Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
BARA ARAB ZAMA ZA JAHILIYYAH, KARNE YA 6 A.D.
7.1 Hali ya Bara Arab zama za Jahiliyyah.
- Bara Arabu imezungukwa na bahari katika tatu, Magharibi kuna bahari ya Shamu,
Mashariki kuna Ghuba ya Uajemi na Oman, Kusini kuna bahari ya Uarabuni na
Kaskazini ni Jangwa la Syria.
- Bara Arabu liko kati kati ya mabara matatu; Asia, Ulaya na Afrika.
- Saudi Arabia ndio nchi kubwa kuliko zote Bara Arabu ambamo kuna miji mitakatifu
ya Makkah na Madinah.
- Wakati anazaliwa Mtume mwaka 570 A.D (karne ya 6 A.D) dunia nzima ilikuwa
katika giza totoro la ujahili.
- Maisha ya jamii yalikuwa yanaendeshwa kibabe na kibinafsi kwa kufuata matashi
ya nafsi zao.
- Ubabe, ukandamizaji, unyonyaji, uporaji na dhuluma katika maisha yalionekana
kama matendo ya kishujaa na kujivunia.
- Walizama katika ushirikina kiasi cha watu kuweza kutembea na miungu mifukoni
mwao.
- Hali hii ya giza totoro ilienea pia nchi na mabara mbali mbali ulimwenguni kote.
- Dini kubwa zilizokuwepo muda huo zilikuwa ni Uyahudi na Ukristo lakini
hazikuweza kumkomboa mwanaadamu kwa lolote hata kidogo.
- Hapakuwa na serikali, kila kabila lilikuwa na kiongozi na taratibu zake katika
kuendeshea maisha.
- Unyanyasaji wa wanawake kila nyanja, mauwaji ya watoto wa kike wakiwa hai
ilikuwa ni desturi ya kawaida katika maisha ya jamii ya Waarabu.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Makafiri wa Kiquraish walikuwa na tabia ya kumghasi Mtume(s.
Soma Zaidi...Historia na sifa ya Mtume Muhammad s.a.w , sehemu ya 14. Hapa utajifunza kuhusu kazi alizozifanya Mtume s.a.w Enzo za ujana wake kabla ya utume.
Soma Zaidi...Uasi katika dola ya kiislamu na matokeo yake.
Soma Zaidi...Tukirejea Qurβan (11:36-48) na (23:26 -29) tunapata maelezo juu ya mchakato wa kuangamizwa makafiri na kuokolewa waumini katika kaumu ya Nabii Nuhu(a.
Soma Zaidi...Njaa ilitokea na ikawa hapana sehemu nyingine yoyote yenye chakula ila Misri.
Soma Zaidi...Baada ya mikataba miwili ya βAqabah na baada ya Waislamu 75 kufika Yathrib salama, Mtume(s.
Soma Zaidi...