Ingawa hakuna ajuaye Kiyama kitakuwa lini, kupitia Aya mbali mbali za Qur’an na Hadith kadhaa za Mtume (s.a.w) zinabainisha kwa uwazi juu ya dalili mbali mbali za kusimama kwa kiyama. Ziko Dalili kubwa na Dalili ndogo, na zipo ambazo tayari zimekwishadhihiri nyingine zinaendelea na ambazo bado kudhihiri kwake; Kama Allah Aliyetukuka anavyotubainishia:
“Kwani wanangoja jingine ila kiyama kiwajie kwa ghafla? Basi alama zake(hicho kiyama) zimekw ishakuja. Kutaw afaa w api kukumbuka wakati kitakapow ajia ? ” (47:18)
Pia anasema“Saa ya Kiyama imekaribia; na mwezi umepasuka” (54 :1)
Dalili Ndogo za Kiyama:
(i)Watu kumiliki mali na hali ya kuwa ni madhalimu wasio na uadilifu
(ii)Kuenea mno kwa riba kiasi cha kila mtu kuathiriwa nayo
(iii)Kuenea kwa kila aina ya Ulevi
(iv)Wanawake kukithiri katika kuvaa nguozinazochochea zinaa (nguo nyepesi za kuangaza , fupi na za kubana)
(v)Wanawake watawaiga wanaume katika mavazi kadhalika wanaume watawaiga wanawake katika mavazi. Leo wanaume wanavaa hereni, shanga, bangili, na mengineyo yanayojulikana kuwa mapambo ya kike.
(vi)Kuenea kwa Liwati (kujimai baina ya jinsia moja-wanaume kuwaendea wanaume wenzao na wanawake kuwaendea wanawake wenzao) Homosexuality and Lesbiansm. Jambo hili leo limehalalishwa na watu wa Magharibi, pia hapa kwetu Afrika na hasa Kenya na Afrika kusini ni halali Mwanaume kuolewa na mwanamume mwenzake! Subhaanallah!
(vii)Kuenea sana kwa zinaa na itafanyika hadharani.
(viii)Watu hawatawajali tena wazazi wao, ndugu zao najamaa zao badala yake watawathamini nakuwasaidia rafiki zao.
(ix)Watu watachukia sana kulea watoto.
(x)Unafiki utaenea sana.
(xi)Mauaji yataenea sana, kwa kutoka Taifa mojakwenda kulivamia Taifa jingine na watu baadhikuwaua wengine kwa maslahi yao binafsi
(xii)Watu wataona uzito sana kutoa sadaka
xiii)Watawala watakuwa wengi sana lakini hakuna atakayekuwa mkweli na mwadilifu
xiv)Mtu ataheshimiwa kwa shari yake na si kwa uadilifu na wema wake.
xv)Kujifaharisha kwa misikiti
xvi)Pamoja na haya yote, bado kutakuwepo na kundi dogo tu la waislamu ambalo litadumu katika njia iliyonyooka na halitatetereka kwa lolote.
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu
Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF
Share On
Facebook
or
Whatsapp
Imesomwa mara 827
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh
👉2 Madrasa kiganjani
👉3 Kitabu cha Afya
👉4 kitabu cha Simulizi
Nguzo za Imani kwa mujibu wa mafunzo ya kiislami.
Makala hii inakwenda kukufundisha kuhusu nguzo sita za imani katika Uislamu. Soma Zaidi...
Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu
Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu Ni upi?
(EDK form 1: mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu) Soma Zaidi...
Mtazamo wa makafiri juu ya dini
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu mtazamo wa uislamu juu ya dini
(EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Njia anazotumia Mwenyezi Mungu (s.w) kuwafundisha na kuwasiliana na wanaadamu
Njia ambazo Allah hutumia kuwasiliana na wanadamu nakuwafundisha elimu mbalimbali. (Edk form 1 dhana ya Elimu) Soma Zaidi...
Neema za Allah(s.w) Juu ya Bani Israil
Katika Qur'an tunakumbushwa neema mbali mbali walizotunukiwa Bani Israil (Mayahudi) na Mola wao ili kuwawezesha kusimamisha Ufalme wa Allah(s. Soma Zaidi...
Uchambuzi wa Neema Alizopewa Nabii Sulaiman(a.s)
(i) Kutiishiwa Upepo Qur'an inatufahamisha kuwa Nabii Sulaiman alitiishiwa upepo akaweza kuutumia apendavyo kwa amri yake. Soma Zaidi...
njia ya maandishi
Soma Zaidi...
Sifa za waumini wa ukweli katika uislamu
Je unamjuwq ni nani muumini, na ni zipi sifa za muumini? Soma Zaidi...
Kumuamini malaika wa mwenyezi Mungu
Nguzo za Imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat at-Tawbah
Mwenyezi Mungu amekuwia radhi (amekusamehe). Soma Zaidi...
Kwa namna gani nabii Musa na Bi Mariam waliweza kuzungumza na Allah nyuma ya pazia
Nabii Musa na Mama yake nabii Isa bi Mariam waliweza kuwasiliana na Allah nyuma ya pazia. Soma Zaidi...
Nafasi ya Elimu katika uislamu
Je ni ipi nafasi ya Elimukatika dini ya uislamu? Soma Zaidi...