picha

Huduma ya Kwanza kwa mtu aloanguka kifafa

Somo hili linakwenda kukueleza jinsi ya kumfanyia huduma ya Kwanza kwa mtu aloanguka kifafa

HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEANGUKA KIFAFA

Kifafa kinaweza kumpata mtu muda wowte. Tafiti zinaonyesha kuwa kati ya watu 10 mmoja anaweza kupata kifafa katika umri wake japo ni mara moja.mara nyingi kifafa ninatokea ndi ya muda mchache. Kikawaida ndani yasekunde kadhaa mpaka dakika 4 na hakizidi dakika 5.

 

Sio lazima kumpeleka mgonjwa hospitali ama kuhitaji msaada wa daktari. Kifafa kinaweza kuondoka chenyewe. Kumbuka hapa hatuzungumzii kifafa cha mimba. Taka msaada wa daktari ama mgonjwa apelekwe hospitali kama:

1.Hajawahi kuwa na kifafa toka azaliwe

2.Anashindwa kuhema ama kutembea baada ya kifafa kuondoka

3.Kifafa kimeendelea kwa muda zaidi ya dakika tano

4.Mtu amepata kifafa kingine punde tu baada ya kurejea hali ya kawaida kutoka kwenye kifafa

5.Mtu ameumia wakati alipopata kifafa

6.Kama kifafa kimetokea akiwa kwenye maji

7.Mtu ana magonjwa ya kisukari, maradhi ya moyo ama ana ujauzito

 

Ili kumsaidia aliyepata kifafa unaweza kumpa huduma ya kwanza kwa kutumia njia kama:-

A.Mlaze mgonjwa chini palipo safi

B.Mlaze mgonjwa upande mmoja

C.Safisha eneo alilopo mgonjwa hakikisha hakuna vitu vyenye ncha kali ama chochote cha kumdhuru

D.Weka kitu kilaini kwenye kicha chake kama mto ama nguo

E.Kama amevaa miwani ivue, vua na tai ana legeza

F.Kama kifafa kitaendelea zaidi ya dakika 5 mpeleke kituo cha afya kilicho karibu.

 

Usifanye haya kwa mtu aliyeanguka kifafa

1.Ukimkamate ama kumzuia miguu na mikono eti asihangaike

2. Usiweke chochote kwenye mdomo wake

3.Usijaribu kumfanyia CPR

4.Usimpe kitu chochote cha kula ama kunywa

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 3445

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 ai web app     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Hatari ya uzito mkubwa

Posti hii inahusu zaidi hatari zilizopo kwa mtu mwenye uzito mkubwa,kwa sababu ya kuwepo kwa uzito mkubwa na pia unene usio wa kawaida usababisha mtu kuwa na matatizo mbalimbali hasa saratani za kila sehemu kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
Makundi manne ya damu na jinsi yanavyotumika

Post hii inahusu zaidi umuhimu wa makundi manne ya damu na jinsi yanavyotumika, Ni magroup manne ya damu ambayo husaidia kuongeza damu kwa mtu ambaye amepungukiwa damu

Soma Zaidi...
Mbinu za kupunguza magonjwa yanayohusiana na figo

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa figo. Ni ugonjwa unaotokana pale figo linaposhindwa kufanya kazi, tuone mbinu za kufanya Ili kuepuka na tatizo hilo.

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyezimia

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyezimia

Soma Zaidi...
fahamu kuhusu vitamini B na faida zake

makala hii inakwenda kukupa faida, kazi na athari za vitamini B mwilini. Nini hutokea endapo utakuwa na upungufu wa vitamini B mwilini?

Soma Zaidi...
Kazi za vitamin B na makundi yake

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu kazi za vitamin B na makundi take

Soma Zaidi...