Mikataba ya aqabah

Mikataba ya aqabah

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

   -  Hii ilikuwa ni baina ya Mtume (s.a.w) na watu wanaotoka nje ya mji wa   

      Makkah hasa waliokuja kuhiji msimu wa Hija.

 

   -  Mtume (s.a.w) alikutana na kikosi cha kwanza kabisa cha watu sita (6) 

      kutoka Madinah (Yathrib) wa kabila la Khazraj, baada ya kuwafikishia 

      ujumbe wa Uislamu, walisilimu na wakaahidi kuufikisha kwao Madina.

 

  -  Mwaka uliofuata, 621 A.D, kikundi kingine cha waislamu 12 (2 Aus na 

     10 Khazraj) walikutana na Mtume (s.a.w) kwa siri eneo la ‘Jaratul 

     ‘Aqabah’ na kuweka mkataba wa kwanza wa ‘Aqaba na kukubaliana 

      yafuatatayo;

  1. Hawataabudu chochote isipokuwa Allah (s.w) pekee.
  2. Hawataiba wala hawatapokonya misafara ya biashara njiani.
  3. Hawatazini.
  4. Hawatawaua watoto wao tena.
  5. Hawatasema uongo wala hawatawasingizia wengine uovu.
  6. Hawatamuasi Mtume kwa kila atakalowaamrisha na watakuwa waaminifu kwake kwa hali yeyote iwayo.

 

                -  Mtume (s.a.w) aliwapa mwalimu wa kuwafundisha Uislamu, ‘Mus’ab bin 

                             Umair.

                -  Mwaka uliofuata, 622 A.D.walimjia Mtume (s.a.w) waislamu 75   

    (wanawake 2) wakiongozwa na mwalimu wao, ‘Mus’ab na kufunga   

    Mkataba wa pili wa ‘Aqabah sehemu ile ile kwa kukubaliana kuwa;

 

               

                -  Mtume (s.a.w) aliwachagulia viongozi 12 (9 Khazraj na 3 Aus) na watu 

                             watakaokuwa chini ya kila kiongozi, na wanaume wote walimpa Mtume 

                            (s.a.w) mkono wa bai’at kwa maana ya utii wao kwake.

 

                -  Baada ya kikundi hicho kurejea na kufika Madinah salama, ndipo Mtume 

                            (s.a.w) aliwatangazia waislamu wote wa Makkah kuhamia Madinah.

 

                -   Na takriban baada ya miezi miwili hivi, Waislamu wote wenye uwezo wa   

                            kuhama walishahamia Yathrib (Madinah) kwenda kujiimarisha zaidi.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 2066

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana: