Mzio (aleji) na Dalili zake
Posti hii inahusu zaidi mzio na Dalili zake ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mtu mwenye mzio, kuna wakati watu wengine ushindwa kutambua kuwa ni mzio au la, lakini leo tunaenda kujua Dalili za mzio kama ifuatavyo.
Mzio (aleji) na Dalili zake.
Mzio usababishwa na vitu mbalimbali kama vile vumbi, kuumwa na wadudu, baadhi ya vyakula, kemikali au madawa fulani, mzio utokea kwa mtu mmoja na mwingine na kila mtu ana mzio wake kwa mfano mtu mmoja anaweza kuwa na Mzio wa vumbi mwingine hana kwa hiyo utofautiana kutoka kwa mtu mmoja na mwingine, na dawa za kutuliza mzio zipo ambazo ni citrizen, pilitin na anti histamine na Mzio ukizidi mwone daktari kwa msaada zaidi.
1. Dalili mojawapo ambayo ilinyesha kubwa ni mzio ni wekundu usoni, mwasho, au upele hayo yanaweza kutokea kwa mtu kwa sababu pengine ametumia dawa fulani ambayo haipatani na mwili wake au chakula fulani kama vile nyama,au amesikia harufu fulani ya maua hali hii umfanya kubwa na vitu vilivyotakiwa hapo juu.
2. Dalili nyingine ni kama vile kuvimba midomo hasa hasa hali hii utokea kwa sababu ya vyakula na kuvimba kinywa na koo, kumeza kwa shida ukiona mgonjwa wako ana dalili kama hizi moja kwa moja anapaswa kupata matibabu yanayofaa ili kuepuka kusababisha madhara makubwa zaidi.
3. Kupumua kwa shida
Aina hii ya mzio uwakumba sana watu mzio wa vumbi, harufu ya maua na vitu vingine ambavyo vinahusiana na kunusa, iwapo mtu amepatwa na Mzio huu uwa na Dalili kama za Asthma kwa hiyo ni vizuri kumpeleka hospitalini ili kuweza kuepuka madhara zaidi, hasa kama ni kwa mtoto hali inaweza kuwa mbaya zaidi kwa hiyo matibabu yanapaswa kutolewa mapema iwezekanavyo.
4. Kuvimba mikono na miguu.
Hii ni Dalili mojawapo ya mzio ambao utokea kwa mtu inawezekana ikawa ni kwa sababu ya dawa au kwa sababu ya vitu vingine kama vile vumbi kwa hiyo kama mgonjwa yuko hospitalini anaumwa dalili hii ukajitokeza anapaswa kufuata ushauri wa daktari au abadilishe dawa au mazingira.
5. Kichefuchefu au maumivu ya tumbo.
Mgonjwa pengine anahisi kichefuchefu kwa sababu pengine mzio unakuwa imeingilia mmeng'enyo wa chakula, kwa hiyo pengine tumbo linaweza kuuma kichefuchefu na hata kutapika kwa mgonjwa kwa hiyo tunapaswa kujua Dalili hizi na kuzifanyia kazi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π2 ai web app π3 Madrasa kiganjani π4 Simulizi za Hadithi Audio π5 Kitabu cha Afya π6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Walio katika hatari ya kupata magonjwa ya ngono
Posti hii inahusu zaidi watu walio kwenye liski ya kupata magonjwa ya ngono, ni watu wanaofanya mambo yanayosababisha kupata magonjwa ya ngono.
Soma Zaidi...Dalili za selulitis.
Selulitis ni maambukizi ya ngozi ya bakteria ya kawaida, ambayo yanaweza kuwa mbaya. Cellulitis inaonekana kama sehemu nyekundu ya ngozi iliyovimba na inahisi joto na laini. Inaweza kuenea kwa kasi kwa sehemu nyingine za mwili. Cellulitis haienei kuto
Soma Zaidi...Dalili za Ugonjwa wa mapafu.
posti hii inahusu dalili za ugonjwa wa mapafu.ambapo kitaalamu hujulikana Kama Ugonjwa wa Acute Respiratory Distress Syndrome (ARDS) hutokea wakati Majimaji yanapojaa kwenye vifuko vidogo vya hewa nyororo (alveoli) kwenye mapafu yako. Majimaji mengi kw
Soma Zaidi...Sababu za Mtoto Kuharisha Mara kwa Mara
βUharishaji kwa watoto ni changamoto ya kawaida inayoweza kusababishwa na maambukizi, lishe, au mabadiliko ya kifizikia. Makala haya yatafafanua sababu kuu za tatizo hili, jinsi ya kukabiliana nalo nyumbani, na wakati mwafaka wa kumpeleka mtoto hospitalini.
Soma Zaidi...Dalili za mawe kwenye kibofu Cha mkono
Mawe ya kibofu ni mkusanyiko mgumu wa madini kwenye kibofu chako. Mawe kwenye kibofu hukua wakati mkojo kwenye kibofu chako unapokolea, na kusababisha madini katika mkojo wako kung'aa.
Soma Zaidi...Presha ya kushuka na matibabu yake
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu presha ya kushuka na matibabu yake
Soma Zaidi...