picha

Presha ya kushuka (hypotension) dalili zake na njia ya kukabiliana nayo

Presha ya kushuka ama kitaalamu huitwa hypotension, presha ya kushuka ni hatari kwa afya kama ilivyo presha ya kupanda, maana mwili unakosa nguvu kabisa.

Presha ya kushuka (hypotension) dalili zake na njia ya kukabiliana nayo

RPESHA YA KUSHUKA (HYPOTENION)


Presha ya kushuka ama kitaalamu huitwa hypotension, presha ya kushuka ni hatari kwa afya kama ilivyo presha ya kupanda, maana mwili unakosa nguvu kabisa. Kama ilivyo presha ya kushuka presha ya kupanda unaweza kuizuia ana kujilinda nayo kwa kula vyakula salama.



VYAKULA MUJARABU KWA MWENYE PRESHA YA KUSHUKA


1.Tumia chumvi zaidi; wataalamu wa afya wanahimiza sana kutumia chumvi zaidi kwani madini ya sodium yaliyomo kwenye chumvi husaidia katika kupandisha presha. Ila tambua kuwa kwa wazee kuzidi kula chumvu kunaweza kusababisha moyo kujashinwa kufanya kazi vyema.
2.Kunywa maji mengi ya kutosha: maji husaidia katika kuongeza hali ya umajimaji kwenye miili. Hii husaidia kukabilia na upungufu wa maji mwilini (dehydration) hali hizi ni muhimu kwa kukabiliana na presha ya kushuka.
3.Punguza ulaji wa vyakula vya wanga kwa zaidi. Kwa mfano viazi mbatata, mchele na mikate
4.Kunywa chai yenye caffein;



DALILI ZA PRESHA YA KUSHUKA


1.Kushundwa kuona vyema
2.Kuchanganyikiwa
3.Kizunguzungu
4.Kuzimia
5.Uchovu wa hali ya juu.
6.Kuhisi baridi
7.Kushindwa kufikiri kwa kina
8.Kichefuchefu
9.Kushindwa kuhema vyema
10.Kutokwa na jasho




NJIA ZA KUKABILIANA NA MRESHA YA KUSHUKA


1.Fanya mazoezi ya mwili na viungo walau kila siku kwa muda wa dakika 30 mpka 60
2.Kunywa maji mengi na ya kutosha
3.Unapokaa usikae mkao wa kukunja miguu
4.Punguza ulaji wa vyakula vya wanga kama viazi mbatata, mchele na mikate
5.Punguza ama wach kabisa uvutaji wa sigara
6.Punguza ama wacha kabisa unywaji wa pombe.




HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEPATWA NA PRESHA YA KUSHUKA


1.Lala chini kwenye kitu kilicho flati.
2.Kunywa maji mengi
3.Tumia chumvi, unaweza kuilamba unaweza pia kukoroga chumvi kwenye kikombe na kunywa.
4.Kama hali inaendelea kuwa mbaya zaidi ni vyema kuwasiliana na kituo cha afya kilicho karibu nawe.



                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 13378

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Madrasa kiganjani     ๐Ÿ‘‰2 ai web app     ๐Ÿ‘‰3 kitabu cha Simulizi     ๐Ÿ‘‰4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     ๐Ÿ‘‰5 web hosting     ๐Ÿ‘‰6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

AFYA NA MAGONJWA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Dalili za saratani ya koo

Saratani ya Koo inarejelea Vivimbe vya Saratani vinavyotokea kwenye koo lako (koromeo), sanduku la sauti (larynx) au tonsils.

Soma Zaidi...
Maumivu ya kifua: Je, yanaweza kuwa ishara ya ugonjwa wa moyo?

Maumivu ya kifua ni dalili inayopaswa kuchukuliwa kwa uzito mkubwa kila wakati. Ingawa si kila maumivu ya kifua yanamaanisha ugonjwa wa moyoโ€”kwani yanaweza kusababishwa na matatizo ya mmeng'enyo wa chakula, misuli, au mapafuโ€”ni vigumu sana kwa mtu wa kawaida kutofautisha kati ya maumivu ya kawaida na yale yanayoashiria dharura ya moyo. Makala haya yanalenga kukupa elimu kuhusu dalili hatari, sababu nyingine za maumivu, na wakati sahihi wa kutafuta msaada wa kitabibu wa haraka.

Soma Zaidi...
Dalili za maambukizi kwenye figo

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Maambukizi kwenye figo (pyelonephritis) ni aina mahususi ya maambukizi ya njia ya mkojo (UTI) ambayo kwa kawaida huanza kwenye urethra au kibofu chako na kusafiri hadi kwenye figo zako.

Soma Zaidi...
Fahamu Ugonjwa wa mshtuko wa sumu.

Ugonjwa wa Mshtuko wa Sumu ni matatizo ya nadra, yanayotishia maisha ya aina fulani za maambukizi ya bakteria. Mara nyingi ugonjwa wa mshtuko wenye sumu hutokana na sumu zinazozalishwa na bakteria.

Soma Zaidi...