picha

Huduma ya Kwanza kwa mtu aloanguka kifafa

Somo hili linakwenda kukueleza jinsi ya kumfanyia huduma ya Kwanza kwa mtu aloanguka kifafa

HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEANGUKA KIFAFA

Kifafa kinaweza kumpata mtu muda wowte. Tafiti zinaonyesha kuwa kati ya watu 10 mmoja anaweza kupata kifafa katika umri wake japo ni mara moja.mara nyingi kifafa ninatokea ndi ya muda mchache. Kikawaida ndani yasekunde kadhaa mpaka dakika 4 na hakizidi dakika 5.

 

Sio lazima kumpeleka mgonjwa hospitali ama kuhitaji msaada wa daktari. Kifafa kinaweza kuondoka chenyewe. Kumbuka hapa hatuzungumzii kifafa cha mimba. Taka msaada wa daktari ama mgonjwa apelekwe hospitali kama:

1.Hajawahi kuwa na kifafa toka azaliwe

2.Anashindwa kuhema ama kutembea baada ya kifafa kuondoka

3.Kifafa kimeendelea kwa muda zaidi ya dakika tano

4.Mtu amepata kifafa kingine punde tu baada ya kurejea hali ya kawaida kutoka kwenye kifafa

5.Mtu ameumia wakati alipopata kifafa

6.Kama kifafa kimetokea akiwa kwenye maji

7.Mtu ana magonjwa ya kisukari, maradhi ya moyo ama ana ujauzito

 

Ili kumsaidia aliyepata kifafa unaweza kumpa huduma ya kwanza kwa kutumia njia kama:-

A.Mlaze mgonjwa chini palipo safi

B.Mlaze mgonjwa upande mmoja

C.Safisha eneo alilopo mgonjwa hakikisha hakuna vitu vyenye ncha kali ama chochote cha kumdhuru

D.Weka kitu kilaini kwenye kicha chake kama mto ama nguo

E.Kama amevaa miwani ivue, vua na tai ana legeza

F.Kama kifafa kitaendelea zaidi ya dakika 5 mpeleke kituo cha afya kilicho karibu.

 

Usifanye haya kwa mtu aliyeanguka kifafa

1.Ukimkamate ama kumzuia miguu na mikono eti asihangaike

2. Usiweke chochote kwenye mdomo wake

3.Usijaribu kumfanyia CPR

4.Usimpe kitu chochote cha kula ama kunywa

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 3772

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

Jifunze kuhusu msukumo wa damu kwa kitaalamu huitwa pressure

Kupanda kwa msukumo wa damu ni ktendo ambapo moyo husukuma damu kwa nguvu kuliko kawaida ambapo hupelekea matatizo mengi kwenye mwili

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu fati na mafuta na kazi zake mwilini

Hata kama mtu atakuambbia usile vyakula yenye mafuta bado itahitajika kula tu. Kuna mafuta na fati je unajuwa utofauti wao. Ni zipi kazi zao mwilini? Endelea na makala hii

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa aliyekazwa na misuli

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyekazwa na misuli

Soma Zaidi...
Malengo ya kumsafisha mgonjwa nywele.

Posti hii inahusu zaidi malengo ya kumsafisha mgonjwa nywele zake, ni sababu ambazo upelekea kumsafisha mgonjwa nywele kama tutakavyoona hapo chini.

Soma Zaidi...
Zijue dalili za upungufu wa maji mwilini

Posti hii inaelezea kuhusiana na upungufu wa maji mwilini

Soma Zaidi...
Faida za tumbo katika mwili wa binadamu

Posti hii inahusu zaidi faida za tumbo,tumbo ni sehemu ya mwili ambayo ushughilika na kutunza chakula,

Soma Zaidi...