Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha tatu.....
MTUMWA WA AJABU
Kama wasemavyo waliokula chumvi nyingi kuwa muomba mungu hachoki, basi waziri Faridi aliendelea kuomba Mungu hata siku moja akapata taarifa kuwa kuna watumwa wametokea nchi za Uajemi. Hapo waziri alitabasamu kwani alifahamu sasa anakwenda kupata alilolitaka. Kwani alitambuwa kuwa maeneo hayo ndipo watumwa wenye sifa hizo wanapatikana. Basi alifika akauta kuna mabinti wasiopungua 150. waziri aliwaangalia vyema sana huku akagunduwa kuwa kuna wwengine walikuwa wakitabasamu. Alitambuwa kuwa hawa hawafai maana wanadiriki kuuza tabasamu lao bila ya sababu.
Kwa mara ya kwanza waziri akachaguwa walio wazuri kuliko wote. Aliamii kuwa mfalme angeanza kuangalia uzuri hata kabla ya kumthaminisha mtumwa wake. Katika mchujo huu akapata mabinti 21. kisha akaanza kuangalia sauti zao, nywele zao, nyusi na rangi za macho yao. Katika mchujo juu akabahatika kupata 12. kisha akaangalia vigezo vya elimu ya dini na dunia, hapa kabahatika kupata 5. kisha akaangalia hati za uanishi, na ufasaha wa kuzungumza hapa akabahatika kupata 3. sasa akaangalia kama wanafahamu kuburudisha hadhira na kumbrusisha mwanaume. Hapa ndipo akampata binti mmoja aliyefahamika kwa jina la An-neese.
Hakika binti huyu alikuwa mzuri aliyepitiliza vigzo vya sultani. Maana urefu wake haukuwa wa kuchuchumia, hakuhitaji kupaka mafuta ndipo kulainisha ngozi yake. Siku zote alitumia vyakula asili kuweza kuweka mwili wake katika afya na urembo. Hakuwa ni mkwaro wa sauti, mach meupe makubwa, yaliyopambwa na nyuzi nyeysi sana zilizotengeneza umbo la mwezi mwandamo. Nywele nyefu na ngumu zenye afya. Alitambuwa kusoma hati za lugha kadhaa zilizokuwa zikitumia maeneo yale kama kiarabu, kihindi, kiroam (latini) na baaadhi ya lugha za hispatia na fursi.
Waziri alikabidhi pesa palepale. Hapo muuzaji wa watumwa akampa ushauri waziri kuwa, “kwa ;leo usimpeleke kwa mfalme maana ametoka mbali,hivyo kwa uchovu alio nao, uzuri wake utajificha kidogo. Hivyo nakushauri, nenda naye kwanko kwa kiasi cha wiki na atakapozoea hali ya hewa uzurio wake utazidi mara dufu na hapo itakuwa vyema kumpeleka kwa mfalme. Waziri alikubwali ushauri huu japo kwa shingo upande akihofia mwanaye Nurdini.
Waziri siku hiyo alikuwa akirurahia na kuamini sasa amempata wazri Masoud. Ila alihitaji iwe ni mshangao hivyo hakuthubuti kumwambia yeyote kuwa amempata mtumwa wa mfalme. Basi siku hiyo wazir wakati anakwenda na mtumwa wake kwake kwa ushauri wa muuzaji alimueleza kila kitu kuwa awe mbali sana na Nurdin maana ataweza kumuharibia kwani hajawahi kuacha sketi ya mtumwa wala mfanyakazi aliyeletwa nyumbani.yule binti mtumwa akaahidi kuwa hatakuwa na mahusiano na Nurdini kabisa. Basi alipofika nyumbani akamueleza mke wake kila kitu na kumtaka ampatie mtumwa yule kila anachohitaji ili baada ya wiki kupita ampeleke kwaMfalme.
Binti mtumwa akatengewa eneo lake mwenyewe kwa ajili ya malazi na makazi. Mabinti wengine waliandaliwa kwa ajili ya kumpatia kila alichohitaji kuhakikisha kuwa anazea hali ya hewa na uzuri wake unaboreka. Hata hivyo baadhi ya vibinti vifanyakaz wa waziri walikuwa wakichukizwa na uwepowa mtumwa ambaye alikuwa ni kama malkia. Mtumwa ambaye alikuwa akifanyiwa kazi. Hakika mambo haya yalikuwa yakiwachokesha. Walikuwa wana kazi ya kumpikia, kumsugua anapokwenda kuoga, kumpamba na kumfanyia mambo mengine zaidi.
Mambo yote haya yalikuwa yakitokea bila ya Nurdini kutambuwa uwepo wa binti yule. Mambo haya yalifanywa kwa siri ili aibu kubwa isijempata Waziri. Waziri aliamini kuwa kama atamueleza Nurdini kuwa asijekwenda kumuona yule binti basi huenda Nurdini ndio angekwenda kwa makusudi, kwa ajili ya kuridhisha udadisi wake. Basi mambo yakawa kama hivyo haimaye siku mbili zikaisha na ya tatu ikaingia. Uzri wa binti ulikuwa ukiongezeka kila siku zinapozidi. Mawazo ya kubadili maamuzi ya waziri yalikuwa yakimjia. Na hata me wake wivu ulianza kumkamata ijapokuwa hakuweza kudhihirisha.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Mankaa Tarehe 2024-09-10 14:57:34 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Masomo File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 123
Sponsored links
👉1
Simulizi za Hadithi Audio
👉2
Kitabu cha Afya
👉3
Kitau cha Fiqh
👉4
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉5
kitabu cha Simulizi
👉6
Madrasa kiganjani
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 7: Mjakazi wa sultani
Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili ..... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 2 Part 1: Hadithi ya jini na mfanya biashara.
Hadithi hii ya jina na mfanya biashara imetoka katika kitabu cha kwanza cha simulizi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza karibu tusikilize simulizi nzuri na zakusisimua Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 13: Wageni wa Baraka kujongea
Muendelezo..... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 26: Kaka wa tano wa kinyozi
Muendelezo.... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 6: Sehemu ya tatu ya safari ya Sinbad
Muendelezo wa sehemu ya tatu ya safari ya Sinbad iliyopo kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA.... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 8 Part 1: Hadithi ya tunda
Simulizi hii pia inapatikana kwenye kitabu cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 22: Kaka wa kwanza wa kinyozi
Muendelezo.... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 3 Part 3: Kisa cha mke na kasuku
Simulizi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza simulizii hii inasimulia kisa cha mke na Kahuku wake.... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 16: Viatu vya ajabu vyaondoka na mkono wangu
Muendelezo..... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 10 Part 3: Asubuhi yenye varangati
Muendelezo.... Soma Zaidi...