Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mambo yanayosaidia kuboresha afya
KUBORESHA AFYA
1.TAHADHARI KWENYE VYAKULA
Ukiweza kuchukuwa tahadhari kwenye vyakula na kujua chakula salama cha kukila kulingana na mahitaji ya mwili hapa unaweza kufanikiwa kuulinda mwili wako na maradhi mengi sana. Uwe na elimu sahihi ya vyakula na faida zake kwenye mwili. Kwani unaweza kukusanya vyakula vingi kumbe ni sawa na kual chakula kimoja
Vyakula vya protini ni m uhimu katika ukuaji wa watoto na ukuaji wa tishu. Vyakula hivi huhusika katika kuurekebisha mwili na ni muhimu hsana katika kuhakikisha afya ya mtu ipo kwenye msitari mzuri. Kwa ufupi tunasema kuwa vyakula vya protini ni vyakula vya kujenga mwili. Unaweza kupata protini kwenye maziwa, samaki, nyama, maini, maharage na mayai. Upungufu wowote wa vyakula hivi unaweza kuleta mdahara makubwa kama tulivyoona hapo juu.
Vyakula vya wanga ni mujarabu sana kwa ajili ya kuupa mwili nguvu. Tumia vyakula hivi hasa kama unafanya kazi za nguvu. Vyakula hivi pia ni muhimu kwa ajili ya kuhakikisha kuwa m ifumo ndani ya mwili inafanya kazi kwa usahihi. Kwa mfano mfumo wa upumuaji na uunguzwaji wa chakula (espiration) unahitajia vyakula hivi kwa ajili ya kuzalisha nguvu ya kutosha ndani ya mwili. Vyakula hivi vinaweza kupatikana kwenye nafaka kama mahindi, ngano na mchele.
Vyakula vya madini, Mwili unahitaji vyakula hivi ili uwezesjhe matumizi ya vyakula vingine yawe mazuri tunahitaji viyamini kwa kuulinda mwili dhidi ya magonkwa. Vitamin c hujulikana kwa kusaidia ugonjwa wa scuvy ugonjwa huu humfanya mtu atoke samu mwenue mafinzi. Vitamin A husaidia kurekebisha afya ya macho. Vitamin K husaidia kuganda kwa damu unapopata jeraha. Mwili unahitaji madini pia ili uweze kujikinga na hatari zingine. Madini ya chuma ni muhimu katika kujenga seli nyekundu za damu.madini ya calcium ni muhimu kwa afya ya mifupa na meno. Madini na vitamin hpatikana zaidi kwenye mboga za majani, na matunda. Matunda yenye uchachu kama limao, chungwa husaidia kwa vitamin C na mapapai pi hujulukana kwa kuwa na vitamin C. spinachi ni muhimu kwa vitamin A. samaki husaidia kwa madini mengine.
Vitamin ni muhimu katika kuhakikisha kuwa mwili unatumia virutubisho vingine kufanya kazi zake. Kuna vitamin A,B,C,D,E na K. vitamin B vimegawanyika katika makundi kama vitamin B1,B2,B6, na B12. Ukosefu wa vitamin vyovyote kati ya hivi unaweza ukapelekea matatizo makubwa kwa afya ya mtu. Vitamin A,D,E na K, vinaitwa fat soluble vitamin. Hivi nhuweza kuhifadhiwa ndani ya mwili. Hivyo hatuhitaji kula vyakula kuvipata kwa kila siku. Kwa upande mwengingine vitamin B na C huitwa water soluble vitamin, hivi havihifadhiwi ndani ya mwili, hivyo tunahitaji kula vyakula vyenye vitamin hivi kwa kila siku. Hivyo mtu awe na tahadhari zaidi juu ya kupangilia vyakula vyake. Tuatona zaidi aina hizi na madhara yake kwenye kurasa zijazo.
Unywaji wa maji ni jambo linalolazimishwa sana. Kwama mtu hana sababu yeyote anatakiwa anywe maji mengi zaidi. Wataalamu wa afya wanashauri angalau kwa siku mtu anywe maji bilauri (glass) nane kwa kiwango cha chini. Mwili wa kiumbe hai asilimia 50-90 ni maji. Hivyo maji yakipungua mwilini kunaweza kutokea madhara makubwa zaidi. Maji huhitajika karibia katika mifumo yote mwilini. Maji hutumika katika kurekebisha afya ya mtu.
2.TAHADHARI KWENYE MAZINGIRA
Kama tulivyoona hapo juu, mazingira yetu ni sababu tosha ya kuathiri ubora wa afya zetu. Hivyo mtu ahakikishe sikuzote anaishi katika mazingira salama na safi. Wataalamu wa afya wanatueleza kusafisha mazingira yetu ya ilasiku ili tuweze kukabilia na na wadudu hatara.
Hakikisha hewa unayoipata ni safi na salama. Futa mavumbi ndani ya nyumba na nguo za kujifunika ziwe safi, kwa namna hii ni rahisi kukabilia na na mafua. Epuka moshi kutoka viwandani, pia usilale ukiwa na jiko la mkaa linalowaka na ikawa madirisha na milango umefunga. Unaweza kupata tatizo la kukosa oxkyjeni na kufariki dunia. Kaa mbali na wavuta sigara kwani hewa yao inaweza kukuathiri na wewe pia. Jambo la msingi hapa ni kuchukua tahadhari dhidi ya hewa ambayo tunaipata kwenye mazingira hetu.
Hakikisha unafyeka na kupunguza nyasi zilizo karibu na wewe. Fukia madimbwi na majimaji yoyote yalotuwama hata kama yapo kwenye kifuniko cha soda kwani hayo ni machache lakini mamia ya mbu yanaweza kuzaliana hapo. Mashimo ya kutupia taka yawe mbali kidogo na nyumba na kuwepo utaratibu wa kuchoma moto mashimo hayo bada ya muda. Usafi wa mazingira unaweza kuwa njia tosha ya kuanza harakati za kukabiliana na malaria na kipindupindu.
Watu wahakikishe wanakunywa maji safi na salama pamoja na kula vyakula ambavyo vimehifadhiwa kwa usalama. Usafi wa maji unaweza kuwa njia ya kupambana na typhod (taifodi) na maradhi mengine ya tumbo. Kuwepo na utaratibu wa kuyatibu maji kama yamepatikana sehemu ambazo sio salama na safi. Maji yanaweza kutibiwa kwa njia za kisasa kama kuweka madawa. Lakini pia unaweza kutumia njia ya kuyachemsha na kuyachuja na kuyatumia.
Sikuzote hakikisha unaishi katika mazingira rafiki na afya yako. Watu ambao tayari wanamaambukizi ya maradhi maalumu wanatakiwa waishi katika mazingira ambayo ni rafiki na hali zao.
TAHADHARI KWENYE SHUGHULI ZETU
Kama tulivyotangulia kuona hapo juu kuwa shughuli za kuwapatia watu rizikinazo zinaweza kuwa chanzo cha maradhi. Hivyo tahadhari maalumu zinatakiwa zitumike ili kuweza kujiepusha na madhara ambayo yangeweza kuthibitiwa. Kwa mfano uaweza kujikinga na baadhi ya adhari kwa kuvaa mavazi maalimu kama gkovs, gunboot makoti maalumu kulingana na kazi husika. Soma vizuri nembo za tahadhari unapofungua kifaa cha kufanyia kazi. Tahadhari zaidi zinategemeana na kazi yenyewe na sehemu husika.
TAHADHARI NA TABIA ZETU
Usafi w mwili ni katika tabia njema na ni rafikipia. Kuufanya mwili iwe na uwezo wa kujikinga. Usafi wa nguo ni njia tosha ya kupambana na maambukizo na maradhi mengineyo kama tulivyotoa mfano huko juu. Mtu anatakiwa kujenga tabia rafikia na afya kama kuwa na utaratibu wa kufanya mazoezi angalau mara tatu kwa wiki. Kutokuwa na abia ya kupenda vyakula vyenye chumvi nyingi hii huweza kumuepushha mtu na athari za kupata maradhi ya moyo kama presha na shambulio la moyo. Kupiga mswaki zaidi ya mara moja kwa siku na ukishindwa basi angalamu unapoamka na unapokwenda kulala. Tabia za kiafya zinaweza kujengwa kwenye vyakula, mazoezi, matendo na mazungumzo pia.
TAHADHARI JUU YA MARADHI YA KURITHI
Ni vigumu sana kujitahadhari kutopata maradhi haya kama kuwa albino. Ila inawezekana wazazi kulinda familia zao na maradhi ya kurithi ila pia ni ngumu. Kwani it itajika kupima kati ya wanandoa wawili kabla ya kupata watoto. Hapa ndio itaweza kugundulika maradhi haya ya kurithi kama yapo kwa wazazi na je upo uwezekano wa kuendelea kwa watoto. Kwa teknolojia iliyorahaisi kwa sasa ni kumlinda mtoto atakayezaliwa na maambukizi ya magonjwa ya zinaa. Ijapokuwa yapo matatizo mengine ya kurithi anaweza kukingwa mtoto akiwa tumboni asijedhurika. Tutaona zaidi matatizo haya kwenye kurasa zijazo.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
maumivu ya kichwa ni moja ya dalili za kiafya ambazo huashiria hali isiyo ya kawaida. hata hivyo maumivu ya kichwa yanaweza kutokea hata kama sio mgonjwa. Hapa nitakuletea sababu zinazopelekea kuumwa na kichwa mara kwa mara.Maumivu
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Aina mbalimbali za vidonda kwenye mwili wa binadamu, ni vidonda ambavyo utokea kwenye mwili wa binadamu kwa Aina tofauti.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi imani potofu juu ya ugonjwa wa Ukimwi,ni Imani walizonazo watu wengi kuhusiana na ugonjwa wa Ukimwi.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vyakula vya fati na mafuta
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mbinu ambazo hutumika kuponyesha majeraha kwa haraka zaidi,tunajua majereha utokana na kupona kwa vile vidonda au kupona kwa sehemu ambayo imekuwa na majeraha kwa hiyo ili kuponyesha majeraha hayo tunapaswa kufanya yafuatayo.
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kukabiliana na minyoo
Soma Zaidi...Posti huu inahusu zaidi visababishi mbalimbali vya magonjwa, tunajua wazi kuwa ugonjwa ni hali ya kutokuwa kawaida kwa ogani mbalimbali kwenye mwili na kusababisha mwili kushindwa kufanya kazi zake vizuri.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu namna ya kumfanyia mgonjwa usafi mwili mzima, ni njia ambazo utumika kumfanyia mgonjwa usafi mwili mzima au kumwosha Mgonjwa hasa wale walio mahututi na hawawezi kuamka kitandani.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu ya kuwepo kwa maumivu ya mwili kwa sababu tunaweza kuhisi maumivu kwenye sehemu za mwili kwa sababu mbalimbali kama tutakavyoona hapo chini
Soma Zaidi...Kushambuliwa kwa moyo na kupumua ni kitendo Cha moyo kusimama ghafla, Hali hii unapaswa kutolewa huduma ya kwanza Ili moyo ufanye kazi tena,
Soma Zaidi...