picha

HUDUMA YA KWANZA KWA MTU ALIYEZIMIA (CARDIOPULMONARYRESUSCITATION) AU CPR

Kuzimia ni hali ya kupoteza fahamu ambako kunaendana na kutokuhema.

HUDUMA YA KWANZA KWA MTU ALIYEZIMIA (CARDIOPULMONARYRESUSCITATION) AU CPR

HUDUMA YA KWANZA KWA MTU ALIYEZIMIA (CARDIOPULMONARYRESUSCITATION) AU CPR


Kuzimia ni hali ya kupoteza fahamu ambako kunaendana na kutokuhema. Ukikutana na mtu huyu usimkimbie. Kwanza msogelee karibu kisha hakikisha kama yupo hai ama laa. Kama yupo hai, kwanza angalia kama utaweza kupiga simu kituo cha afya, ama mtaalamu wa afya. Hakikisha maamuzi haya na utekelezwaji unafanyika haraka bila ya kuathiri hali ya mgojwa.



Baada ya kujiridhisha na maamuzi uliyochukuwa unaweza kuanza huduma ya kwanza, ya kumsaidia mgonjwa asiyepumua aweze kupumua. Hapa tutafanya huduma ya kwanza itambulikayo kama CPR. Hii ni huduma ya kwanza inayohitaji umkini wa hali ya juu. Lakini kwa ambaye hafahamu chochote kuna namna anavyotakiwa kufanya



1.mlaze mgonjwa kichalichali juu ya sehemu iliyo ngumu, isiwe sehemu inayobonyea kama kitandani


2.Punguza nguo zilizopo kifuani kwake, na kama ni mwanaume unaweza kumvua shati kabisa.


3.Bidua kidogo kichwa cake


4.Weke mkono wako wa mmoja juu ya mwengine, kisha iweka katikati ya chuchu za mgonjwa.


5.Anza kumbonyeza kifua chake kwa wastani wa mibonyezo 100 paka 120 kwa dakika moja. Yaani karibia mibonyezo miwili kwa sekunde.


6.Hakikisha unabonyeza kwa nguvu mpaka uone kifua cha mgonjwa kinapanda na kuchuka kutokana na mibonyezo yako.


7.Usizidishe nguvu kupitiliza ukavunja mifupa ya mgonjwa.


8.Enelea kufanya hivi mpaka utakapoona mgonjwa anweza kupumua.


9.Muwahishe mgonjwa kituo cha afya baada ya kuanza kupumua.



                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 8872

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 ai web app     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEKUNYWA SUMU

Maisha ya mtu yanaweza kuwa hatarini ama kupotea mara moja baada ya kunywa sumu.

Soma Zaidi...
Sababu za michubuko kwa watoto wanaozaliwa

Post hii inahusu zaidi sababu za michubuko kwa watoto wanaozaliwa,ni sababu ambazo uweza kuchangia kuwepo kwa michubuko kwa watoto wanaozaliwa.

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa aliyepatwa na presha ya kupanda

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na presha ya kupanda

Soma Zaidi...
Mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa wagonjwa walio na majeraha ya macho.

Posti hii inaelezea kuhusiana na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa walio na majeraha ya macho kutokana na aina mbalimbali ya jeraha

Soma Zaidi...
Zijue faida za maji ya uvuguvugu.

Posti hii inahusu zaidi faida za maji ya uvuguvugu, hasa hasa maji haya ni vizuri kabisa kuyatumia hasa wakati wa asubuhi na pia wakati tumbo likiwa halina kitu, kwa hiyo zifuatazo ni faida za maji ya uvuguvugu.

Soma Zaidi...
Utaratibu wa lishe kwa wagonjwa

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa wagonjwa

Soma Zaidi...