picha

Bara arabu enzi za jahiliyyah, jiografia ya bara arabu

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

BARA ARAB ZAMA ZA JAHILIYYAH, KARNE YA 6 A.D.

      7.1 Hali ya Bara Arab zama za Jahiliyyah.

-  Bara Arabu imezungukwa na bahari katika tatu, Magharibi kuna bahari ya Shamu, 

    Mashariki kuna Ghuba ya Uajemi na Oman, Kusini kuna bahari ya  Uarabuni na  

    Kaskazini ni Jangwa la Syria.

 

        -  Bara Arabu liko kati kati ya mabara matatu; Asia, Ulaya na Afrika.

                 -  Saudi Arabia ndio nchi kubwa kuliko zote Bara Arabu ambamo kuna miji mitakatifu 

                     ya Makkah na Madinah.

 

          -  Wakati anazaliwa Mtume mwaka 570 A.D (karne ya 6 A.D) dunia nzima ilikuwa 

                      katika giza totoro la ujahili.

          

        -  Maisha ya jamii yalikuwa yanaendeshwa kibabe na kibinafsi kwa kufuata matashi 

                      ya nafsi zao.

         

        -  Ubabe, ukandamizaji, unyonyaji, uporaji na dhuluma katika maisha yalionekana 

                     kama matendo ya kishujaa na kujivunia.

 

        -  Walizama katika ushirikina kiasi cha watu kuweza kutembea na miungu mifukoni 

                     mwao.

        -  Hali hii ya giza totoro ilienea pia nchi na mabara mbali mbali ulimwenguni kote.

 

        -  Dini kubwa zilizokuwepo muda huo zilikuwa ni Uyahudi na Ukristo lakini 

                     hazikuweza kumkomboa mwanaadamu kwa lolote hata kidogo.

 

        -  Hapakuwa na serikali, kila kabila lilikuwa na kiongozi na taratibu zake katika 

                    kuendeshea maisha. 

 

        -  Unyanyasaji wa wanawake kila nyanja, mauwaji ya watoto wa kike wakiwa hai 

            ilikuwa ni desturi ya kawaida katika maisha ya jamii ya Waarabu.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Views 2267

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 web hosting     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Vita vya Al Fijar na sababu zake

Historia na shida ya Mtume Muhammad S.A.W, sehemu ya 12. Hapa utajifunza kuhusu kutokea kwa vita vya al fijar.

Soma Zaidi...
Shukurani za Nabii Ibrahiim(a.s) kwa Allah(s.w)

Kwa neema hii ya kuruzukiwa watoto wawili - Ismail na Is- haqa(a.

Soma Zaidi...
Maswali kuhusu Quran

Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...