Simulizi za Hadithi EP 7 Part 11: Ndani mwa junba la Aladini

Muendelezo....

NDANI YA JUMBA LA ALADINI

 

 

 

Hatimaye Aladini anaingia ndani, Loo! Alitamani kupiga kelele, huku ameziba mdomo wake kwa mshangao. Uzuri wa ndani ulikuwa mara dufu ya nje. Ukumbi kubwa ilio katika umbo la duara. Mlango mkuu wa kuingilia kwenye ukumbi ulukuwa na pazia la rangi ya kijivu. Maashindi ya kiarabu yaliyopangiliwa na kutengeneza umbo la uwa zuri lililoonekana kuchanua. Maandishi yalikuwa ya rangi za kuchanganyika huku rangi ya zambarau ikitawala vyema. “Marhaban bikum” yaani karibuni sana, yalikuwa ndio maneno yaliyoandikwa yalivyosomeka.

 

 

Zuria la rangi nyekundu lilitandikwa na kuenea ukumi mzima. Zuria lilikuwa na michirizi ya zambarau na kutengeneza madoa makubwa ya rangi ya buluu. Zuria lilichanganya rangi nyingine na kutengeneza mauwa majubwa yaliyo mazuri. Rangi za mauwa hayo zilifanana sana na rangi za magoya ya kanga. Yaani madoa meupe na meuzi. Madirisha makubwa yaliyongaa vyema na kuonyesha kwa ufasaha kilicho nje. Michirizi ya madirisha ilikuwa inavutia kama vile ni mikufu ya dhahabu iliyoning’inizwa kweye vipete vya madirisha.

 

 

Mapazia yaliyokunywa mafundo yalining’inia kwenye madirisha. Aladini aliliendea dirisha moja na kufungua pazia. Loo! Lilikuwa ni pazia zuri sana, lenye rangi ya kijivu kama lile pazia kubwa. Pazia lilikuwa na picha ya ndege yule aliyeunganisha roho mbili hizi. Alikuwa ni ndege mzuri sana kwa kumuangalia. Vipete kwa kuning’inizia pazia vilikuwa vya rangi ya ugoro iliyo wiva sana iliyochanganyika na michirizi ya rangi ya samawati na kutengeneza mabadilishano ya rangi kama pundamilia aliyenona. Pazia lilifunika diisha na kushuka kwa chini na kutengeneza sura ya kuvutia.

 

 

Meza kubwa iliyozungukwa na viti iliwekwa katikati ya chumba. Ibila shaka ni meza ya kulia chakula, kwani vitu vilivyoonekana kwenye meza vinasadivu yaliyomo. Masinia 6 yaliyofunikwa na makawa ya rangi ya samawati, yenye micirizi ya kahawiya kwa chini. Masinia yalingaa kama ni almazi iliyowekwa. Kabaesni kadogo kalikojaa vijiko, visahani na vitu vingine. Maji safi yalionekana kwenye jagi. Ni masafi sana kiasi cha kuonyesha kana kwamba jagi ni tupu. Aani anaonekana aliye upande wa pili kama ni kioo. Harufunzuri ilikuwa ikitokea kwnye meza kubwa.

 

 

Viti vikubw avyenye magodoro ya harir vilizunguka meza na kutengeneza duara lama kiota cha mayai ya kuku anayelalia. Viti vizuri vilivyokuwa vya rangi za kupendeza na kuwekwa vikuku nya lulu pembeni ya kila kimoja. Basi uzuri ulioje wa ndani ya jumba hili. Juu karabai mishumaa mikubwa ya rangi nyekundu na njano ilining’inizwa ikiwa kwenye matovu makubwa ya rangi ya zamabarau. Matovu yalionekana kuwa na vijiwe vya ranirangi vikining’inia hakuna aliyejuwa ni madini ya aina gani. Ila vijiwe hivi ifikapo usiku kuakisi mwanga kutoka kwenye mishumaa na kugeuka kama taa zinazowaka.

 

 

 

Mjakazi mkubwa aliyeandaliwa na mama Aladini akaanza kupanga kundi la wajakazi na wafanyakazi kila mmoja kwenda kwenye eneo lake la kazi. Mjakazi mwingine aliye mrefu zaidi na mzuri sana akamchukuwa Aladini na mke wake kuwapeleka kwenye chumba chao. Walikutana na mfululizo wa mapazia yasiyopungua 5 ynye rangi mbalimbali za kupendeza. Hatimaye wakakaribishwa na harufu nzuuri iliyotoka nyuma ya pazia lenye rangirangi kama uwa la waridi. Mjakazi akawakaribisha na kurudi nyuma, huku akimuashiria binti sultani sasa ni kazi kwake kuongoza njia.

 

 

Mjakazi akabakia pale pale, binti sultani akafungua pazia, Loo! Kitasa cha dhahabu kikawakaribisha. Aladini kwa mkono wake akafungua kitasa, mlango ukafunguka. Hatimaye wawili hawa wapo ndani, kinanukia sana chumba chao. Uzuri wa chumba na mapambo hakukuwa na tofauti sana ya kile chumba cha binti Sultani. Tofauti ni kuwa vitu vyake vilikuwa ni vya thamani sana. Hatimaye kwa uchovu wa safari wawili hawa wakaamuwa kupumzika na mlango ukafungwa.

 

 

Atimaye siku ikaenda hivyo na muda wa chakula ukafika, wakapata chakula kizuri. Mama Aladni aliendeela kuwa pale, ijapokuwa hakupendelea kuishi pale. Alitarajia baada ya ujio wa Sultani arudi nyumbani kwake. Mama Aladini ijapokuwa mambo yote alikuwa akiyashuhudia kwa macho yake lakini hakuwa akiamini hasa uhalisia na nini itakuwa hatima ya mambo yale. Hivyo hakutaka kulekeza maisha yake ya mwanzo kirahisi. Masi ambo yakawa hivyo na usiku ukaingia na hatimaye kukakucha.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Mankaa image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Burudani File: Download PDF Views 473

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 web hosting    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 11: Hadithi ya kisiwa cha mawe yanayolia

Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 14: Simulizi ya binti wa kwanza na mbwa

Tuendeleee kuburudika na simulizii zetu nzuri kutoka katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 2: Kisa cha kinyozi msiri..

Karibuni tuendelee kusimuliana stori za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza, stori nzuri sana na za kuvutia zimeandaliwa kwaajili ya kujifunza na kujiburudisha pia.....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 1 Part 1: Simulizi ya kiapo cha Sultan

Simulizi hii inatoka kwenye kitabu cha kwanza cha hadidhi za HALIF LELA U LELA.

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 2 Part 2: Hadithi ya mzee wa kwanza na mbuzi wake

Simulizi za HALIF LELA U LELA zipo nyingi sana na husikiliwa na kusomwa na wakubwa kwa wadogo pia hadithi hizi zimeenea duniani Kate zikisikilizwa na maelfu ya watu mbalimbali.

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 10: Mapenzi kwenye mtihani

Simulizii hii inapatikana katika kitabu cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 7: Hadithi ya safari ya majibu juu ya maswali mawili

Wapendwa wasomaji na wasikilizaji wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza karibu tuendelee kusikiliza hadithi zetu mzuri na za kusisimua....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 15: Hadithi ya safari ya Sinbad

Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza muendelezo....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 5: Nani ni binti?

Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili....

Soma Zaidi...