image

swala ya kuomba mvua na namna ya kuiswali

12.

swala ya kuomba mvua na namna ya kuiswali

12. Swala ya Kuomba Mvua - (Swalatul Istisqaa)’



Istisqaa ina maana ya kuomba maji. Uislamu unatuhimiza kumuelekea Allah kwa msaada wakati wa matatizo na dhiki. Kwa hiyo panapokuwa na ukame Waislamu wanahimizwa kumuomba Allah(s.w)kwa unyenyekevu katika jamaa. Maombi haya yanajulikana kama “Swalatul Istisqaa”. Kutokana na Hadithi mbali mbali maombi haya yanaweza kuombwa katika namna tatu zifuatazo:



(a)Kuomba Dua bila ya swala.
(b)Kuomba dua katika khutuba ya Ijumaa au mwisho wa swala za faradhi.
(c)Namna ya tatu ambayo ni muhimu sana ni ile ya kuswali rakaa mbili zinazofuatiwa na khutuba na kumalizia na Dua.
Maombi haya hapana budi yaombwe kwa unyenyekevu mkubwa ukiambatana na imani kamili juu ya uwezo waAllah usio mipaka.



Swalatul Istisqaa Inavyoswaliwa



Swala hii ni sunnah iliyokokotezwa wakati wa ukame na huswaliwa katika jamaa uwanjani kama inavyo swaliwa swala ya Idd. Kama swala ya Idd katika rakaa ya kwanza kuna takbira saba baada ya Takbira ya kuhirimia na kuna Takbira tano kabla ya kuanza Suratul Fatiha katika rakaa ya pili. Ni sunnah katika rakaa ya kwanza, baada ya Al-fatiha kusoma Surat-Qaf au Al-A’laa na katika rakaa ya pili kusoma baada ya Alfatiha. suratul-Qamar au Al-Ghashiyah. Imamu ni sharti awe kiongozi wa ngazi ya juu au naibu wake anayeshughulikia mambo ya Waislamu.



Swala hii hufuatiwa na khutuba mbili kama ilivyo katika khutuba za Idd. Ni sunnah Imamu kuleta istighf'aari mara tisa kabla hajaanza khutuba ya kwanza na ya pill.


Istighfaari hii ni kusema
"Astaghafirullahil-aladhim alladhii laa ilaaha illa huwal-hayyul-qayyuum-almudabbiru kullu-shayin wa-atubu ilaihi"


Ni sunnah wakati wa kuomba dua kugeuza mikono au kuelekeza mbinguni migongo ya viganja vya mikono . Tunafahamishwa hill katika Hadith za Mtume (s.a.w) zifuatazo kuwa:
Abduilah blrs 7.aid Al-Arrsarl (r.a) amesimuiia kuwa Mtume (s.aw) aWaaenda rye ya rryi Qi Iwswali swaIatu1-IsiisgaaAUpotaka. kuorrtba dua, alielekea Qibia nra alaageura. kiiemba choke. (Muslim).
Arras bin MaWc (r.a) amestmuIia kuu~a Mturne (s.a w) katika kuomba dua ya mvua alielekaezaJuu mtgongo yaviganfa uyake vya miknno. (Muslim).




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 242


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-