Suratul-takaathur (102) imeteremshwa makkah Ina aya nane
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
- Suratul- Takaathur (102): Imeteremshwa Makkah, Ina Aya Nane.
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.
- Kumekughafilisheni (katika) kutafuta wingi (wa mali na jaha na watoto na kujifakharisha kwayo).
- Hata mmeingia makaburini (mmekufa kabla ya kufanya kheri yeyote).
- Sivyo hivyo! Karibuni hivi mtajua (kuwa sivyo hivyo).
- Kisha (nasema) sivyo hivyo karibuni hivi mtajua (kuwa sivyo hivyo).
- Sivyo hivyo! Lau kama mnajua ujuzi wa yakini (kuwa sivyo hivyo msingefanya hivyo).
- Hakika mtauona moto wa Jahiym.
- Kisha (nasema) mtauona (moto) kwa yakini.
- Kisha kwa hakika mtaulizwa siku hiyo juu ya neema mlizopewa (mlizitumiaje).
Mafunzo kwa Ufupi.
- Pupa katika kutafuta anasa za dunia ndizo hupelekea mtu kumuasi Mwenyezi Mungu (s.w).
- Kuchuma mali na kuhangaikia watoto sio jambo baya, bali lisitusahaulishe katika kumtumikia Mwenyezi Mungu (s.w).
- Kuwepo siku ya mwisho ni jambo lisilo na shaka ili kila mtu akaulzwe juu ya jinsi alivyotumia neema alizopewa.
- Kutumia vibaya neema na vipawa tulivyonavyo hupelekea kumuasi Mola wake na hivyo kustahiki adhabu.
- Neema na vipawa tulivyonavyo ni dhamana kwetu na tutaulizwa siku ya Kiama.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Share follows: 0 |
Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Dai kuwa Muhammad (s.a.w) aliitunga Qur-an ili Kuwania Madaraka na Ukubwa
(x) Dai kuwa Muhammad (s.
Soma Zaidi...Hukumu za waqfu na Ibtida
waqfu ni misimamo ambapo msomaji wa Quran anaruhusiwa kusimama, kuhema au kumeza mate. Na ibtidai ni kuanza baada ya kutoka kwenye waqf
Soma Zaidi...HUKUMU ZA TAFKHIIM NA TARQIQ
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa
Soma Zaidi...ASBAB-NUZUL SABABU ZA KUSHUKA AYA NA SURA KWENYE QURAN
ASBAB NUZUL SABABU ZA KUSHUKA AYA NA SURA KWENYE QURAN Quran imeteremka kwa muda wa miaka 23 kidogokido.
Soma Zaidi...Fadhila za kusoma surat al Kahaf siku ya Ijumaa
Je unajuwa ni kwa nini unatakiwa usikose kusoma surat al Kahaf siku ya ijumaa. Makala hii itakujibu swali hili
Soma Zaidi...Hukumu za Tajwid katika usomaji wa bismillah (basmalah)
Hapa utajifunza kanuni za tajwid katika kusoma bismillah au basmalah.
Soma Zaidi...