viapo

20.

20.Kujiepusha na Viapo



Waislamu tumekatazwa kuapa apa ovyo ovyo. Kiapo kinakubalika tu pale inapobidi kutolewa mbele ya Kadhi kama ushahidi. Mara nyingi mtu anayeapa apa ovyo ovyo ni muongo. Anaapa ili ahalalishe uwongo. Anahisi kuwa akisema bila kuapa watu hawatamuamini. Kuapa apa ovyo ni tabia ya kinafiki. Tunafahamishwa katika Qur-an kuwa wanafiki wakati wa Mtume (s.a.w) walikuwa wakificha ubaya wao dhidi ya Uislamu na Waislamu kwa kutoa viapo mbele ya Mtume (s.a.w). Lakini Allah (s.w) alimfahamisha Mtume wake kuwa asiamini viapo vyao kwani wao ni waongo.



21.Kujiheshimu na kuwaheshimu wengine


Katika Uislamu kila mtu anayo haki ya kuheshimiwa. Heshima ni haki ya mwanaadamu aliyozaliwa nayo. Miongoni mwa mambo ya msingi aliyousia Mtume (s.a.w) katika khutuba yake ya kuaga aliyoitoa katika uwanja wa Arafa 9 Dhul-Hijjah 10A.H, ni kulinda heshima ya kila mtu. Aliusia:
“Enyi watu hakika damu yenu (yaani uhai wenu), mali zetu na heshima yenu ni vitu vitakatifu kamwe visiharibiwe hadi mtakaposimamishw a mbele ya Mola w enu, kw a utukufu w a vitu hivyo ni kama ulivyo Utukufu wa siku hii, na mwezi huu na mji huu. Kwa hakika mtakutana na Mola wenu na atakuulizeni juu ya vitendo vyema. Je, nimefikisha ujumbe? Ee! Allah shuhudia ”.



Kutokanana usia huu kila Muumini analazimika kuwaheshimu wanaadamu wenzake wakubwa na wadogo. Aseme nao kwa uzuri, asiwadharau, asiwadhalilishe, asiwafedheheshe na asiwavunjie heshima kwa namna yoyote ile. Awatii wazazi, wenye mamlaka juu yake na walio wakubwa kwake katika mambo yote yanayowafikiana na Qur-an na Sunnah, awahurumie na kuwasikiliza walio chini yake au wadogo zake. Kwani Mtume (s.a.w) amesema:
“Si katika sisi yule ambaye hamheshimu mkubwa wetu na kumhurumia mdogo wetu ”.
Kuwaheshimu watu kama ilivyosisitizwa katika Qur-an ni pamoja


Kuzungumza na watu kwa kauli nzuri, kwa upole na huruma. Qur-an inatuamrisha:
“... Na semeni na watu kwa wema...” (2:83).


(ii) Kuwatii wazazi, kuwahurumia na kusema nao kwa vizuri:


~ ~ ~
“... Na sema nao (wazazi) kwa msemo wa heshima (kabisa)”. (17:23).


“Na wanapofika wale wanaoamini aya zetu wambie “Assalaam alaykum” (yaani amani iwe juu yenu)...” (6:54)
(iv)Kurudishia saalam kwa ucheshi baada ya kusalimiwa:


“Na mnapoamkiwa kwa maamkio yoyote yale; basi itikieni kwa yaliyo bora kuliko hayo, au rejesheni hayo hayo. (4:86)
(v)Kuwaheshimu watu wa dini nyingine kwa kutowabughudhi, kutowadharau au kutowadhalilisha kwa namna yoyote ile:


“Wala msiwatukane ambao wanaabudu kinyume cha Allah, was ije wakamtukana Allah kwa jeuri zao bila kujua....” (6:108).


“Waite (watu) katika njia ya Mola wako kw a hekima na mawaidha mema, na ujadiliane nao kwa namna iliyo bora. Hakika Mola wako ndiye anayemjua aliyepotea katika njia yake.. (16:125).
(vi)Kuwakaribisha wageni na kuwapisha kwenye viti au nafasi ya kukaa:



“Enyi mlioamini mnapoambiw a (katika mikutano): “Wafanyieni w asaa wenzenu katika (nafasi za) kukaa”, wafanyieni nafasi. Na Mwenyezi Mungu atakufanyieni nafasi (Duniani na Akhera). Na (hata) ikisemwa, “Simameni”, (ondokeni muw apishe w enzenu), basi ondekeni. Mwenyezi Mungu atawainua wale walioamini miongoni mwenu, waliopewa elimu watapata daraja zaidi. Na Mwenyezi Mungu anazo habari za mnayoyatenda ”. (58:11)



Ili mtu aheshimiwe hana budi kujiheshimu yeye mwenyewe na kuwaheshimu wengine.Mtu asiyejiheshimu hujidharaulisha yeye mwenyewe kwa wanaadamu wenzake. Muheshimiwa zaidi mbele ya Allah ni yule anayemheshimu na kumtii Allah (s.w) na Mtume wake.


“... Hakika aheshimiw aye sana miongoni mwenu mbele ya Allah ni yule amchaye Allah zaidi katika nyinyi. Kwa yakini Allah ni Mjuzi Mwenye habari(za mambo yote).” (49:13)




                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Huduma Main: Afya File: Download PDF Views 236

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Nyanja sita za afya

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu nyanja sita za afya

Soma Zaidi...
HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEUNGUA

Kuungua kupo kwa aina nyingi.

Soma Zaidi...
Makundi manne ya damu na jinsi yanavyotumika

Post hii inahusu zaidi umuhimu wa makundi manne ya damu na jinsi yanavyotumika, Ni magroup manne ya damu ambayo husaidia kuongeza damu kwa mtu ambaye amepungukiwa damu

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa mwenye kizunguzungu

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu mwenye kizunguzungu

Soma Zaidi...
Ratiba ya chanjo ya Pentavalenti

Posti hii inahusu zaidi chanjo ya pentavalent ni aina ya chanjo ambayo inazuia Magonjwa matano ambayo ni kifadulo, pepopunda, homa ya ini na magonjwa yanayohusiana na upumuaji.

Soma Zaidi...
Utaratibu wa lishe kwa watoto

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa watoto

Soma Zaidi...
Zijue kazi za chanjo ya DTP au DPT (Donda Koo,Pepopunda, na kifaduro))

Posti hii inahusu zaidi kazi ya chanjo ya DTP au DPT ambayo Inazuia magonjwa ya Donda Koo, Pepopunda na kifaduro.

Soma Zaidi...
Njia ambazo maradhi huambukizwa

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia ambazo maradhi huambukizwa

Soma Zaidi...
Athari za mkojo mwilini.

Posti hii inahusu zaidi athari za mkojo mwilini, kwa kawaida tunafahamu kwamba mkojo ni matokeo ya mkusanyiko wa uchafu wa maji maji yanayokusanyika kutoka mwilini ikiwa mkojo umebaki mwilini usababisha madhara mbalimbali kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
Maumivu ya kifua yanayosababishwa na kupungua kwa mtiririko wa Damu kwenye moyo.

 Maumivu ya kifua yanayosababishwa na kupungua kwa mtiririko wa damu kwenye misuli ya moyo, kitaalamu huitwa Angina ni dalili ya Ugonjwa wa ateri ya Coronary. Ugonjwa huu kawaida hufafanuliwa kama kufinya, shinikizo, uzito, kubana au maumivu kwenye

Soma Zaidi...