Muendelezo.......
NURDINI AMLAGHAI MTUMWA.
Siku ya tano Nurdini alipata taarifa kutoka kwa watu wake yaani wafanyakazi wa chumba chake kuwa kuna binti mgeni ameletwa ila ametengewa sehemu yake maalumu. Na kuna walinzi wa kike hivyo haruhusiwi mwanaume yeyote kwenda hasahasa nurdini. Nurdini alitabasamu kusikia hivyo. Tabasamu lililowaacha wafanyakazi wa chumba chake mioyo yao kuwaenda mbio. hakikaNurdini alikuwa ni kijana mzuri. Sharubu zake fupi zilizokuwa zikichomoza kama mbegu za mpunga zinazoota sasa, pua iliuotokeza kwa mbele kidogo, mashavu yaliyojaza na kutengeneza uso usio duara kama wanawake wa nchi za Balkan.
Siku hiyo Nurdini hakuamua ubaya ila alitamani kwenda kumuona huyo mtumwa japo kwasiri. Alipenda kujiridhisha macho yake kama huyo mtumwa ni kiwango cha kuweza kuchukuliwa na mfalme kama ilivyokusudiwa na baba yake. Siku hiyo mtumwa alikwenda kuoga, Nurdin alitumia fursa hiyo kuingia chumbani kwa binti kisha akajificha nyuma ya pazia. Alipomaliza kuoga binti akaingia ndani, hapo Nurdini akajifanya anamtafuta mama yake. Wakati anaulizia yule binti akapatapo kusikia sautti ya kijana Nurdini, na hapo nafsi yake ikaingia udadisi kutaka kujuwa hasa kama sauti ya kijana huo imemridhisha kiasi kile vipi sura yake.
Binti akatoka kwenda varandani kumuona kijana aliyekuwa akimuuliza mama yake, Loo akakutana na sura nzuri. Hapo alitamani hata kumkumbatia, loo pepo la uchafu na hisia za uharibifu zikaanza kuzunguka kaiyao kama kibirinzi. Nurdini akajifanya kusema maneno ya uwongo “dah ivi wewe ndiye mtumwa ambaye baba yangu amekununua kwa ajili yangu, binti bila hata kufikiri akajibu “ndio bwana wangu”. Nurdini akasogea karibu, akamuangalia vyema, kisha akaongeza ukaribu hata pasibakie na nafasi kati yao. Nurdini akamuangalia vyema kisha akasema “kwa hakika baba amenichagulia mke na si mtumwa”
Maneno haya yalipenya ndani sana kwenye moyo wa binti na kuchokoa hisia zilizolala toka zamani sana. Kisha nurdini akaongeza “je utakubali kuwa mke wangu, ama kuwa mtumwa sehemu nyingine” nyundo ya mapenzi ikapenya ndani zaidi na kwenda kugonga msumari wa mapenzi uliokuwa umelegea kwenye moyo wa binti. Hapo akajikuta kuruhusu hisia zake kupokea Nurdini. Binti hakujibu kitu, ila kwa ishara ya macho Nurdini alishatambua jibu. Nurdini akamkumbatia na kumpusu, hapo binti akaanza kutetemeka. Hakuna hakika kama sababu I baridi, uwoga ama ndio mambo ymefana.
Wakiwa katika hali hiyo ghafla mlango ukafunguliwa na loo! Mama Nurdini akashuhudia wawili hawa wakiwa wamekumbatiana. Mama nurdini akaangalia vyema akagundua kuwa binti alikuwa bado amevaa zile nguo alizotoka nazo kuoga. Mama nurdini alikasirika sana, ila kwa upande wa pili aliona pia bora iwe hivi maana mwanzo alikuwa akimuonea wivu mtumwa kwa mumewe. Lakini sasa mwanaye ndiye amemchukuwa mtumwa kabla ya kufikishwa kwa mfalme. Kilichokuwa kikimpataaba mama ni kuwa mumwe wake mzee faridi atachukuwa maamuzi gani?
Nurdini kuona vile alikimbia kwa kumuogopa mama yake. Yule binti moyo ulimruka na kutamani ardhi ipasuke ili apotelee ardhini. Mama Nurdini alimpiga kibao kimoja kizito sana. “huna hata haya wewe, hivi ukaribu wote mume wangu aliokupa ndio unamuharibia hivyo, ataiweka wapi sura yake mume wangu pindi mfalme akigundua jambo hili, ivi unajuwa kuwa ulichokifanya unaweza kuhatarisha maisha ya familia nzima, ikiwemo huyo kibwana chako Nurdini, shetani mkubwa wewe” yalikuwa ni maneno ya mama Nurdini. Hakika yule mtumwa alijiona ni mkosaji sana. Kisha akasema “nisamehe mama, ila Nurdini ndio chaguo langu, la kwanza na ni la mwisho”.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Simulizii hii inapatikana katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA
Soma Zaidi...Muendelezo wa safari ya Sinbad.......
Soma Zaidi...Hii ni hadithi ya kitabu cha tatu cha hadithi za HALIF LELA U LELA...
Soma Zaidi...Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili....
Soma Zaidi...Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili.....
Soma Zaidi...Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili.....
Soma Zaidi...