Kuungua kupo kwa aina nyingi.
Kuungua kupo kwa aina nyingi. Mtu anaweza kuungua kwa umeme, moto wa kuni, moto wa gesi ama mvuke unaotoka kwenye mashine kama bomba la pikipiki. Pia mtu anaweza kuungua kutokana na miripuko kama baruti. Pia mtu anaweza kuunguwa kwa kemikali. Namna zote hizi zina utoaji huduma wake. Hapa nitaelezea kwa ufupi kuungua kwa moto.
Mtu anapoungua na moto angalia kwanza ni kwa kiasi gani ameungua. Kama ameungua sana ama eneo kubwa ni vyema kuwahi kutoa taarifa kituo cha afya kilicho karibu, ama kumuwahisha mgonjwa. Pia kuwa makini sana kama ameungua usoni, kwenye makalio ama miguu ama mikono au sehemu za siri.
Kama ameungua kawaida unaweza kumpatia huduma ya kwanza kisha uaendelea kumuangalia mgonjwa kama itahitajika kumpeleka kituo cha afya. Mtu aliyeungua unaweza kumpatia huduma ya kwanza kwa njia zifuatazo:
1.mwagilizia maji kwa muendelezo kwenye jeraha kwa muda wa dakika 15. ikishindikana kufanya hivi
2.Pepea sehemu yenye jeraha, ila usitumie barafu kwani linaweza kusababisha athari zaidi.
3.Unaweza kumpa mgonjwa dawa za maumivu kupunguza maumivu
4.Safisha jeraha kwa kimiminika cha iodine, ama aloevera gel. Na katu usimpake mafuta ya aina yeyote.
5.Unaweza kumpaka asali kwenye jeraha
6.ili kulinda jeraha dhidi ya kuvamiwa na bakteria mpake mmgonjwa kimiminika cha antibiotic
7.Lizibe jeraha kwa kulifunga na bendeji ama kitambaa kilicho safi na hakikisha hukazi sana wakati wa kufunga.
8.Angalia hali ya mgonjwa kisha umpeleke kituo cha afya kilicho karibu kwa uangalizi zaidi
Umeionaje Makala hii.. ?
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kujilinda dhidi ya mapunye
Soma Zaidi...Post hii inahusu namna ya kutoa huduma ya kwanza kwa mtu aliyeungua moto, kuingia moto ni kitendo Cha kubabuka ngozi ya juu inaweza kuwa kwa kemikali,umeme na just,
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuangalia kwa mtu aliyepoteza fahamu, kama mtu amepoteza fahamu Kuna mambo muhimu yanapaswa kuangaliwa kwa makini kama ifuayavyo.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi namna mimba inavyotungwa mpaka mtoto kuingia kwenye mfuko wa uzazi, mimba kutungwa ni kitendo ambapo mbegu za kiume kuungana na yai la kike na kutengeneza zygote.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa vidonda, kwa sababu tunaona vidonda vinashambulia sehemu mbalimbali za mwili ila tunakuwa hatuna sababu kwa hiyo zifuatazo ni sababu za kuwepo kwa vidonda.
Soma Zaidi...Posti huu inahusu zaidi visababishi mbalimbali vya magonjwa, tunajua wazi kuwa ugonjwa ni hali ya kutokuwa kawaida kwa ogani mbalimbali kwenye mwili na kusababisha mwili kushindwa kufanya kazi zake vizuri.
Soma Zaidi...Hii posti inahusu zaidi sifa za mkojo usio wa kawaida,ukiona mkojo wa namna hii unapaswa kwenda hospitalini kwa matibabu au vipimo vya zaidi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi vipimo vya kuchunguza kama una kiwango kikubwa cha asidi au tindikali tumboni
Soma Zaidi...Katika post hii utajifunza sababu zinazowezabkuorlekea kibofu kuuma upande mmoja
Soma Zaidi...