picha

Huduma ya Kwanza kwa mtu aloanguka kifafa

Somo hili linakwenda kukueleza jinsi ya kumfanyia huduma ya Kwanza kwa mtu aloanguka kifafa

HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEANGUKA KIFAFA

Kifafa kinaweza kumpata mtu muda wowte. Tafiti zinaonyesha kuwa kati ya watu 10 mmoja anaweza kupata kifafa katika umri wake japo ni mara moja.mara nyingi kifafa ninatokea ndi ya muda mchache. Kikawaida ndani yasekunde kadhaa mpaka dakika 4 na hakizidi dakika 5.

 

Sio lazima kumpeleka mgonjwa hospitali ama kuhitaji msaada wa daktari. Kifafa kinaweza kuondoka chenyewe. Kumbuka hapa hatuzungumzii kifafa cha mimba. Taka msaada wa daktari ama mgonjwa apelekwe hospitali kama:

1.Hajawahi kuwa na kifafa toka azaliwe

2.Anashindwa kuhema ama kutembea baada ya kifafa kuondoka

3.Kifafa kimeendelea kwa muda zaidi ya dakika tano

4.Mtu amepata kifafa kingine punde tu baada ya kurejea hali ya kawaida kutoka kwenye kifafa

5.Mtu ameumia wakati alipopata kifafa

6.Kama kifafa kimetokea akiwa kwenye maji

7.Mtu ana magonjwa ya kisukari, maradhi ya moyo ama ana ujauzito

 

Ili kumsaidia aliyepata kifafa unaweza kumpa huduma ya kwanza kwa kutumia njia kama:-

A.Mlaze mgonjwa chini palipo safi

B.Mlaze mgonjwa upande mmoja

C.Safisha eneo alilopo mgonjwa hakikisha hakuna vitu vyenye ncha kali ama chochote cha kumdhuru

D.Weka kitu kilaini kwenye kicha chake kama mto ama nguo

E.Kama amevaa miwani ivue, vua na tai ana legeza

F.Kama kifafa kitaendelea zaidi ya dakika 5 mpeleke kituo cha afya kilicho karibu.

 

Usifanye haya kwa mtu aliyeanguka kifafa

1.Ukimkamate ama kumzuia miguu na mikono eti asihangaike

2. Usiweke chochote kwenye mdomo wake

3.Usijaribu kumfanyia CPR

4.Usimpe kitu chochote cha kula ama kunywa

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 3798

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 ai web app     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Bongolite - Game zone - Play free game     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Ijue rangi ya mkojo isiyo ya kawaida

Post hii inahusu zaidi rangi isiyo ya kawaida kwenye mkojo, kawaida mkojo huwa na rangi ya kahawia Ila ukiona rangi zifuatazo Kuna shida kwenye mkojo.

Soma Zaidi...
Vyakula vya kuongeza nguvu za kiume

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya vyakula vinavyoongeza nguvu za kiume

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa aliyepatwa na presha ya kupanda

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na presha ya kupanda

Soma Zaidi...
Visababishi vya magonjwa.

Posti huu inahusu zaidi visababishi mbalimbali vya magonjwa, tunajua wazi kuwa ugonjwa ni hali ya kutokuwa kawaida kwa ogani mbalimbali kwenye mwili na kusababisha mwili kushindwa kufanya kazi zake vizuri.

Soma Zaidi...
Ajali ya jicho

Post hii inahusu zaidi ajali ya jicho na visababishi vyake, ajali ya jicho ni pale jicho linavyoingiliwa na uchafu na vitu vingine ambavyo havistahili kuwa kwenye jicho

Soma Zaidi...
Huduma ya kwanz akwa aliyeumwa na nyoka

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kumsaidia aliyeumwa na nyoka

Soma Zaidi...