picha

Mzio (aleji) na Dalili zake

Posti hii inahusu zaidi mzio na Dalili zake ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mtu mwenye mzio, kuna wakati watu wengine ushindwa kutambua kuwa ni mzio au la, lakini leo tunaenda kujua Dalili za mzio kama ifuatavyo.

Mzio (aleji)  na Dalili zake.

Mzio usababishwa na vitu mbalimbali kama vile vumbi, kuumwa na wadudu, baadhi ya vyakula, kemikali au madawa fulani, mzio utokea kwa mtu mmoja na mwingine na kila mtu ana mzio wake kwa mfano mtu mmoja anaweza kuwa na Mzio wa vumbi mwingine hana kwa hiyo utofautiana kutoka kwa mtu mmoja na mwingine, na dawa za kutuliza mzio zipo ambazo ni citrizen, pilitin na anti histamine na Mzio ukizidi mwone daktari kwa msaada zaidi.

 

1. Dalili mojawapo ambayo ilinyesha kubwa ni mzio ni wekundu usoni, mwasho, au upele hayo yanaweza kutokea kwa mtu kwa sababu pengine ametumia dawa fulani ambayo haipatani na mwili wake au chakula fulani kama vile nyama,au amesikia harufu fulani ya maua hali hii umfanya kubwa na vitu vilivyotakiwa hapo juu.

 

2. Dalili nyingine ni kama vile kuvimba midomo hasa hasa hali hii utokea kwa sababu ya vyakula na kuvimba kinywa na koo, kumeza kwa shida ukiona mgonjwa wako ana dalili kama hizi moja kwa moja anapaswa kupata matibabu yanayofaa ili kuepuka kusababisha madhara makubwa zaidi.

 

3. Kupumua kwa shida 

Aina hii ya mzio uwakumba sana watu mzio wa vumbi, harufu ya maua na vitu vingine ambavyo vinahusiana na kunusa, iwapo mtu amepatwa na Mzio huu uwa na Dalili kama za Asthma  kwa hiyo ni vizuri kumpeleka hospitalini ili kuweza kuepuka madhara zaidi, hasa kama ni kwa mtoto hali inaweza kuwa mbaya zaidi kwa hiyo matibabu yanapaswa kutolewa mapema iwezekanavyo.

 

4. Kuvimba mikono na miguu.

Hii ni Dalili mojawapo ya mzio ambao utokea kwa mtu inawezekana ikawa ni kwa sababu ya dawa au kwa sababu ya vitu vingine kama vile vumbi kwa hiyo kama mgonjwa yuko hospitalini anaumwa dalili hii ukajitokeza anapaswa kufuata ushauri wa daktari au abadilishe dawa au mazingira.

 

5. Kichefuchefu au maumivu ya tumbo.

Mgonjwa pengine anahisi kichefuchefu kwa sababu pengine mzio unakuwa imeingilia mmeng'enyo wa chakula, kwa hiyo pengine tumbo linaweza kuuma kichefuchefu na hata kutapika kwa mgonjwa kwa hiyo tunapaswa kujua Dalili hizi na kuzifanyia kazi.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3520

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰2 ai web app     πŸ‘‰3 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰5 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Kuharisha choo cha marenda renda ni dalili gani?

Hivi huwa unachunguza choo chako? ivi huwa kinazama kwenye maji ama kinaelea? Kila damu ama malendalenda, je ni cheusi sana na kina harufu kali sana.

Soma Zaidi...
Sababu za wanawake kuwa na maumivu kwenye kiuno

Posti hii inahusu zaidi sababu za wanawake kuwa na maumivu kwenye viungo, ni ugonjwa unaowapata na wanaume ila kwa wanaweza unaowapata sana ukilinganisha na wanaume.

Soma Zaidi...
Tatizo la damu kutokufikia tishu baada ya kutokea jeraha kwenye tishu (gangrene)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na tatizo la damu kutokufikia tishu baada ya kutokea jeraha kwenye tishu ambao hujulikana Kama gangrene inahusu kifo cha tishu za mwili kutokana na ukosefu wa mtiririko wa damu au maambukizi ya bakteria. Ugonjwa wa gangre

Soma Zaidi...
Zijue sababu za moyo kutanuka.

Posti hii inahusu zaidi sababu za moyo kutanuka, Kuna kipindi ambapo moyo utoka kwenye hali yake ya kawaida na kutanuka hali ambayo usababisha madhara kwa mwenye tatizo hilo, ila Kuna sababu ambazo usababisha moyo kutanuka kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
Dalili za mnungu'nguniko wa moyo

Manung'uniko ya moyo ni sauti wakati wa mzunguko wa mapigo ya moyo wako kama vile kutetemeka inayotolewa na damu yenye msukosuko ndani au karibu na moyo wako.

Soma Zaidi...
Dalili za Minyoo kwa Watoto

​Minyoo ni tatizo la kawaida kwa watoto ambalo linaweza kuathiri ukuaji na afya zao kwa ujumla. Makala haya yataeleza dalili za kawaida za maambukizi ya minyoo, ukweli muhimu kuhusu tiba yake, na umuhimu wa usafi katika kuzuia tatizo hili.

Soma Zaidi...