Yajue magonjwa nyemelezi.


image


Posti hii inahusu zaidi magonjwa nyemelezi ambayo kwa kawaida utokea pale ambapo kinga ya mwili inashuka.


Magonjwa nyemelezi

1.Ugonjwa wa kifua kikuu

 Ni mojawapo ya magonjwa nyemelezi kwa kawaida utokea pale ambapo kinga ya mwili ikishuka huu ugonjwa unaweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya hewa au endapo mgonjwa hajaanza kutumia dawa na pengine uambukizwa pale mtu akishika makohozi ya mgonjwa wa kifua kikuu na kama hajanawa mikono anaweza kushika kitu chochote Cha kula akajiambukiza, zifuatazo ni dalili za ugonjwa wa kifua kikuu.

_ kukohoa ndani ya wiki mbili na zaidi

_ kupungua uzito

_ kuwa na joto hasa wakati wa usiku

_ Homa za mara kwa mara

_ makohozi kuwa na damu

 

2. Magonjwa ya ngozi

Huu ni ugonjwa ambao pia ni nyemelezi kwa mtu ambaye kinga yake Iko chini, ambapo ngozi ya mgonjwa ushambulia sana na bakteria na kufanya mwili uwe na maupele upele ambayo hayaponi au uchukua mda mrefu kupona na pengine vidonda uweza kusababisha maambukizi mengine kama vile Homa kupanda zaidi na kusababisha madhara makubwa hasa kwa watoto kama vile degedege kwa hiyo tunapaswa kuwa macho iwapo kinga ya mwili ikishuka na kutafuta njia ya kuipandisha.

 

3.Kandidiasisi

Ni ugonjwa nyemelezi ambao utokea ikiwa kinga ya mwili ikishuka na hasahasa ushambulia sehemu za Siri na kusababisha maupele na kumfanya mtu aanze kujikinga , huu ugonjwa usababishwa na fangasi ambazo ushambulia sehemu za Siri,kwahiyo unaweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kujamiiana kwa mtu Mwenye ugonjwa na ambaye Hana,kwa hiyo mtu akiwa na huu ugonjwa anapaswa kwenda hospitalini Ili akapatiwe dawa maana ugonjwa huu upo na unatibika

 

4. Mkanda wa jeshi.

Huu ni ugonjwa ambao utokea Baada ya kinga ya mwili kushuka, ugonjwa huu usababishwa na virusi ambaye ushambulia kulingana na sehemu ya nevu zinapopita kwa hiyo maambukizi uendana na nevu ya sehemu ndo maana utakuta mtu amishambuliwa sehemu fulani, Dalili za ugonjwa huu ni pamoja na Homa kutokea, maumivu kwenye sehemu ya maambukizi. Mgonjwa wa mkanda wa jeshi anaweza kupatiwa dawa kwa kufuata nadalili na hali ya maumivu na vidonda vilivyopo.

 

Magonjwa nyemelezi yakitokea ni lazima mgonjwa apelekwe hospitali mara moja Ili kuepuka madhara makubwa yanayoweza kujitokeza kwa sababu iwapo kinga imeshuka sana magonjwa zaidi ya mawili yanaweza kutokea kwa wakati mmoja, kwa hiyo tuwe makini kulinda afya nzetu na kutumia dawa zinazohitajika .

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    2 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    3 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    4 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Faida za kusafisha vidonda.
Posti hii inahusu zaidi faida za kusafisha vidonda, ni faida ambazo Mgonjwa mwenye vidonge uzipata kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

image Maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa Soma Zaidi...

image Fahamu Ugonjwa wa hepatitis A
Hepatitis A ni ugonjwa wa kuambukiza wa ini unaosababishwa na virusi vya Hepatitis A. Virusi ni mojawapo ya aina kadhaa za virusi vya Hepatitis vinavyosababisha kuvimba na kuathiri uwezo wa ini wako kufanya kazi. Soma Zaidi...

image Zifahmu Dalili za homa ya ini Kali ya pombe.
Posti hii inaonyesha dalili na Mambo Hatari yanayosababisha homa ya ini Kali ya pombe. Soma Zaidi...

image Ninashida Kuna mtu anaumwa pressure Kila anap pima Iko juu il mwil aumuumi at kidg n dawa anatumia unawez kunisaidiaj
Kama unasumbuliwa na presha post hii ni kwa ajili yako. Hapa tutakuoatia ushauri kutokana na swali alilouliza mdau wetu. Soma Zaidi...

image Faida za chanjo
Posti hii inahusu zaidi faida ya chanjo, tunajua wazi kuwa chanjo Ina faida kubwa kwenye mwili wa binadamu na vile vile kwenye jamii kama tutakavyoona hapo chini. Soma Zaidi...

image Sababu za ugumba kwa wanawake
Post hii inahusu zaidi sababu za ugumba kwa wanawake, ni sababu ambazo upelekea wanawake wengi kuwa wagumba ukizingatia kuwa wanazaliwa wakiwa na uwezo kabisa wa kupata watoto lakini kwa sababu mbalimbali za kimazingira wanakoswa watoto, zifuatazo ni sababu za ugumba kwa wanawake. Soma Zaidi...

image Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto wadogo.
Posti inahusu zaidi madhara ya kaswende kwa mama mjamzito na mtoto, Ni ugonjwa unaopatikana hasa kwa njia ya kujamiiana na utoka kwa mwenye Ugonjwa kwenda kwa mtu ambaye hana ugonjwa, kwa hiyo tunapaswa kujua madhara ya ugonjwa huu kwa mama mjamzito na mtoto. Soma Zaidi...

image Siku za kupata mimba
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu siku za kupata mimba Soma Zaidi...

image Dalili za fangasi ukeni
Post hii inakwenda kukujulisha dalili za kuwa huwenda una fangasi sehemu zako za siri. Soma Zaidi...