viapo
20.
20.Kujiepusha na Viapo
Waislamu tumekatazwa kuapa apa ovyo ovyo. Kiapo kinakubalika tu pale inapobidi kutolewa mbele ya Kadhi kama ushahidi. Mara nyingi mtu anayeapa apa ovyo ovyo ni muongo. Anaapa ili ahalalishe uwongo. Anahisi kuwa akisema bila kuapa watu hawatamuamini. Kuapa apa ovyo ni tabia ya kinafiki. Tunafahamishwa katika Qur-an kuwa wanafiki wakati wa Mtume (s.a.w) walikuwa wakificha ubaya wao dhidi ya Uislamu na Waislamu kwa kutoa viapo mbele ya Mtume (s.a.w). Lakini Allah (s.w) alimfahamisha Mtume wake kuwa asiamini viapo vyao kwani wao ni waongo.
21.Kujiheshimu na kuwaheshimu wengine
Katika Uislamu kila mtu anayo haki ya kuheshimiwa. Heshima ni haki ya mwanaadamu aliyozaliwa nayo. Miongoni mwa mambo ya msingi aliyousia Mtume (s.a.w) katika khutuba yake ya kuaga aliyoitoa katika uwanja wa Arafa 9 Dhul-Hijjah 10A.H, ni kulinda heshima ya kila mtu. Aliusia:
“Enyi watu hakika damu yenu (yaani uhai wenu), mali zetu na heshima yenu ni vitu vitakatifu kamwe visiharibiwe hadi mtakaposimamishw a mbele ya Mola w enu, kw a utukufu w a vitu hivyo ni kama ulivyo Utukufu wa siku hii, na mwezi huu na mji huu. Kwa hakika mtakutana na Mola wenu na atakuulizeni juu ya vitendo vyema. Je, nimefikisha ujumbe? Ee! Allah shuhudia ”.
Kutokanana usia huu kila Muumini analazimika kuwaheshimu wanaadamu wenzake wakubwa na wadogo. Aseme nao kwa uzuri, asiwadharau, asiwadhalilishe, asiwafedheheshe na asiwavunjie heshima kwa namna yoyote ile. Awatii wazazi, wenye mamlaka juu yake na walio wakubwa kwake katika mambo yote yanayowafikiana na Qur-an na Sunnah, awahurumie na kuwasikiliza walio chini yake au wadogo zake. Kwani Mtume (s.a.w) amesema:
“Si katika sisi yule ambaye hamheshimu mkubwa wetu na kumhurumia mdogo wetu ”.
Kuwaheshimu watu kama ilivyosisitizwa katika Qur-an ni pamoja
Kuzungumza na watu kwa kauli nzuri, kwa upole na huruma. Qur-an inatuamrisha:
“... Na semeni na watu kwa wema...” (2:83).
(ii) Kuwatii wazazi, kuwahurumia na kusema nao kwa vizuri:
~ ~ ~
“... Na sema nao (wazazi) kwa msemo wa heshima (kabisa)”. (17:23).
“Na wanapofika wale wanaoamini aya zetu wambie “Assalaam alaykum” (yaani amani iwe juu yenu)...” (6:54)
(iv)Kurudishia saalam kwa ucheshi baada ya kusalimiwa:
“Na mnapoamkiwa kwa maamkio yoyote yale; basi itikieni kwa yaliyo bora kuliko hayo, au rejesheni hayo hayo. (4:86)
(v)Kuwaheshimu watu wa dini nyingine kwa kutowabughudhi, kutowadharau au kutowadhalilisha kwa namna yoyote ile:
“Wala msiwatukane ambao wanaabudu kinyume cha Allah, was ije wakamtukana Allah kwa jeuri zao bila kujua....” (6:108).
“Waite (watu) katika njia ya Mola wako kw a hekima na mawaidha mema, na ujadiliane nao kwa namna iliyo bora. Hakika Mola wako ndiye anayemjua aliyepotea katika njia yake.. (16:125).
(vi)Kuwakaribisha wageni na kuwapisha kwenye viti au nafasi ya kukaa:
“Enyi mlioamini mnapoambiw a (katika mikutano): “Wafanyieni w asaa wenzenu katika (nafasi za) kukaa”, wafanyieni nafasi. Na Mwenyezi Mungu atakufanyieni nafasi (Duniani na Akhera). Na (hata) ikisemwa, “Simameni”, (ondokeni muw apishe w enzenu), basi ondekeni. Mwenyezi Mungu atawainua wale walioamini miongoni mwenu, waliopewa elimu watapata daraja zaidi. Na Mwenyezi Mungu anazo habari za mnayoyatenda ”. (58:11)
Ili mtu aheshimiwe hana budi kujiheshimu yeye mwenyewe na kuwaheshimu wengine.Mtu asiyejiheshimu hujidharaulisha yeye mwenyewe kwa wanaadamu wenzake. Muheshimiwa zaidi mbele ya Allah ni yule anayemheshimu na kumtii Allah (s.w) na Mtume wake.
“... Hakika aheshimiw aye sana miongoni mwenu mbele ya Allah ni yule amchaye Allah zaidi katika nyinyi. Kwa yakini Allah ni Mjuzi Mwenye habari(za mambo yote).” (49:13)
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 web hosting 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Hatua za kufuata baada ya kuhisi kuwa umeambukizwa na virusi vya HIV
Posti hii inahusu zaidi hatua za kufuata unapohisi umeambukizwa na virus vya ukimwi. Kwa sababu watu wengi wanakuwa na kiwewe anapohisi ameambukizwa na virus vya ukimwi kwa hiyo wanapaswa kufanya yafuatayo.
Soma Zaidi...Haya hayawezi kuambukiza UKIMWI
Somo hili linakwenda kukuletea mambo ambayo hayawezi kuambukiza UKIMWI
Soma Zaidi...Jinsi ya kutoa huduma ya kwanza kulingana na tatizo
Posti hii inahusu sana mambo ya huduma ya kwanza ambayo huduma ya kwanza inapatikana au inatolewa na mtu yeyote katika jamii .
Soma Zaidi...Dalili za shambulio la hofu
Shambulio la hofu ni tukio la ghafla la hofu kali ambayo husababisha athari kali za kimwili wakati hakuna hatari halisi au sababu inayoonekana. Mashambulizi ya hofu yanaweza kuwa ya kutisha sana. Mashambulizi ya hofu yanapotokea, unaweza kufikiri kwamba
Soma Zaidi...HUDUMA YA KWANZA KWA MTU ALIYEZIMIA (CARDIOPULMONARYRESUSCITATION) AU CPR
Kuzimia ni hali ya kupoteza fahamu ambako kunaendana na kutokuhema.
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu vitamini K na kazi zake mwilini
vitamini k ni moja katika vitamini vinavyoitajika sana mwilini. Je unazijuwa athari za upungufu wa vitamini k mwilini?
Soma Zaidi...