Suratul-takaathur (102) imeteremshwa makkah Ina aya nane

Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.

  1. Kumekughafilisheni (katika) kutafuta wingi (wa mali na jaha na watoto na kujifakharisha kwayo).
  2. Hata mmeingia makaburini (mmekufa kabla ya kufanya kheri yeyote).
  3. Sivyo hivyo! Karibuni hivi mtajua (kuwa sivyo hivyo).
  4. Kisha (nasema) sivyo hivyo karibuni hivi mtajua (kuwa sivyo hivyo).
  5. Sivyo hivyo! Lau kama mnajua ujuzi wa yakini (kuwa sivyo hivyo msingefanya hivyo).
  6. Hakika mtauona moto wa Jahiym.
  7. Kisha (nasema) mtauona (moto) kwa yakini.
  8. Kisha kwa hakika mtaulizwa siku hiyo juu ya neema mlizopewa (mlizitumiaje).

 

Mafunzo kwa Ufupi.

  1. Pupa katika kutafuta anasa za dunia ndizo hupelekea mtu kumuasi Mwenyezi Mungu (s.w).
  2. Kuchuma mali na kuhangaikia watoto sio jambo baya, bali lisitusahaulishe katika kumtumikia Mwenyezi Mungu (s.w).
  3. Kuwepo siku ya mwisho ni jambo lisilo na shaka ili kila mtu akaulzwe juu ya jinsi alivyotumia neema alizopewa.
  4. Kutumia vibaya neema na vipawa tulivyonavyo hupelekea kumuasi Mola wake na hivyo kustahiki adhabu.
  5. Neema na vipawa tulivyonavyo ni dhamana kwetu na tutaulizwa siku ya Kiama.

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/01/20/Thursday - 02:07:46 am     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 625

Post zifazofanana:-

Maadui wakubwa wa dola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Dalili za Utasa wa wanaume
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Utasa wa Mwanaume hutokana na uzalishaji mdogo wa mbegu za kiume, utendakazi usio wa kawaida wa manii au kuziba kwa manii ambayo huzuia utoaji wa mbegu za kiume. Magonjwa, majeraha, matatizo ya kiafya sugu, u Soma Zaidi...

Dawa za fangasi ukeni
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za fangasi ukeni Soma Zaidi...

Ambao hawapaswi kupata chanjo
Posti hii inahusu zaidi watu ambao hawapaswi kupewa chanjo, hawa ni wale ambao wana hali tofauti na ikitokea wakapata chanjo wanaweza kupata madhara badala ya kuwasaidia. Soma Zaidi...

Athari za ugonjwa wa Homa ya inni
Posti hii inahusu zaidi adhari za ugonjwa wa Homa ya inni, hizi ni athari ambazo zinaweza kutokea ikiwa ugonjwa huu wa inni haujatibiwa, zifuatazo ni athari za ugonjwa wa inni Soma Zaidi...

Faida za kiafya za tangawizi
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kutumia tangawizi Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 6 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
hili ni somo la sita katika mfululizo wa mafunzo ya HTML level 1. Katika somo hili tutajifunza mambo makuu matatu ambayo ni kuweka menyu, kuweka background color na kufanya faili lako liwe responsive. Soma Zaidi...

Alif lela ulela
Posti hii inakwenda kukusimulia hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Kondomu za kike
Posti hii inaonyesha Faida na hasara za Kondomu za kike Soma Zaidi...

Mtazamo wa makafiri juu ya dini
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu dawa za kutibu minyoo
Post hii inahusu zaidi dawa mbalimbali za kutibu minyoo, tunafahamu kabisa minyoo ni ugonjwa ambao uwapata watu mbalimbali hasa watoto. Soma Zaidi...

Ulaji wa protini kupitiliza
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu athari za ulaji wa protini kupitiliza Soma Zaidi...