Mzio (aleji) na Dalili zake
Posti hii inahusu zaidi mzio na Dalili zake ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mtu mwenye mzio, kuna wakati watu wengine ushindwa kutambua kuwa ni mzio au la, lakini leo tunaenda kujua Dalili za mzio kama ifuatavyo.
Mzio (aleji) na Dalili zake.
Mzio usababishwa na vitu mbalimbali kama vile vumbi, kuumwa na wadudu, baadhi ya vyakula, kemikali au madawa fulani, mzio utokea kwa mtu mmoja na mwingine na kila mtu ana mzio wake kwa mfano mtu mmoja anaweza kuwa na Mzio wa vumbi mwingine hana kwa hiyo utofautiana kutoka kwa mtu mmoja na mwingine, na dawa za kutuliza mzio zipo ambazo ni citrizen, pilitin na anti histamine na Mzio ukizidi mwone daktari kwa msaada zaidi.
1. Dalili mojawapo ambayo ilinyesha kubwa ni mzio ni wekundu usoni, mwasho, au upele hayo yanaweza kutokea kwa mtu kwa sababu pengine ametumia dawa fulani ambayo haipatani na mwili wake au chakula fulani kama vile nyama,au amesikia harufu fulani ya maua hali hii umfanya kubwa na vitu vilivyotakiwa hapo juu.
2. Dalili nyingine ni kama vile kuvimba midomo hasa hasa hali hii utokea kwa sababu ya vyakula na kuvimba kinywa na koo, kumeza kwa shida ukiona mgonjwa wako ana dalili kama hizi moja kwa moja anapaswa kupata matibabu yanayofaa ili kuepuka kusababisha madhara makubwa zaidi.
3. Kupumua kwa shida
Aina hii ya mzio uwakumba sana watu mzio wa vumbi, harufu ya maua na vitu vingine ambavyo vinahusiana na kunusa, iwapo mtu amepatwa na Mzio huu uwa na Dalili kama za Asthma kwa hiyo ni vizuri kumpeleka hospitalini ili kuweza kuepuka madhara zaidi, hasa kama ni kwa mtoto hali inaweza kuwa mbaya zaidi kwa hiyo matibabu yanapaswa kutolewa mapema iwezekanavyo.
4. Kuvimba mikono na miguu.
Hii ni Dalili mojawapo ya mzio ambao utokea kwa mtu inawezekana ikawa ni kwa sababu ya dawa au kwa sababu ya vitu vingine kama vile vumbi kwa hiyo kama mgonjwa yuko hospitalini anaumwa dalili hii ukajitokeza anapaswa kufuata ushauri wa daktari au abadilishe dawa au mazingira.
5. Kichefuchefu au maumivu ya tumbo.
Mgonjwa pengine anahisi kichefuchefu kwa sababu pengine mzio unakuwa imeingilia mmeng'enyo wa chakula, kwa hiyo pengine tumbo linaweza kuuma kichefuchefu na hata kutapika kwa mgonjwa kwa hiyo tunapaswa kujua Dalili hizi na kuzifanyia kazi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 ai web app 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Sababu za maumivu ya tumbo
hapa utajifunza maradhi mbalimbali yanatopelekea kuwepo kwa maumivu ya tumbo
Soma Zaidi...Namna ya kuzuia Ugonjwa wa kaswende
Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia Ugonjwa wa kaswende, tunajua wazi kuwa Ugonjwa huu unasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kufanya ngono zembe na njia nyingine kwa hiyo tunaweza kuzuia kusambaa na kuenea kwa ugonjwa huu kwa n
Soma Zaidi...Faida za Kunywa Maji Mengi Kila Siku
​Maji ni kiini cha uhai na yanachukua zaidi ya nusu ya uzito wa mwili wa binadamu. Post hii inaangazia umuhimu wa kunywa maji ya kutosha kila siku, jinsi yanavyosaidia utendaji kazi wa viungo vya mwili, na vidokezo vya kuhakikisha unakunywa maji ya kutosha
Soma Zaidi...Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto wadogo.
Posti inahusu zaidi madhara ya kaswende kwa mama mjamzito na mtoto, Ni ugonjwa unaopatikana hasa kwa njia ya kujamiiana na utoka kwa mwenye Ugonjwa kwenda kwa mtu ambaye hana ugonjwa, kwa hiyo tunapaswa kujua madhara ya ugonjwa huu kwa mama mjamzito na mt
Soma Zaidi...Dalili za ugonjwa wa gonoria (gonorrhea)
UGONJWA WA GONORIA NA DALILI ZAKE (GONORRHEA)Gonoria (gonorrhea) ni katika maradhi yanayoambukizwa kwa njia ya ngono.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa surua kwa watoto.
Surua ni ugonjwa wa kuambukiza unaosababishwa na homa na upele mwekundu, unaotokea utotoni. Wakati mtu aliye na virusi akikohoa au kupiga chafya, matone yaliyoambukizwa huenea angani na kutua kwenye sehemu zilizo karibu. Mtoto anaweza kupata virusi kwa ku
Soma Zaidi...