Somo Hili linakwenda kukueleza sababu za kwanini mbu hawezi kuambukiza ukimwi
KWA NINI MBU HAWEZI KUAMBUKIZA HIV (UKIMWI)
? Tumekusha kuona na kujua kuwa mbu anaweza kuambukiza maradhi mengi na ya virusi kama zika. Na mradhi mengine kama malaria na homa ya bonde la ufa. Lakini kuna jambo linaumiza sana fikra za wasomaji. “kama mbu wanaweza kuambukiza maradhi hayo ya virusi, sasa ni kwa nini mbu hawezi kuambukiza HIV?”
? Kwa hakika swali hili linasumbua fikra za watu wengi sana. Tafiti nyingi za kisayansi zimefanywa ili kuthibitisha majibu sahihi na kuwaridhisha waulizaji. Ukweli ni kuwa mbu katu hawezi kueneza HIV. Na huu ni ukweli ambao haupingiki katu, lakini sasa ni kivipi?. katika makala hii nitakueleza jibu la swali hili katika namna tatu:-
? Mdomo wa mbu una sehemu kuu 6, katika hizo 6 nne hutumika kutoboa ngozi ya mwili wa kiumbe anachotaka kunyonya damu. Na sehemu 2 zilizobakia ni kwa ajili ya kunyonya damu. Katika sehemu 2 hizo mojawapo ni kunyonya damu na nyingine ni kupeleka mate kutoka kwenye mwili wa mbu na kuelekea kwenye mwili wa kiumbe kinachonyonywa damu. Mate haya hutumika kwa kuifanya damu isigande.
? Hivyo basi kitu ambacho kinatoka kwa mbu kwenda kwa kiumbe kinachonyonywa damu ni mate ya mbu tu, na si damu, kwani damu haiwezi kutoka kutoka kwa mbu kwenda kwa kiumbe kinachonyonywa. Tafiti zinaonesha kuwa mate kati hayawezi kuambukiza ukimwi, hata yawe ya mtu. Hivyo basi hata kama mate ya mbu yataingia kwa mbu kati hayawezi kuambukiza ukimwi kkama amebeba virusi.
? Virusi vya HIV vikifika mwilini mwa mbu vinaliwa na kupotea kabisa. Virusi vya HIV ili viendelee kuzaliana vinahitaji kupata T seli (T cell), lakini mbu hana seli aina hii. Hivyo virusi vinapofika kwa mbu, vinaliwa pamoja na damu na kupotea kabisa. Kwa sababu hii hakuna uwezekano wa virusi vya HIV kuingia kwenye mate ya mbu ambayo ndio huenda kwa kiumbe kinachonyonywa damu. Hii inaonyesha kuwa katu HIV haiwezi kusambazwa kwa mbu.
? hata kama virusi vya HIV vitaweza kuingia kutoka kwa mbu kwenda kwa kiume kinachonyonywa damu (japo jambo hili haliwezekani) hakua uwezekano wa kuambukiza HIV. Tafititi zinaonyesha kuwa ili damu ama mate ya mbu yasambaze HIV inahitajika ang’ate si chini ya mara milioni 10. Jambo hili kisayansi haliwezekani. Pia kummeza mbu aliyebeba HIV HAIWEZEKANI KUSAMBAZA HIV. Haka akipasukia kwenye jeraha la mtu katu damu yake haiwezi kuambukiza HIV.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi ratiba ya chanjo ya kuzuia Nimonia, hii ni chanjo inayozuia hasa hasa Magonjwa ya mfumo wa hewa kwa hiyo nayo upewa watoto wenye umri chini ya miaka mitano.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi umuhimu wa makundi manne ya damu na jinsi yanavyotumika, Ni magroup manne ya damu ambayo husaidia kuongeza damu kwa mtu ambaye amepungukiwa damu
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Aina kuu tatu za mvunjiko ni Aina za kuvunjika ambazo uwakumba watu mbalimbali na watu ushindwa kutambua hizi Aina tatu za mvunjiko, zifuatazo ni Aina za mvunjiko.
Soma Zaidi...Kupanda kwa msukumo wa damu ni ktendo ambapo moyo husukuma damu kwa nguvu kuliko kawaida ambapo hupelekea matatizo mengi kwenye mwili
Soma Zaidi...Kungโatwa na nyuki kunaweza kukahitaji huduma ya kwanza kwa haraka kama mgonjwa ana aleji na nyuki.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu kazi ya chanjo ya kifua kikuu kwa kitaalamu huitwa BCG. Ni chanjo ambayo uzuia kifua kikuu na ukoma.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi aina mbalimbali ya maumivu ya mwili, Maumivu ya mwili utokea kwa aina mbalimbali kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na shambulio la moyo
Soma Zaidi...Ajali ya kichwa na ajali inayotolewa kwenye sehemu mbalimbali za kichwa, ambavyo husababishwa madhara kwa aliyepata ajali hiyo
Soma Zaidi...