Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
BARA ARAB ZAMA ZA JAHILIYYAH, KARNE YA 6 A.D.
7.1 Hali ya Bara Arab zama za Jahiliyyah.
- Bara Arabu imezungukwa na bahari katika tatu, Magharibi kuna bahari ya Shamu,
Mashariki kuna Ghuba ya Uajemi na Oman, Kusini kuna bahari ya Uarabuni na
Kaskazini ni Jangwa la Syria.
- Bara Arabu liko kati kati ya mabara matatu; Asia, Ulaya na Afrika.
- Saudi Arabia ndio nchi kubwa kuliko zote Bara Arabu ambamo kuna miji mitakatifu
ya Makkah na Madinah.
- Wakati anazaliwa Mtume mwaka 570 A.D (karne ya 6 A.D) dunia nzima ilikuwa
katika giza totoro la ujahili.
- Maisha ya jamii yalikuwa yanaendeshwa kibabe na kibinafsi kwa kufuata matashi
ya nafsi zao.
- Ubabe, ukandamizaji, unyonyaji, uporaji na dhuluma katika maisha yalionekana
kama matendo ya kishujaa na kujivunia.
- Walizama katika ushirikina kiasi cha watu kuweza kutembea na miungu mifukoni
mwao.
- Hali hii ya giza totoro ilienea pia nchi na mabara mbali mbali ulimwenguni kote.
- Dini kubwa zilizokuwepo muda huo zilikuwa ni Uyahudi na Ukristo lakini
hazikuweza kumkomboa mwanaadamu kwa lolote hata kidogo.
- Hapakuwa na serikali, kila kabila lilikuwa na kiongozi na taratibu zake katika
kuendeshea maisha.
- Unyanyasaji wa wanawake kila nyanja, mauwaji ya watoto wa kike wakiwa hai
ilikuwa ni desturi ya kawaida katika maisha ya jamii ya Waarabu.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
KUANGAMIZWA KWA JESHI LA TEMBOTukio la pili ni lile tukio la tembo, na ilikuwa hivi:- Kiongozi mmoja wa kiyemeni aliyetambulika kwa jina la Abrah aliona waarabu kutoka maeneo mbalimbali wanafunga misafara kuelekea Makkah kwa lengo la kwenda kuhiji.
Soma Zaidi...MAPIGANO YA AL-FIJAR (MAPIGANO YA UOVU).
Soma Zaidi...Mtume Ilyasa ni mmoja wa Mitume waliotumwa kupitia kizazi cha Bani Israil.
Soma Zaidi...Kutokana na Historia ya Nabii Musa na Harun(a.
Soma Zaidi...KULELEWA NA MAMA YAKE ALIPOFIKA MIAKA MINNEMtume (s.
Soma Zaidi...