HISTORIA YA NABII IBRAHIIM(A.S) NA KUANDALIWA KWAKE:

Nabii Ibrahiim(a.

HISTORIA YA NABII IBRAHIIM(A.S) NA KUANDALIWA KWAKE:

HISTORIA YA NABII IBRAHIIM(A.S) NA KUANDALIWA KWAKE:

Nabii Ibrahiim(a.s) ni Mtume wa Allah(s.w) aliyemfuatia Salih(a.s) katika wale waliotajwa katika Qur-an. Alizaliwa na kulelewa katika mji wa Ur huko Iraq. Baba yake,Azara,alikuwa akichonga masanamu na kuyauza kwa washirikina waliokuwa wakiyaabudu badala ya Allah(s.w). Hivyo ni wazi kuwa NabiiIbrahiim(a.s) aliletwa kwa jamii iliyozama katika giza la ushirikina.



Kuandaliwa kwa Nabii Ibrahiim(a.s)
Tangu angali mdogo, NabiiIbrahiim(a.s) aliyakinisha kuwepo kwa Allah(s.w) kwa kuchunguza dalili zilizomzunguka katika maumbile ya mbingu na ardhi. Baada ya kuyakinisha kuwepo kwa Allah(s.w), alichukua azma ya kumtii kwa unyenyekevu katika maisha yake yote kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:



“(Kumbukeni habari hii) Mola wake (Ibrahim) alipomwambia “Silimu” (Jisalimishe) akanena: Nimejisalimisha kwa Mola wa walimwengu wote”. (2:131)



Imani yake ya kweli juu ya Allah(s.w), ilimpelekea kuwa na tabia njema isiyo na mfano wake katika jamii kama tunavyojifunza katika Qur-an:

Hakika Ibrahim alikuwa Imamu (mfano mzuri wa wema wa kuigwa), mnyenyekevu kwa Mwenyezi Mungu, mtii kamili, wala hakuwa miongoni mwa washirikina.(16:120)



(Alikuwa) mwenye kuzishukuru neema Zake (Mwenyezi Mungu zilizo juu yake), akamchagua na kumuongoza katika njia iliyonyooka. Na tukampa wema katika dunia; na hakika yeye katika Akhera atakuwa miongoni mwa watu wema (pia). (16:121-122)

“...........Kwa yakini Ibrahim alikuwa mwingi wa kurejea kwa Mwenyezi Mungu na mvumilivu”. (9:114)



“Na mtaje Ibrahim katika kitabu (hiki) bila shaka yeye alikuwa mkweli sana, Nabii.” (19:41)



Kutokana na aya hizi tunajifunza kuwa NabiiIbrahiim(a.s) alikuwa Hanifa, yaani aliyejiepusha na Dini za upotevu na hakuwa mshirikina. Alikuwa mnyenyekevu kwa Allah(s.w) na mtii kamili. Alikuwa mwenye kushukuru neema za Allah(s.w), alikuwa mkweli, mwingi wa kurejea kwa Allah(s.w) na alikuwa mvumilivu. Pia alikuwa mwepesi katika kukirimu wageni kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:



“Na wajumbe wetu walimwendea Ibrahim kwa bishara, (njema) wakasema: “Salaam – amani”, akasema (Ibrahim). “Juu yenu pia iwe amani”. Na hakukaa (Ibrahim) ila mara alileta ndama (aliyechomwa vizuri).” (11:69)



                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 4081

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Mafunzo yatokanayo na upinzani wa maquraish dhidi ya uislamu

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Makubaliano ya Mkataba wa Al Fudhul

Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 13. Hapa utajifunza historia ya Mkataba wa al fudhul na makubaliano yake.

Soma Zaidi...
HISTORIA YA KUJENGWA UPYA KWA AL-KA'BAH (NYUMBA TUKUFU YA ALLAH)

KUJENGWA UPYA KWA AL-KA’ABAHItambulike kuwa Al-ka’abah ndio mjengo wa kwanza kujengwa duniani.

Soma Zaidi...
vita vya ahzab, sababu ya kutokea vita hivi na mafunzo tunayoyapata

Vita vya Ahzab- Maquraish waliungana na mayahudi, wanafiki na makabila mengine ya waarabu baada ya kuona kuwa wao peke yao hawawezi kuufuta Uislamu.

Soma Zaidi...