ya mwili inashuka.

Magonjwa nyemelezi

1.Ugonjwa wa kifua kikuu

 Ni mojawapo ya magonjwa nyemelezi kwa kawaida utokea pale ambapo kinga ya mwili ikishuka huu ugonjwa unaweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya hewa au endapo mgonjwa hajaanza kutumia dawa na pengine uambukizwa pale mtu akishika makohozi ya mgonjwa wa kifua kikuu na kama hajanawa mikono anaweza kushika kitu chochote Cha kula akajiambukiza, zifuatazo ni dalili za ugonjwa wa kifua kikuu.

_ kukohoa ndani ya wiki mbili na zaidi

_ kupungua uzito

_ kuwa na joto hasa wakati wa usiku

_ Homa za mara kwa mara

_ makohozi kuwa na damu

 

2. Magonjwa ya ngozi

Huu ni ugonjwa ambao pia ni nyemelezi kwa mtu ambaye kinga yake Iko chini, ambapo ngozi ya mgonjwa ushambulia sana na bakteria na kufanya mwili uwe na maupele upele ambayo hayaponi au uchukua mda mrefu kupona na pengine vidonda uweza kusababisha maambukizi mengine kama vile Homa kupanda zaidi na kusababisha madhara makubwa hasa kwa watoto kama vile degedege kwa hiyo tunapaswa kuwa macho iwapo kinga ya mwili ikishuka na kutafuta njia ya kuipandisha.

 

3.Kandidiasisi

Ni ugonjwa nyemelezi ambao utokea ikiwa kinga ya mwili ikishuka na hasahasa ushambulia sehemu za Siri na kusababisha maupele na kumfanya mtu aanze kujikinga , huu ugonjwa usababishwa na fangasi ambazo ushambulia sehemu za Siri,kwahiyo unaweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kujamiiana kwa mtu Mwenye ugonjwa na ambaye Hana,kwa hiyo mtu akiwa na huu ugonjwa anapaswa kwenda hospitalini Ili akapatiwe dawa maana ugonjwa huu upo na unatibika

 

4. Mkanda wa jeshi.

Huu ni ugonjwa ambao utokea Baada ya kinga ya mwili kushuka, ugonjwa huu usababishwa na virusi ambaye ushambulia kulingana na sehemu ya nevu zinapopita kwa hiyo maambukizi uendana na nevu ya sehemu ndo maana utakuta mtu amishambuliwa sehemu fulani, Dalili za ugonjwa huu ni pamoja na Homa kutokea, maumivu kwenye sehemu ya maambukizi. Mgonjwa wa mkanda wa jeshi anaweza kupatiwa dawa kwa kufuata nadalili na hali ya maumivu na vidonda vilivyopo.

 

Magonjwa nyemelezi yakitokea ni lazima mgonjwa apelekwe hospitali mara moja Ili kuepuka madhara makubwa yanayoweza kujitokeza kwa sababu iwapo kinga imeshuka sana magonjwa zaidi ya mawili yanaweza kutokea kwa wakati mmoja, kwa hiyo tuwe makini kulinda afya nzetu na kutumia dawa zinazohitajika .

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 2332

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

DALILI ZA MIMBA BAADA YA TENDO LA NDOA

Je unahitaji kujuwa kama umepata ujauzito baada ya kufanya tendo la ndoa? hakika sio rahisi ila kama utakuwa makini utaweza.

Soma Zaidi...
Sababu zinazopelekea maumivu ya Matiti.

 Maumivu ya matiti hutokea zaidi kwa watu ambao hawajamaliza hedhi, ingawa yanaweza kutokea baada ya kukoma hedhi. 

Soma Zaidi...
Magonjwa ya moyo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu magonjwa ya moyo

Soma Zaidi...
Sasa UKIMWI unatokeaje?

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia ambazo UKIMWI hutokea

Soma Zaidi...
Maradhi ya Pumu yanatokeaje?

Nini hasa kinatokea mpaka mtu anakuwa na pumu, ama anashambuliwa na pumu. Makala hii itakwenda kukufundisha jambo hili

Soma Zaidi...
Dalili za Kuvimbiwa kwa watoto

Posti hii inazungumzia kuhusiana Kuvimbiwa kwa watoto ni tatizo la kawaida.Kuvimbiwa kwa watoto mara nyingi kuna sifa ya kupata haja kubwa mara kwa mara au kinyesi kigumu, kikavu. Sababu mbalimbali zinaweza kusababisha kuvimbiwa kwa watoto.Sababu za kawa

Soma Zaidi...
Jinsi ya kutoa huduma ya kwanz akwa liyeshambuliwa na pumu

Hii ni huduma ya kwanza kwa aliyeshambuliwa na pumu katika mazingira ambayo ni mbali na kituo cha afya, na hakuna dawa.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa vitiligo, chanzo, dalili na matibabu yake

Katika post hii utajifunza kuhusu ugonjwa wa vitiligo, chanzo chake, dalili zake na matibabu yaje

Soma Zaidi...
Sababu za kuumwa na tumbo, chini ya kitomvu ama upande wa kulia

Post hii inakwenda kukutajia baadhi tu ya sababu zinazopelekea kuumwa na tumbo. Hali hizi zinawweza kuwapata watu wa jinsia zote katika umri wowote ule. Ijapokuwa nyingine si kwa wote ni kwa baadhi ya watu. hapa nitakuletea sababu 5 tu.

Soma Zaidi...