Hstora ya Nabii Ilyasa
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu historia ya Nabii Ilyasa
HISTORIA YA MTUME ILYASA(A.S)
Mtume Ilyasa ni mmoja wa Mitume waliotumwa kupitia kizazi cha Bani Israil. Alitumwa kwa watu ambao walitupa mafundisho ya Mitume waliotangulia na badala yake wakawa wanaabudu Mungu- jua waliyemuita - Baal. Mtume Ilyasa(a.s) aliwaita watu wake wamwabudu Mungu Mmoja, Allah(s.w); lakini walimkadhibisha. Kwa ajili hiyo ya kukataa mafundisho ya Mtume wao, wakawa katika kundi la watakaoingia katika adhabu ya Allah(s.w). Isipokuwa kwa wale waliorejea kwa Mola wao wakajitakasa. Kwa muhtasari ujumbe wa Mtume Ilyasa(a.s) unapatikana katika aya zifuatazo:
"Na hakika Ilyas alikuwa miongoni mwa Mitume. (Wakumbushe) Alipowaambia watu wake: "Oh! Hamuogopi?" "Mnamuomba (na kumuabudu) Baal na mnamuacha aliye Mbora wa waumbaji (na ndiye Muumbaji peke yake)." "Mwenyezi Mungu, Mola wenu na Mola wa wazee wenu wa mwanzo!" Wakamkadhibisha. Basi bila shaka watarudishwa (adhabuni). Isipokuwa waja wa
Mwenyezi Mungu waliosafishwa (na Mwenyezi Mungu). Na tumemuachia (sifa nzuri) kwa (watu wote) Amani kwa Ilyas" (37:123-130).
Katika historia
Alyasa katika Uislamu
Alyasa (Kiarabu: اليسع, Alyasaʿ) ni nabii wa Mungu aliyepelekwa kuwaongoza Wana wa Israeli. Katika Quran, Alyasa anatajwa mara mbili kama nabii mwenye heshima na mara zote akiwa pamoja na manabii wenzake. Anaheshimiwa kama mrithi wa kinabii wa Ilyas (Elia).
Kutajwa katika Quran
Jina la Alyasa limetajwa mara mbili katika Al-An'am 6:86 na Sad 38:48. Aya hizo zinamtaja kuwa "amepewa neema" na "miongoni mwa wateule":
"Na Ismail na Alyasa na Yunus, na Lut; na kila mmoja tulimneemesha juu ya walimwengu." — Al-An'am 6:86
"Na kumbuka watumishi wetu Ismail, Alyasa, na Dhul-Kifl, kila mmoja wao ni wema wa kweli." — Sad 38:48
Makaburi Yanayodaiwa
Baadhi ya Waislamu wanaamini kaburi la Alyasa lipo Al-Awjam, Saudi Arabia, lakini liliondolewa na Serikali ya Saudi kwa sababu heshima hiyo haikubaliani na vuguvugu la Wahhabi. Kaburi lingine linadaiwa kuwa lipo katika wilaya ya Eğil, Mkoa wa Diyarbakir, Uturuki. Kituo hicho kilihamishwa usiku kabla ya eneo hilo kufurika mwaka 1994 na mwili wa nabii huyo ulihamishiwa kwenye kilima kinachoangalia tambarare iliyojaa maji.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 web hosting 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Hstora ya Nab Sulaman
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu historia ya Nabii Sulaman
Soma Zaidi...Historia ya Nabii Shu'aib
atika makala hii utakwenda kujifunza kuhusu historia ya Nabii Shu'aib katika Quran
Soma Zaidi...Hstora ya Nab Ishaqa katika quran
Katika post hii tutakwenda kujifunza historia ya Mtume Ishaqa
Soma Zaidi...hHistoria ya Nabii Dhul-kifl
Katika makala hii tutakwenda kujifunza kuhusu historia ya Nabii Dhul-kifl
Soma Zaidi...Hstora ya Nabii Yahya
Katika somo hili uatkwenda kujifunza kuhusu historia ya Nabii Yahya
Soma Zaidi...Historia ya Nabii Musa
atika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu historia ya Nabii Musa
Soma Zaidi...