image

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Nudhini na mtumwa

Muendelezo.......

NURDINI AMLAGHAI MTUMWA.

 

 

 

 

 

Siku ya tano Nurdini alipata taarifa kutoka kwa watu wake yaani wafanyakazi wa chumba chake kuwa kuna binti mgeni ameletwa ila ametengewa sehemu yake maalumu. Na kuna walinzi wa kike hivyo haruhusiwi mwanaume yeyote kwenda hasahasa nurdini. Nurdini alitabasamu kusikia hivyo. Tabasamu lililowaacha wafanyakazi wa chumba chake mioyo yao kuwaenda mbio. hakikaNurdini alikuwa ni kijana mzuri. Sharubu zake fupi zilizokuwa zikichomoza kama mbegu za mpunga zinazoota sasa, pua iliuotokeza kwa mbele kidogo, mashavu yaliyojaza na kutengeneza uso usio duara kama wanawake wa nchi za Balkan.

 

 

 

 

 

Siku hiyo Nurdini hakuamua ubaya ila alitamani kwenda kumuona huyo mtumwa japo kwasiri. Alipenda kujiridhisha macho yake kama huyo mtumwa ni kiwango cha kuweza kuchukuliwa na mfalme kama ilivyokusudiwa na baba yake. Siku hiyo mtumwa alikwenda kuoga, Nurdin alitumia fursa hiyo kuingia chumbani kwa binti kisha akajificha nyuma ya pazia. Alipomaliza kuoga binti akaingia ndani, hapo Nurdini akajifanya anamtafuta mama yake. Wakati anaulizia yule binti akapatapo kusikia sautti ya kijana Nurdini, na hapo nafsi yake ikaingia udadisi kutaka kujuwa hasa kama sauti ya kijana huo imemridhisha kiasi kile vipi sura yake.

 

 

 

 

 

Binti akatoka kwenda varandani kumuona kijana aliyekuwa akimuuliza mama yake, Loo akakutana na sura nzuri. Hapo alitamani hata kumkumbatia, loo pepo la uchafu na hisia za uharibifu zikaanza kuzunguka kaiyao kama kibirinzi. Nurdini akajifanya kusema maneno ya uwongo “dah ivi wewe ndiye mtumwa ambaye baba yangu amekununua kwa ajili yangu, binti bila hata kufikiri akajibu “ndio bwana wangu”. Nurdini akasogea karibu, akamuangalia vyema, kisha akaongeza ukaribu hata pasibakie na nafasi kati yao. Nurdini akamuangalia vyema kisha akasema “kwa hakika baba amenichagulia mke na si mtumwa”

 

 

 

 

 

Maneno haya yalipenya ndani sana kwenye moyo wa binti na kuchokoa hisia zilizolala toka zamani sana. Kisha nurdini akaongeza “je utakubali kuwa mke wangu, ama kuwa mtumwa sehemu nyingine” nyundo ya mapenzi ikapenya ndani zaidi na kwenda kugonga msumari wa mapenzi uliokuwa umelegea kwenye moyo wa binti. Hapo akajikuta kuruhusu hisia zake kupokea Nurdini. Binti hakujibu kitu, ila kwa ishara ya macho Nurdini alishatambua jibu. Nurdini akamkumbatia na kumpusu, hapo binti akaanza kutetemeka. Hakuna hakika kama sababu I baridi, uwoga ama ndio mambo ymefana.

 

 

 

 

 

Wakiwa katika hali hiyo ghafla mlango ukafunguliwa na loo! Mama Nurdini akashuhudia wawili hawa wakiwa wamekumbatiana. Mama nurdini akaangalia vyema akagundua kuwa binti alikuwa bado amevaa zile nguo alizotoka nazo kuoga. Mama nurdini alikasirika sana, ila kwa upande wa pili aliona pia bora iwe hivi maana mwanzo alikuwa akimuonea wivu mtumwa kwa mumewe. Lakini sasa mwanaye ndiye amemchukuwa mtumwa kabla ya kufikishwa kwa mfalme. Kilichokuwa kikimpataaba mama ni kuwa mumwe wake mzee faridi atachukuwa maamuzi gani?

 

 

 

 

 

Nurdini kuona vile alikimbia kwa kumuogopa mama yake. Yule binti moyo ulimruka na kutamani ardhi ipasuke ili apotelee ardhini. Mama Nurdini alimpiga kibao kimoja kizito sana. “huna hata haya wewe, hivi ukaribu wote mume wangu aliokupa ndio unamuharibia hivyo, ataiweka wapi sura yake mume wangu pindi mfalme akigundua jambo hili, ivi unajuwa kuwa ulichokifanya unaweza kuhatarisha maisha ya familia nzima, ikiwemo huyo kibwana chako Nurdini, shetani mkubwa wewe” yalikuwa ni maneno ya mama Nurdini. Hakika yule mtumwa alijiona ni mkosaji sana. Kisha akasema “nisamehe mama, ila Nurdini ndio chaguo langu, la kwanza na ni la mwisho”.

 

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Mankaa Tarehe 2024-09-10 14:58:17 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Masomo File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 68


Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Simulizi za Hadithi EP 1 Part 2: Simulizi ya kisa cha mfugaji na mkewe
Simulizii hii ni inatoka katika kitabu cha kwanza cha HALIF LELA U LELA Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Barua ya mfalme wa baghadad
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 5: Nani ni binti?
Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 10 Part 5: Safari ya kwenda nyumbani
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 23: Kaka wa pili wa kinyozi
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Nudhini akiwa hatiani
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Hadithi ya Nurdini Mtoto wa Waziri
Hii ni hadithi ya kitabu cha tatu cha hadithi za HALIF LELA U LELA... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 14: Wageni
Simulizii hii ni nzuri na ni mojawapo ya hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili...... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 4: Kilema mtanashati asiye na mkono
Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 20: Kinyozi maishani mwangu
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 12: Sehemu ya tano ya safari ya Sinbad
Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 2 Part 2: Hadithi ya mzee wa kwanza na mbuzi wake
Simulizi za HALIF LELA U LELA zipo nyingi sana na husikiliwa na kusomwa na wakubwa kwa wadogo pia hadithi hizi zimeenea duniani Kate zikisikilizwa na maelfu ya watu mbalimbali. Soma Zaidi...