Somo hili linakwenda kukueleza jinsi ya kumfanyia huduma ya Kwanza kwa mtu aloanguka kifafa
HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEANGUKA KIFAFA
Kifafa kinaweza kumpata mtu muda wowte. Tafiti zinaonyesha kuwa kati ya watu 10 mmoja anaweza kupata kifafa katika umri wake japo ni mara moja.mara nyingi kifafa ninatokea ndi ya muda mchache. Kikawaida ndani yasekunde kadhaa mpaka dakika 4 na hakizidi dakika 5.
Sio lazima kumpeleka mgonjwa hospitali ama kuhitaji msaada wa daktari. Kifafa kinaweza kuondoka chenyewe. Kumbuka hapa hatuzungumzii kifafa cha mimba. Taka msaada wa daktari ama mgonjwa apelekwe hospitali kama:
1.Hajawahi kuwa na kifafa toka azaliwe
2.Anashindwa kuhema ama kutembea baada ya kifafa kuondoka
3.Kifafa kimeendelea kwa muda zaidi ya dakika tano
4.Mtu amepata kifafa kingine punde tu baada ya kurejea hali ya kawaida kutoka kwenye kifafa
5.Mtu ameumia wakati alipopata kifafa
6.Kama kifafa kimetokea akiwa kwenye maji
7.Mtu ana magonjwa ya kisukari, maradhi ya moyo ama ana ujauzito
Ili kumsaidia aliyepata kifafa unaweza kumpa huduma ya kwanza kwa kutumia njia kama:-
A.Mlaze mgonjwa chini palipo safi
B.Mlaze mgonjwa upande mmoja
C.Safisha eneo alilopo mgonjwa hakikisha hakuna vitu vyenye ncha kali ama chochote cha kumdhuru
D.Weka kitu kilaini kwenye kicha chake kama mto ama nguo
E.Kama amevaa miwani ivue, vua na tai ana legeza
F.Kama kifafa kitaendelea zaidi ya dakika 5 mpeleke kituo cha afya kilicho karibu.
Usifanye haya kwa mtu aliyeanguka kifafa
1.Ukimkamate ama kumzuia miguu na mikono eti asihangaike
2. Usiweke chochote kwenye mdomo wake
3.Usijaribu kumfanyia CPR
4.Usimpe kitu chochote cha kula ama kunywa
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Kuzimia ni hali ya kupoteza fahamu ambako kunaendana na kutokuhema.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi jinsi moyo unavyosukuma damu, moyo ni ogani ambayo usukuma damu kwenye sehemu mbalimbali za mwili.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi vifaa vya kutumia wakati wa kusafisha vidonda, ni vifaa muhimu ambavyo mara nyingi kutwa hospitalini.
Soma Zaidi...Kungโatwa na nyuki kunaweza kukahitaji huduma ya kwanza kwa haraka kama mgonjwa ana aleji na nyuki.
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa wajawazito na wanaonyonyesha
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vyakula vya roghage
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa asidi iliyo kwenye tumbo kwa kitaalamu huitwa HCL, ni asidi inayofanya kazi nyingi hasa wakati wa kumengenya chakula.
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa vijana
Soma Zaidi...