MALARIA INATOKEAJE? (Namna ambavyo malaria inatokea, inaanza na inavyoathiri afya)

Kama tulivyokwisha kuona kuwa malaria inaweza kuambukizwa kwa kung'atwa na mbu aina ya anophelesi.

MALARIA INATOKEAJE? (Namna ambavyo malaria inatokea, inaanza na inavyoathiri afya)

NAMNA AMBAVYO MALARIA HUTOKEA

Kama tulivyokwisha kuona kuwa malaria inaweza kuambukizwa kwa kung'atwa na mbu aina ya anophelesi. basi tambua kuwa ni mbu jike tu ndiye huweza kuambukiza malaria.  basi hapa nitakueleza namna ambavyo malaria huweza kutokea.

 

kwanza kabisa lazima kuwepo kwa vimelea vya malaria aidha kwa mtu ama kwenye mwili wa mbu jike aina ya anophelesi. vimelea hivi vya malaria vinaanza kuzaliana kwenye mwili wa mbu jike. baada ya siku 10 mpaka 18 vimelea hivi vinakomaa na kuwa kimelea kipya kinachojulikana kama sporozoite. Kisha hivi vimelea vingi vinahamia kwenye tezi za mate za mbu na hatimaye kuingia kwenye mate ya mbu.

 

Mdomo wa mbu una mirija mikuu miwiliu. Mmoja ni wa kunyonyea damu na mwingine ni wa kutolea mate. Wakati anapong'ata mtu mate yake huingia kwenye mwili wa mtu. Mate haya yakiwa yana vimelea vya malaria (sporozoite) vijidudu hivi huingia kwenye mwili wa mtu. Na hapa hatua nyingine ya vimelea hivi inaanza.

 

Vimelea hivi (sporozoite) vinapoingia kwenye mwili wa mtu moja kwa moja vinaelekea kwenye ini. na huko huanza kukuwa na kuwa schizonts baadaye hupasuka na kutoa merozoites hivi ni vimelea vipya vilivyokomaa. vimelea hivi kama havitapatiwa dawa ya kuondolewa vitaendelea kwenye mfumo wa damu na kuanza kushambulia seli nyekundu za damu.

 

Baada ya merozoite kupatikana huelekea kwenye mfumo wa damu na kuanza kushambulia seli hai nyekundu za damu na kuanza kuzaliana humo kwa mara nyingine na kuleta vimelea vipya vitambulikavyo kama schizont na baadaye kupasuka na kutoa vimlea waitwao merozoites.

 

Na hapa sasa vimelea hawa wapya wanaanza kushambulia seli hai nyekundi na kuzaliana humo kisha seli hupasuka na kuleta vimelea wengi zaidi. Na kuanzia hapa ndipo mgonjwa sasa ataanza kuona dalili za malaria kama homa, maumivu ya kichwa, tumbo, misuli na viungo, kichefuchefu, kutapika na kuharisha.

 

Kama vimelea hivi havitatibiwa athari zaidi itatokea na kuanza kushambulia maeneo mengine ya mwili kama ini, figo, mapafu na moyo. hapa mgonjwa ataweza kuchanganyikiwa, matatizo ya ini na figo, kupumua kwa shida ama kuhohoa. Kama mgonjwa hatatibiwa athari zaidi inaweza kutokea kama kupoteza fahamu na hatimaye kifo.

 


                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 864

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Maambukizi kwenye mfumo wa usagaji chakula unaotokea kwenye utumbo mkubwa (diverticulitis)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na mifuko midogo midogo, iliyobubujika ambayo inaweza kuunda kwenye utando wa mfumo wako wa usagaji chakula. Wao hupatikana mara nyingi katika sehemu ya chini ya utumbo mkubwa (koloni). Hali hiyo inajulikana kama Divert

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu ya tumbo kitovuni

Somo hili linakwenda kukuletea sababu za maumivu ya tumbo kitovu i

Soma Zaidi...
MATIBABU YA VIDONDA VYA TUMBO

MWISHO Vidonda vya tumbo vinatibika bila ya shaka.

Soma Zaidi...
Zijue sababu za moyo kutanuka.

Posti hii inahusu zaidi sababu za moyo kutanuka, Kuna kipindi ambapo moyo utoka kwenye hali yake ya kawaida na kutanuka hali ambayo usababisha madhara kwa mwenye tatizo hilo, ila Kuna sababu ambazo usababisha moyo kutanuka kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
Dalili za uvimbe kwenye kinywa

Post hii inahusu dalili za uvimbe kwenye kinywa ambapo kitaalamu hujulikana Kama oral candidiasis Uvimbe kwenye kinywa husababisha vidonda vyeupe, kwa kawaida kwenye ulimi au mashavu ya ndani. Wakati mwingine uvimbe kwenye kinywa huweza ku

Soma Zaidi...
Nini kinasababisha kizunguzungu?

Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili za kizunguzungu zinazotekea katika mwili wa binadamu

Soma Zaidi...
Koo langu limekauka yaweza kuwa ni muadhirika?

kuwashwa na koo ni katika dalili za kuwa na maambukizi mwilini. Kuwa na maambukizi haimaanishi ni HIV ama UKIMWI laa hili ni neno pana. Hapa nitakujuza kwa ufupi kuhusu swali hilo la muulizaji kuwa anawashwa na koo.

Soma Zaidi...
Dalili za ukimwi siku za mwanzo

Makala hii inakwenda kukupa majibu ya maswali mengi kuhusu VVU na UKIMWI. tutakwenda kuona kwa ufupi historian a chanzo cha VVU na UKIMWI. hatuwa za maambukizi ya VVU na ukimwi na dalili zake za kuonekana toka kupata maambukizi. Pia hapa utajifunza namna

Soma Zaidi...
Kiungulia, dawa yake na namna ya kuzuia kiungulia

Tambuwa kiungulia, sababu zake, dawa za kiungulia na namna ya kupambana na kiungulia

Soma Zaidi...
Je vidonda vya tumbo husababisha maumivu mpka upande mmoja wa mgongoni !?

Ni ngumu kujuwa vidonda vya tumbo uhakika wake bila ya kupata vipimo. Unajuwa ni kwa nini, ni kwa sababu maumivu ya tumbo ni dalili ya shida nyingi za kiafya kama ujauzito, mimba, typhod, na shida kwenye unfumo wa chakula.

Soma Zaidi...