HISTORIA YA NABII IBRAHIIM(A.S) NA KUANDALIWA KWAKE:

Nabii Ibrahiim(a.

HISTORIA YA NABII IBRAHIIM(A.S) NA KUANDALIWA KWAKE:

HISTORIA YA NABII IBRAHIIM(A.S) NA KUANDALIWA KWAKE:

Nabii Ibrahiim(a.s) ni Mtume wa Allah(s.w) aliyemfuatia Salih(a.s) katika wale waliotajwa katika Qur-an. Alizaliwa na kulelewa katika mji wa Ur huko Iraq. Baba yake,Azara,alikuwa akichonga masanamu na kuyauza kwa washirikina waliokuwa wakiyaabudu badala ya Allah(s.w). Hivyo ni wazi kuwa NabiiIbrahiim(a.s) aliletwa kwa jamii iliyozama katika giza la ushirikina.



Kuandaliwa kwa Nabii Ibrahiim(a.s)
Tangu angali mdogo, NabiiIbrahiim(a.s) aliyakinisha kuwepo kwa Allah(s.w) kwa kuchunguza dalili zilizomzunguka katika maumbile ya mbingu na ardhi. Baada ya kuyakinisha kuwepo kwa Allah(s.w), alichukua azma ya kumtii kwa unyenyekevu katika maisha yake yote kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:



“(Kumbukeni habari hii) Mola wake (Ibrahim) alipomwambia “Silimu” (Jisalimishe) akanena: Nimejisalimisha kwa Mola wa walimwengu wote”. (2:131)



Imani yake ya kweli juu ya Allah(s.w), ilimpelekea kuwa na tabia njema isiyo na mfano wake katika jamii kama tunavyojifunza katika Qur-an:

Hakika Ibrahim alikuwa Imamu (mfano mzuri wa wema wa kuigwa), mnyenyekevu kwa Mwenyezi Mungu, mtii kamili, wala hakuwa miongoni mwa washirikina.(16:120)



(Alikuwa) mwenye kuzishukuru neema Zake (Mwenyezi Mungu zilizo juu yake), akamchagua na kumuongoza katika njia iliyonyooka. Na tukampa wema katika dunia; na hakika yeye katika Akhera atakuwa miongoni mwa watu wema (pia). (16:121-122)

“...........Kwa yakini Ibrahim alikuwa mwingi wa kurejea kwa Mwenyezi Mungu na mvumilivu”. (9:114)



“Na mtaje Ibrahim katika kitabu (hiki) bila shaka yeye alikuwa mkweli sana, Nabii.” (19:41)



Kutokana na aya hizi tunajifunza kuwa NabiiIbrahiim(a.s) alikuwa Hanifa, yaani aliyejiepusha na Dini za upotevu na hakuwa mshirikina. Alikuwa mnyenyekevu kwa Allah(s.w) na mtii kamili. Alikuwa mwenye kushukuru neema za Allah(s.w), alikuwa mkweli, mwingi wa kurejea kwa Allah(s.w) na alikuwa mvumilivu. Pia alikuwa mwepesi katika kukirimu wageni kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:



“Na wajumbe wetu walimwendea Ibrahim kwa bishara, (njema) wakasema: “Salaam – amani”, akasema (Ibrahim). “Juu yenu pia iwe amani”. Na hakukaa (Ibrahim) ila mara alileta ndama (aliyechomwa vizuri).” (11:69)



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 5850

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

MJADALA JUU YA NDOA YA MTUME S.A.W NA BI KHADIJA (HADIJA)

LAKINI UMRI WANGU MKUBWABaada ya kuwaza na kufikiri muda mrefu, bibi Khadija (Radhiya Llahu anha) akafikia uamuzi wa kutaka kuolewa na Muhammad (Swalla Laahu alayhi wa sallam).

Soma Zaidi...
MTUME MUHAMMAD (S.A.W)ANAKUTANA NA BAHIRA (MTAWA WA KIYAHUDI)

KUKUTANA NA BAHIRA (MTAWA) WA KIYAHUDIMzee Abu talib alikuwa ni mfanya biashara, hivyoslikuwa akimchukuwa kijana wake kwenda kwenye biashara.

Soma Zaidi...
KUCHIMBWA UPYA KWA KISIMA CHA ZAMZAMA NA KUNYWA MAJI YA ZAMZAMA KISIMA KILICHO BARIKIWA

KUCHIMBWA UPYA KISIMA CHA ZAMZAMKwa kifupi ni kuwa Abdul-Muttalib alipata agizo kutoka ndotoni kuwa achimbe kisima cha zamzam, na akaelekezwa sehemu ya kupachimba.

Soma Zaidi...
Kujengwa upya al Kabah baada ya kuwa na mipasuko.

Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w sehemu ya 18. Hapa utajifunza kuhusu tukio la kujengwa upya kwa al kaaba 🕋

Soma Zaidi...