image

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Mtumwa wa mfalme na mawaziri

Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha tatu.....

MTUMWA WA AJABU

 

 

 

Kama wasemavyo waliokula chumvi nyingi kuwa muomba mungu hachoki, basi waziri Faridi aliendelea kuomba Mungu hata siku moja akapata taarifa kuwa kuna watumwa wametokea nchi za Uajemi. Hapo waziri alitabasamu kwani alifahamu sasa anakwenda kupata alilolitaka. Kwani alitambuwa kuwa maeneo hayo ndipo watumwa wenye sifa hizo wanapatikana. Basi alifika akauta kuna mabinti wasiopungua 150. waziri aliwaangalia vyema sana huku akagunduwa kuwa kuna wwengine walikuwa wakitabasamu. Alitambuwa kuwa hawa hawafai maana wanadiriki kuuza tabasamu lao bila ya sababu.

 

 

 

Kwa mara ya kwanza waziri akachaguwa walio wazuri kuliko wote. Aliamii kuwa mfalme angeanza kuangalia uzuri hata kabla ya kumthaminisha mtumwa wake. Katika mchujo huu akapata mabinti 21. kisha akaanza kuangalia sauti zao, nywele zao, nyusi na rangi za macho yao. Katika mchujo juu akabahatika kupata 12. kisha akaangalia vigezo vya elimu ya dini na dunia, hapa kabahatika kupata 5. kisha akaangalia hati za uanishi, na ufasaha wa kuzungumza hapa akabahatika kupata 3. sasa akaangalia kama wanafahamu kuburudisha hadhira na kumbrusisha mwanaume. Hapa ndipo akampata binti mmoja aliyefahamika kwa jina la An-neese.

 

 

 

Hakika binti huyu alikuwa mzuri aliyepitiliza vigzo vya sultani. Maana urefu wake haukuwa wa kuchuchumia, hakuhitaji kupaka mafuta ndipo kulainisha ngozi yake. Siku zote alitumia vyakula asili kuweza kuweka mwili wake katika afya na urembo. Hakuwa ni mkwaro wa sauti, mach meupe makubwa, yaliyopambwa na nyuzi nyeysi sana zilizotengeneza umbo la mwezi mwandamo. Nywele nyefu na ngumu zenye afya. Alitambuwa kusoma hati za lugha kadhaa zilizokuwa zikitumia maeneo yale kama kiarabu, kihindi, kiroam (latini) na baaadhi ya lugha za hispatia na fursi.

 

 

 

Waziri alikabidhi pesa palepale. Hapo muuzaji wa watumwa akampa ushauri waziri kuwa, “kwa ;leo usimpeleke kwa mfalme maana ametoka mbali,hivyo kwa uchovu alio nao, uzuri wake utajificha kidogo. Hivyo nakushauri, nenda naye kwanko kwa kiasi cha wiki na atakapozoea hali ya hewa uzurio wake utazidi mara dufu na hapo itakuwa vyema kumpeleka kwa mfalme. Waziri alikubwali ushauri huu japo kwa shingo upande akihofia mwanaye Nurdini.

 

 

 

Waziri siku hiyo alikuwa akirurahia na kuamini sasa amempata wazri Masoud. Ila alihitaji iwe ni mshangao hivyo hakuthubuti kumwambia yeyote kuwa amempata mtumwa wa mfalme. Basi siku hiyo wazir wakati anakwenda na mtumwa wake kwake kwa ushauri wa muuzaji alimueleza kila kitu kuwa awe mbali sana na Nurdin maana ataweza kumuharibia kwani hajawahi kuacha sketi ya mtumwa wala mfanyakazi aliyeletwa nyumbani.yule binti mtumwa akaahidi kuwa hatakuwa na mahusiano na Nurdini kabisa. Basi alipofika nyumbani akamueleza mke wake kila kitu na kumtaka ampatie mtumwa yule kila anachohitaji ili baada ya wiki kupita ampeleke kwaMfalme.

 

 

 

Binti mtumwa akatengewa eneo lake mwenyewe kwa ajili ya malazi na makazi. Mabinti wengine waliandaliwa kwa ajili ya kumpatia kila alichohitaji kuhakikisha kuwa anazea hali ya hewa na uzuri wake unaboreka. Hata hivyo baadhi ya vibinti vifanyakaz wa waziri walikuwa wakichukizwa na uwepowa mtumwa ambaye alikuwa ni kama malkia. Mtumwa ambaye alikuwa akifanyiwa kazi. Hakika mambo haya yalikuwa yakiwachokesha. Walikuwa wana kazi ya kumpikia, kumsugua anapokwenda kuoga, kumpamba na kumfanyia mambo mengine zaidi.

 

 

 

Mambo yote haya yalikuwa yakitokea bila ya Nurdini kutambuwa uwepo wa binti yule. Mambo haya yalifanywa kwa siri ili aibu kubwa isijempata Waziri. Waziri aliamini kuwa kama atamueleza Nurdini kuwa asijekwenda kumuona yule binti basi huenda Nurdini ndio angekwenda kwa makusudi, kwa ajili ya kuridhisha udadisi wake. Basi mambo yakawa kama hivyo haimaye siku mbili zikaisha na ya tatu ikaingia. Uzri wa binti ulikuwa ukiongezeka kila siku zinapozidi. Mawazo ya kubadili maamuzi ya waziri yalikuwa yakimjia. Na hata me wake wivu ulianza kumkamata ijapokuwa hakuweza kudhihirisha.

 

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Mankaa Tarehe 2024-09-10 14:57:34 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Masomo File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 69


Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 1: Hadithi ya safari saba za Sinbad
Hadithi hii inapatikana katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 2: Sehemu ya safari ya kwanza ya sinbad
Muendelezo wa stori ya safari ya Sinbad ambayo ipo kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 7 Part 7: Upendo uliotafsiriwa
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 3: Uokozi kwenye kisiwa
Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza...... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 26: Kaka wa tano wa kinyozi
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 9: Hadithi ya binti wa ndotoni.
Simulizi hii pia inapatikana kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 10 Part 2: Ni ndoto ama kweli???
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 7 Part 1: Aladini na taa ya mshumaa wa ajabu
Hii ni simulizi iliyopo ndani ya kitabu cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA...... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 16: Viatu vya ajabu vyaondoka na mkono wangu
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 13: Wageni wa Baraka kujongea
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 8: Simulizi ya chongo wa tatu mtoto wa mfalme
Muendelezo wa hadithi ya mtoto wa mfalme mwenye chongo katika hadithi ya HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 7: Mjakazi wa sultani
Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili ..... Soma Zaidi...