Mifumo ya benki na kazi zake

Mifumo ya benki na kazi zake

Hapa utajifunza kazi za benki.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

7. Mfumo wa benki
Mabenki ni taasisi za fedha ambazo ni muhimu sana katika uchumi. Benki husaidia uchumi kwa kutoa huduma kuu zifuatazo:

 


Kwanza, Benki hutoa huduma ya kuhifadhi akiba za watu na kuhifadhi mali zenye thamani kubwa kama vile dhahabu, na mfano wake.

 


Pili, kutokana na akiba inazozikusanya, benki hujikuta kila wakati ina fedha nyingi zisizo na shughuli yoyote. Benki hukopesha fedha hizi kwa watu wanaozihitajia ili ziwe mtaji wa kuendeleza biashara, viwanda, kilimo na sekta nyingine mbali mbali za uchumi na utoaji huduma.

 


Tatu, benki hutoa huduma ya kurahisisha malipo kwa njia ya hundi (cheque) kuwalipa Wafanyakazi kupitia benki zao au kwa hundi, huwaepusha walipaji na hatari ya ku ib iwa.

 


Nne, pia benki hutoa huduma ya kutoa malipo ya mbali popote pale penye matawi yake nchini au ulimwenguni. Huduma hii ni muhimu sana kwani huwapunguzia watu mzigo wa kusafiri na fedha nyingi mkononi.

 


Badala yake benki huidhinisha malipo kwa simu au kwa njia yoyote ya mawasiliano ya haraka katika tawi la Benki hiyo popote lilipo nchini au ulimwenguni kupitia kwenye Account ya huyo anayestahiki kulipwa.

 


Huduma hizi muhimu na nyinginezo nyingi ambazo hatukuzitaja hapa zinatudhihirishia umuhimu wa kuwepo taasisi hii ya fedha katika jamii. Hivyo ni dhahiri kwamba Uislamu ukiwa ni mfumo kamili wa maisha unaojitegemea kwa kila kitu, hautarajiwi ukapinga au ukaharamisha kuwepo kwa mabenki katika jam ii.Bali Uislamu u n ah aram is ha m ab en ki yanayoendeshwa kwa kipato cha riba.

 

Mabenki ya Riba
Mabenki ya kitwaghuti (yasiyokuwa ya Kiislamu) sehemu kubwa ya kipato chake hutokana na riba.
Mabenki ya Riba hukopesha watu wenye miradi mbali mbali ya uchumi na kuwatoza riba kubwa katika mfumo wa malimbikizo (compound interest). Sehemu ndogo ya riba inayokusanywa na Benki za Riba, hutumiwa katika kuwalipa wateja walioweka akiba zao ambao ndio hasa matajiri walioifanya Benki iwepo.

 


Ni kutokana na unyonyaji wa namna hii utakuta, wakati wakulima na Wafanyakazi wa ngazi za chini ambao ndio wanaovuja jasho ili kuchangia riba, hawajimudu katika kujipatia chakula, mavazi, na makazi bora, wenye mabenki wanagawa “bonus ” kwa wafanya kazi wao na wao wenyewe wanaponda starehe na anasa zilizopindukia kutokana na riba ambayo hawakuitoleo jasho lolote.

 

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1080

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Kwa nini waislamu wanaoa mke zaidi ya mmoja
Kwa nini waislamu wanaoa mke zaidi ya mmoja

Post hiibitakugundisha hekima ya kuruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja katika sheria za kiislamu.

Soma Zaidi...
Ni kwa nini riba imeharamishwa kwenye Uislamu
Ni kwa nini riba imeharamishwa kwenye Uislamu

Hapa utajifinza uharamu wa riba na sababu za kuharamishwa kwake.

Soma Zaidi...
Hadathi ya kati na kati
Hadathi ya kati na kati

Posti hiibinakwenda kukufundisha kuhusu hadathi ya kati na kati.

Soma Zaidi...
msimamo wa uislamu juu ya kupanga uzazi na uzazi wa mpango
msimamo wa uislamu juu ya kupanga uzazi na uzazi wa mpango

Msimamo wa Uislamu juu ya kudhibiti uzaziKama tulivyoona, msukumo wa kampeni ya kudhibiti kizazi, umetokana na mfumo mbaya wa kijamii na kiuchumi ulioundwa na wanadamu kutokana na matashi yao ya ubinafsi.

Soma Zaidi...
Zijuwe funga za sunnah na jinsi ya kuzifunga
Zijuwe funga za sunnah na jinsi ya kuzifunga

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu funga za sunnah na jinsi ya kuzigunga.

Soma Zaidi...
Yajuwe masharti ya udhu yaani yanayofanya udhu kukubalika
Yajuwe masharti ya udhu yaani yanayofanya udhu kukubalika

Posti hii itakufundisha masharti yanayohitajika kwa mwenye kutaka kutia udhu.

Soma Zaidi...
Njia za kujitwaharisha, na vitu vinavyotumika kujitwaharisha
Njia za kujitwaharisha, na vitu vinavyotumika kujitwaharisha

Post hii inakwenda kukufundisha njia zinazotumika kujitwaharisha.

Soma Zaidi...