Historia ya Mwanadamu

Historia ya Mwanadamu

Historia ya Mwanadamu



Historia ya mwanadamu ukiichunguza tangu mwanzo wake utakuta matukio mengi yanayothibitisha kuwepo Allah (s.w) Mmiliki wa kila kitu na mwenye nguvu na uwezo juu ya kila kitu. Mara kwa mara tunatanabahishwa katika Qur-an:“Je! Haikuwabainikia tu kama (kaumu) ngapi tuliziangamiza kabla yao? Na hawa (makafiri wa sasa) wanatembeatembea katika maskani yao, (hawaoni alama za kuangamizwa kwao)? Bila shaka katika hayo zimo ishara kwa wenye akili. ” (20:128 “Je! Haw atembei katika nchi na kuona jinsi ulivyokuw a mwisho wa wale waliokuwa kabla yao? Walikuwa wenye nguvu zaidi kuliko wao na wakilima ardhi na kuistawisha zaidi kuliko wao walivyostawisha. Na mitume wao waliwajia kwa dalili waziwazi, basi hakuwa Mwenyezi Mungu ni mwenye kuwadhulumu, lakini walikuwa wenyewe wakijidhulumu nafsi zao.” (30:9)“Je! Huoni Mola wako alivyo wafanya watu wenye ndovu? Hakujaalia vitimbi vyao kuharibika? Na akawapeleka ndege makundi kwa makundi, wakawapiga kwa mawe ya udongo wa kuchoma, Akaw afanya kam a majani yaliyotafunw a. ” (1 05:1-5)


Tukio hili la watu wenye ndovu lilitokea mwaka 570. A.D. miezi michache kabla ya kuzaliwa Mtume Muhammad (s.a.w).


Mnamo mwaka wa 570 A.D. Abraha, gavana wa Yemen, chini ya himaya ya Kikiristo ya Uhabeshi alikusanya jeshi lenye askari 60,000 na ndovu (tembo) kumi na tatu (13) kwa nia ya kuibomoa na kuisambaratisha Al-Ka’abah, nyumba takatifu ya Allah (s.w) iliyopo Makka.


Walinzi wa Ka’abah, kabila la Quraish waliongozwa na Abdul-Muttalib, Babu yake Mtume (s.a.w), walimfahamisha Abraha kuwa wao hawana uwezo wa kupambana na jeshi lake hilo bali mwenye Ka’abah ndiye atakayeilinda. Abraha alipokaidi na kusisitiza kutekeleza azma yake ya kuivunja Ka’abah, Abdul-Muttalib aliwaamuru wakazi wa Makka wampishe na akaingia ndani ya Ka’abah na kumuomba Allah (s.w) kwa unyenyekevu kama ifuatavyo:“O Allah, mtu hulinda nyumba yake, nawe ilinde nyumba yako.


Usiuachie msalaba na hila zao kesho kushinda hila zako. Kama utaamua kuwaachia waifanye watakavyo Qibla yetu, Basi w ewe ni muweza wa kufanya upendavyo. Wanusuru leo watumishi wako dhidi ya watumishi wa Msalaba na waabudu wake.


Ewe Mola wangu, sina matumaini yoyote toka kwa yeyote dhidi yao isipokuwa kwako. Ewe Mola wangu, ilinde nyumba yako dhidi yao. Adui wa nyumba hii ni adui yako. Wazuie w asiiharibu nyumba yako”.
Kesho yake, Abraha na jeshi lake kabla hawajapiga hatua kutoka kwenye kambi yao, kilometa tano (5) tokea Makka, walizingirwa na jeshi la ndege wadogo wadogo walioitwa “Ababil” waliokuwa na silaha ya vijiwe. Kila ndege alimlenga askari wake na kijiwe hicho kilichomchakaza na kumfanya kama majani yaliyotafunwa na kutemwa.



Tukio hili la “watu wa ndovu” ni kielelezo tosha kutokana na historia ya binaadamu kuwa Allah (s.w) yupo na anauwezo ulio juu ya hila zote za binaadamu na juu ya kila kitu.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1308

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Kwa namna gani Allah huwasiliana na wanadamu kwa kupitia ndoto.

Ndoto za kweli ni moja kati ya njia ambazo Allah huwasiliana na wanadamu.

Soma Zaidi...
Mtazamo wa kikafiri juu ya maana ya dini.

Maana ya dini kwa mujibu wa makafiri ina utofauti mkubwa na vile ambavyo uislamu unaamini kuhusu dini.

Soma Zaidi...
Kwa nini Elimu imepewa nafasi ya kwanza katika Uislamu?

Kwa nini katika uislamu elimu imepewa nafasi ya kwanza ( EDK form 1 Dahana ya elimu)

Soma Zaidi...
Sifa za waumini zilizotajwa katika surat ash-Shuura

“Basi vyote hivi mlivyopewa ni starehe ya maisha ya dunia tu, lakini kilicho kwa Mwenyezi Mungu ni bora na cha kudumu (milele).

Soma Zaidi...
Kuangamizwa Waovu na Kuokolewa Waumini

Baada ya kuonywa wasionyeke, Allah(s.

Soma Zaidi...
Nafasi ya Elimu katika uislamu

Je ni ipi nafasi ya Elimukatika dini ya uislamu?

Soma Zaidi...
Kujiepusha na maringo na majivuno

Maringo, majivuno, majigambo, dharau ni vipengele vya kibri.

Soma Zaidi...
Mambo ya lazima kufanyiwa maiti ya muislamu

Mambo ya faradhi kuhusu maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...