Huduma ya Kwanza kwa mtu aloanguka kifafa
Somo hili linakwenda kukueleza jinsi ya kumfanyia huduma ya Kwanza kwa mtu aloanguka kifafa
HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEANGUKA KIFAFA
Kifafa kinaweza kumpata mtu muda wowte. Tafiti zinaonyesha kuwa kati ya watu 10 mmoja anaweza kupata kifafa katika umri wake japo ni mara moja.mara nyingi kifafa ninatokea ndi ya muda mchache. Kikawaida ndani yasekunde kadhaa mpaka dakika 4 na hakizidi dakika 5.
Sio lazima kumpeleka mgonjwa hospitali ama kuhitaji msaada wa daktari. Kifafa kinaweza kuondoka chenyewe. Kumbuka hapa hatuzungumzii kifafa cha mimba. Taka msaada wa daktari ama mgonjwa apelekwe hospitali kama:
1.Hajawahi kuwa na kifafa toka azaliwe
2.Anashindwa kuhema ama kutembea baada ya kifafa kuondoka
3.Kifafa kimeendelea kwa muda zaidi ya dakika tano
4.Mtu amepata kifafa kingine punde tu baada ya kurejea hali ya kawaida kutoka kwenye kifafa
5.Mtu ameumia wakati alipopata kifafa
6.Kama kifafa kimetokea akiwa kwenye maji
7.Mtu ana magonjwa ya kisukari, maradhi ya moyo ama ana ujauzito
Ili kumsaidia aliyepata kifafa unaweza kumpa huduma ya kwanza kwa kutumia njia kama:-
A.Mlaze mgonjwa chini palipo safi
B.Mlaze mgonjwa upande mmoja
C.Safisha eneo alilopo mgonjwa hakikisha hakuna vitu vyenye ncha kali ama chochote cha kumdhuru
D.Weka kitu kilaini kwenye kicha chake kama mto ama nguo
E.Kama amevaa miwani ivue, vua na tai ana legeza
F.Kama kifafa kitaendelea zaidi ya dakika 5 mpeleke kituo cha afya kilicho karibu.
Usifanye haya kwa mtu aliyeanguka kifafa
1.Ukimkamate ama kumzuia miguu na mikono eti asihangaike
2. Usiweke chochote kwenye mdomo wake
3.Usijaribu kumfanyia CPR
4.Usimpe kitu chochote cha kula ama kunywa
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 ai web app 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Vifaa vya kutumia wakati wa kusafisha vidonda.
Posti hii inahusu zaidi vifaa vya kutumia wakati wa kusafisha vidonda, ni vifaa muhimu ambavyo mara nyingi kutwa hospitalini.
Soma Zaidi...Kazi ya chanjo ya Surua
Posti hii inahusu zaidi kazi ya chanjo ya Surua kwa watoto, ni Aina ya chanjo ambayo utolewa kwa watoto na kufanya kazi mbalimbali mwilini ambazo ni kumkinga mtoto asipatwe na magonjwa.
Soma Zaidi...Vipimo vya kuchunguza kama una asidi nyingi tumboni
Posti hii inahusu zaidi vipimo vya kuchunguza kama una kiwango kikubwa cha asidi au tindikali tumboni
Soma Zaidi...Mzunguko wa mwezi kwa mwanamke
Posti hii inahusu zaidi mzunguko wa mwezi kwa mwanamke, ni mzunguko ambao huchukua siku ishilini na nane kwa kawaida Ila lla ubadilika kulingana na mtu, Ila ngoja tuangalie siku ishilini na nane tu.
Soma Zaidi...Hatari ya uzito mkubwa
Posti hii inahusu zaidi hatari zilizopo kwa mtu mwenye uzito mkubwa,kwa sababu ya kuwepo kwa uzito mkubwa na pia unene usio wa kawaida usababisha mtu kuwa na matatizo mbalimbali hasa saratani za kila sehemu kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...