Dalili za kujifunguwa, na dalili za uchungu wa kujifunguwa

Nitajuwaje kama mjamzito amekaribia kujifunguwa, ni dalili gani anaonyesha, dalili za uchungu wa kujifunguwa

Dalili za kujifunguwa, na dalili za uchungu wa kujifunguwa



DALILI ZA KUJIFUNGUWA HATUA KWA HATUWA:

Ni ndoto za wanawake wengi siku moja abebe ujauzito, azae mtoto kisha aitwe mama. Haswa hata wanaume hupendelea hivyo. Ila mwanamke anapofikia kujifunguwa hapa ndipo kizaazaa huonekana. Sasa makala hii itakwenda kukueleza dalili za kujifunguwa.

Daliili za kukaribia kujifunguwa kwa siku kadhaa
1.Maumivu ya nyonga kuongezeka
2.Uchovu kuongezeka
3.Kutoa damu yenye utelezi
4.Viungo kuachia
5.Njia ya kuzalia kutanuka zaidi.
6.Maumivu ya tumbo kuongezeka.
7.Maumivu ya tumbi na kutungwa.
8.Kuharisha
9.Maumivu ya mgongo kuongezeka



Dalili za kujifunguwa kwa masaa machache:
1.Mikazo ya tumbo inayotokea katika muda maalumu
2.Kutokwa na damu yenye utelezi
3.Kutokwa na utelezi kwa wingi
4.Njia kuachia zaidi
5.Mtoto kushuka karibu na njia ya kutokea.



Uchungu wa kujifunguwa:
Uchungu wa kujifunguwa hauwezi kuelezeka kwa maandishi machache haya. Hata hivyo kuna machache naweza kukueleza ijapokuwa huwenda usiwe uhalisia. Kujifunguwa kunapitia hatuwa kuu tatu ambazo ni kama ifuatavyo:-



1.Katika hatuwa ya kwanza
cevix (mlango wa mimba) hulegea na kufumguka kwa sentimita 10. hata hivyo kulegea kwa cevix kunaweza kuanza siku chache nyma, kidogo kidogo. Majimaji yanayotoka ukeni huongezeka baada ya kupasuka kwa utando uliomzunguka mtoto. Katika hatuwa hii mikazo ya tumbo la kujifunguwa yanaweza kuwa makali sana ndani ya sekunde 30 mpaka 60 kisha yanakata kwa dakika kama 4 ama 5 kisha huanza tena kama hivi.



Katika hatuwa hii maumivu yanaweza kuwa makali sana kiasi cha kuwa kama vile hayakati. Hapa mtoto anaanza kusogea kwenye njia ya kuzalia. Wakati huu atakuwa ana sukumana na njia ya haja kubwa na hapa mwanamke anaweza kujisikia kuenda haja kubwa. Baadhi ya wanawake walio mara ya kwanza kupata ujauzito wanaweza kwenda chooni na hatimaye anazalia chooni. Kumbuka mikazo ya tumbo haupoi hata kwa dawa za kukata maumivu.



2.Hatua hii ya pili
Hatuwa hii huanzia toka pale mlango wa kuzalia unapofunguka hadi mwisho (sentimita 10) mpaka mtoto atakapozaliwa. Mikazo ya tumbo katika hatuwa hii inazidi na kuwa katika mpangilio maalumu kwa kuachana. Kila mkazo unapokuwa mkubwa hapa mwanamke atajihisi kusukuma mtoto. Hapa mwanamke atahisi moto kwenye uke wake wakati mtoto anashuka ama atahisi kutanuka kwa uke wake hasa pale kichwa cha mtoto kinapoanza kutoka.



Kipindi hiki mama mamzito atakuwa anapewa maelekezo kuhuku kusukuma mtoto ili kuwezehsa kuzaa kwa haraka. Kuna mengi ambayo daktari ama anayezalisha atatakiwa kuyafanya hapa ili kuwezesha kujifunguwa kwa salama. Mtoto ataanza kutokeza kichwa kisha shingo ikifuatiwa na mabega na baadaye mwili kumalizia. Katika hatuwa hii wahudumu wa afya huwa makini zaidi maana ndio hatuwa yenye hatari sana. Hatuwa hii kwa wanawake ambao ndio ujauzito wao wa kwanza inaweza kuchukuwa lisaa limoja mpaka masaa mawili (1 - 2)



3.Hatuwa ya tatu
Hatuwa hii huanza pale mwanamke atakapojifunguwa. Hatua hii huhu huhusisha kutowa placent, ama kondo la uzazi. Hatuwa hii inaweza kuchukuwa mpaka dakika 30. upotevu wa damu hapa utaendelea kuwepo ijaokuwa si mkubwa. Mikazo ya tumbo la uzazi itasaidia kupunguza upotevu wa damu. Kitukibaya zaidi katika hatuwa hii ni endapo damu itatoka kwa wingi.



Hali hii inaweza kupelekea tatizo lijulikanalo kama postpartum haemorrhage na kupelekea upungufu wa damu na uchovu. Hivyo wakunga na wahudumu wataendelea kuwa makini sana katika hatuwa hii. Katika hatuwa hii ndipo mtoto atatenganishwa na placenter.





NINI UFANYE UKIWA KATIKA UCHUNGU WA KUJIFUNGUA KATIKA
1.Kunywa maji ama juisi kwa wingi ama chai
2.Unaweza pia kula kitu kitamu cha kufyonza kama utaruhusiwa. Hii ni kwa ajili ya kukuongezea nguvu
3.Badilisha mikao kuaa, kulala, ubavuubavu, chalichali, kusimama na kukaa na kadhalika)
4.Kama utaweza kuoga maji ya moto fanya hivyo kabla ya kuingia leba
5.Mwambie msimamizi wako kama ataruhusiwa kuingia akufanyie maseji mgongoni ana akusuguesugue
6.Jitahidi kurilax kati ya mikazo ya tumbo usisukume mtoto mpaka uambiwe kufanya hivyo
7.Unaweza kuomba dawa za maumivu kama utaruhusiwa.
8.Usione aibu hata kidogo ukiwa katika leba. Hao unaowaonea aibu wameshaona kila kitu kwako na kwa watu wengine. Kama unataka kulia lia sana, tambuwa kuwa kila kitakachokutokea hapo ni siri na katu hakuna atakayehadithia, hata hivyo kila kitu ni kawaida sana katika leba.
9.Fuata maelekezo kama utakavyoambiwa na wahudumu wako. Kosa lolote utakalofanya kumbuka linaweza kuhatarisha maisha yako na ya mtoto wako.



Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Download App yetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 9835

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Hatua za ukuwaji was mimba na dalili zake

Somo hili linakwenda kukuletea hatua za ukuaji mimba na dalili zake

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuacha kupiga punyeto.

Post hii inakwenda kukupa njia za kukusaidia kuacha punyeto.

Soma Zaidi...
NAMNA YA KUITAMBUA SIKU HATARI YA KUPATA MIMBA (UJAUZITO)

SIKU YA KUPATA UJAUZITO Mimba hutokea pindi mbegu ya kiume (sperm) inapokutana na yai la mwanamke (ova) na kuungana kwa pamoja kutengeneza selli moja iitwayo zygote.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya tetracycline katika kupambana na bakteria

Post hii inahusu zaidi dawa ya tetracycline katika kupambana na bakteria,ni mojawapo ya antibiotics au anti bacteria ambayo upambana na bakteria kama tutakavyoona hapo mbeleni.

Soma Zaidi...
Kazi ya homoni ya testosterone

Posti hii inahusu zaidi kazi ya homoni ya testosterone, hii homoni kwa kiwango kikubwa ukutwa kwa wanaume ndiyo homoni ambayo umfanya mwanaume aonekane jinsi alivyokuwa na sifa zake zote.

Soma Zaidi...
Mwenye ujauzito wa wiki moja na ana u.t.i anaweza kutumia dawa za aina gani ambozo zitakua salama kwa kiumbe kilichoanza kukua?

Ujauzito unaweza kutoka kwa sababu nyingi kama maradhi, madawa, vyakula na ajali. Unawezakutoa mimba bila kujuwa amakwakujuwa. Damu kutoka ni moja ya dalili za kutoka kwa mimba hata hivyo maumivu ya tumbo huweza kuandamana na damu hii.

Soma Zaidi...
Post hii inahusu zaidi umuhimu wa kondo la nyuma

Kondo la nyuma ni sehemu ya mwili wa mama anapokuwa mjamziti,kondo la nyuma husaidia katika kazi mbalimbali katika ukuaji wa mtoto.

Soma Zaidi...
Dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza

Soma Zaidi...
Mambo yanayodhihirisha afya ya nguvu za kiume

Posti hii inahusu zaidi mambo mbalimbali yanayodhoofisha afya za wanaume, kwa wakati mwingine wanaume ukosa kujiamini kwa sababu ya mambo ambayo yanaadhiri afya za wanaume.

Soma Zaidi...
Mm tumbo linaniuma mara kwa mara na linakua kama linages alaf kichwa kinauma mara kwa mara na nakosa choo wakati mwingine na kiuno kinauma je?inawezakua n ujauzito? Maana nilshirki tendo la ndoa siku ya tano baada ya kutoka hedhi

Dalili za mwanzo za ujauzito zinaweza kuwa ni changamoto kwamwanamke hasa ikiwa ndio mimba yake ya kwanza. Maumivu ya tumbo, kujaa kwa tumbo gesi, kukosa choo ama hamu ya kula na kadhalika huweza pia kuambatana na ujauzito.

Soma Zaidi...