Makala hii inakwenda kukueleza faida za kula maboga, na mbegu zake kwa afya yako
19. Boga (pumpkin)
Boga ni katika vyakula vya asili walivyotumia mababu zetu toka enzi za zamani sana. Boga ni katika chakula chenye vitamin A. pia boga husaidia katika kushusha presha kwani mna kwenye mbegu za maboga aina ya mafuta pytoestrogens ambayo ndio hupunguza shinikizo la damu (hypertension).
Maboga husaidia katika ku[ata usingizi mnono kwani mna kwenye mbegu za maboga typtophan aina ya amino asid ambayo husaidia katika kurelax. Pia mna beta-carotene na aina zingine za antioxidant ambazo husaidia katika kuzuia kupata cancer.
Maboga ni muhimu katika kuboresha na kuimarisha afya ya nguvu za kiume. Pia chakula hiki ni muhimu kwa afya ya moyo. Kwani kutokana na kambakamba zilizomo kwenye maboga mlaji anakuwa na nafasi ndogo sana ya kuweza kupata mabonjwa ya moyo (coronary heart diseases).
Chakula cha maboga pia husaidia katika kuzuia na mlaji kupata ugonjwa wa kisukari. Pia huimarisha vyema afya ya mwenye kisukari. Chakula hiki husaidia katika ufyonzwaji wa glucose kwenda kwenye tishu za mwili. Pia husaidia katika kubalans kiwango cha sukari ndani ya mwili.
Maboga husaidia katika kuboresha na kuimarisha mfumo wa kinga mwilini (immune system). kwani vitamin C pamoja na beta-carotene husaidia mara dufu katika kuimarisha mfumo wa kinga ili kuweza kupambana na maradhi mbalimbali mwilini. Isitoshe beta-carotene kuweza kubadilishwa kuwa vitamin A, na hali hii huweza kusaidia katika kuzalishwa kwa seli hai nyeupe mwilini ambazo ndio hupambana na maradhi na vijidudu vishambulizi kama bakteria, fangas na virusi.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Somo Hili linakwenda kukuletea vyakula vyeny maji kwa wingi na umuhimu wake mwilini
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula topetope
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi faida mbalimbali ambazo anaweza kuzipata mtu anayetumia kachumbari, tunajua wazi kwamba kachumbari ni mchanganyiko wa nyanya, vitunguu maji,kabichi,na pilipili kidogo.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vyakula vya hatari kwa mjamzito hasa mimba changa
Soma Zaidi...zijuwe faida za kula njegere kiafya na umuhimu wa kula jegere pia jifunze njegere zina kazi gani mwilini?
Soma Zaidi...Mpaka sasa hakuna dawa ya kuponyesha saratani wala kinga ya saratani. Hata hivyo vipo vyakula ambavyo vinakadiriwa kuwa hupunguza hatari ya kuweza kupata saratani. Je unadhani uyoga ni moja ya vyakula hivyo?
Soma Zaidi...Zitambue aina zote za vyakule na ufanye maamuzi yaliyo kuwa sahihi katika uandaaji wa chakula chako
Soma Zaidi...