Sifa za malaika

Sifa za malaika

Sifa za malaika




Ni viumbe watiifu wasiomuasi Allah(SW)
Malaika ni viumbe watiifu kwa Allah(SW). Wakipewa amri ya kumuadhibu mtu muovu, hawagomi wala kumuonea huruma mtu huyo.Enyi mlioamini! Ziokoeni nafsi zenu na nafsi za watu wenu na moto ambao kuni zake ni watu na mawe. Juu yake kuna Malaika w akali wenye nguvu.Haw amuasi Allah(SW) katika yale anayowaamuru, na wanatekeleza vile walivyoamrishwa.(66:6)


Wana elimu ya kutosha kutekeleza majukumu yao
Malaika wana elimu inayowawezesha kutekeleza majukumu yao bila ya kubabaisha. Elimu waliyopewa malaika ni sehemu ndogo sana katika ujuzi wa Allah(SW). Na wenyewe walikiri mbele ya Allah(SW)Wakasema: Utukufu ni wako! Hatuna elimu ila ile uliyotufundisha, bila shaka wewe ndiye mjuzi na mwenye hekima(2:32)

Malaika hawana jinsia ya kike wala ya kiume. Qur'an inawakosoa watu wanaodhani kuwa malaika ni wanawake. In a h oji:
Na wamewafanya malaika ambao ni waja wa Mwingi wa Rehma kuwa ni wanawake. Je wameshuhudia kuumbwa kwao(43:19).
Ni viumbe wenye mbawa



'Sifa zote njema ni za Allah, Muumba wa mbingu na ardhi. Aliyewafanya malaika kuwa wajumbe wenye mbawa mbili-mbili, na tatu tatu, na nne nne. Huzid is ha katika kuumba apendavyo. Bila shaka Allah ni mwenye uweza juu ya kila kitu'. (35:1)
Huweza kujimithilisha umbile la mwanadamu
Malaika huweza kujimithilisha kuwa kama wanadamu. Hufanya hivyo pale wanapotumwa na Allah(SW)kuleta ujumbe kwa watu maalumu. Kwa mfano, Bibi Maryam, mama yake nabii Isa(a.s), alijiwa na malaika katika umbo mithili ya mwanaume.Na mtaje katika kitabu, Maryam, alipojitenga na watu wake katika upande wa mashariki.


Tukampelekea Muhuisha sharia Yetu(Jibril) akajimithilisha kwake kwa sura ya binaadamu aliye kamilifu. (19:16-1 7)
Lengo la kuumbwa malaika
Lengo la kuumbwa malaika ni kumtumikia Allah(SW). Katika kutekeleza lengo la kuumbwa kwao, malaika hawana hiyari katika kutekeleza amri za Allah(SW), hufanya mambo yote vile anavyotaka Allah(SW).


..Hawamuasi Allah(SW) katika yale anayowaamuru, na w anatekeleza vile w alivyoamrishw a.(66:6)




                   


Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 376

Post zifazofanana:-

Mtume Muhammad hakujuwa kusoma wala kuandika ni hoja na kuna hekima zake
(i)Mtume Muhammad (s. Soma Zaidi...

Ni zipi nguzo za swaumu na masharti ya Swaumu
Soma Zaidi...

Vyakula vya vitamini A na kazi zake
Soma Zaidi...

STANDARD FOUR ENGLISH TEST 007
Soma Zaidi...

tarekh 3
KUCHIMBWA UPYA KISIMA CHA ZAMZAMKwa kifupi ni kuwa Abdul-Muttalib alipata agizo kutoka ndotoni kuwa achimbe kisima cha zamzam, na akaelekezwa sehemu ya kupachimba. Soma Zaidi...

Chemsha bongo namba 09
16. Soma Zaidi...

NAFASI YA SUNNAH KATIKA UISLAMU
Nafasi ya Sunnah katika UislamuMtume Muhammad (s. Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula Nazi
Soma Zaidi...

Vitabu
VITABU: Karibu kwenye Maktaba yetu ya vitabu, hapa utaweza kusoma na kudownload vitabu vyetu bure. Soma Zaidi...

je kutokwa na maji mengi wakati wa tendo la ndoa inaashilia nini?
Je kutokwa na maji ukeni ambayo hayana harufu na meupe Hadi kuroanisha chupi, na je kutokwa na maji mengi wakati wa tendo la ndoa inaashilia nini? Soma Zaidi...

Chanzo cha vita vya Ngamia Vita Kati ya Bibi Aisha na Khalifa Ali
Soma Zaidi...

KUJIANDAA KWA AJILI YA KUMUONA DAKTARI
KUJIANDAA KWA AJILI YA KUMUONA DAKTARI Fanya miadi na daktari wako wa kawaida ikiwa una ishara au dalili zinazokupa wasiwasi. Soma Zaidi...