Baada ya Quraish kufeli mbinu zao za mateso, sasa wanaanza mbinu za diplomasi, wanajaribu kumshawishi Mtume kwa kumpa mali nauongozi
Mazungumzo ya Utbah bin Rabi'a na Mtume Muhammad (SAW)
Baada ya kusilimu kwa mashujaa wawili wenye nguvu, Hamzah bin Abdul-Muttalib na Umar bin Al-Khattab, mateso dhidi ya Waislamu yalianza kupungua. Watu wa Makkah walitambua kuwa kuendelea kuwatesa hakutawafanya Waislamu waache imani yao. Kwa hiyo, wakaanza kubuni njia mpya ya kushawishi. Wakuu wa Makkah walimshauri Utbah bin Rabi'a kumwendea Mtume Muhammad (SAW) na kumshawishi kwa ahadi za mali, cheo, na hata ufalme, mradi tu aache kuhubiri Uislamu.
Utbah alikutana na Mtume (SAW) na kusema: “Hakuna mwingine aliyewaletea watu wa Arabia msiba mkubwa kama wewe. Umeikashifu dini yetu, miungu yetu, na mababu zetu. Kama unataka mali, tutakupa utajiri mkubwa kuliko mtu yeyote wa Quraish; kama unataka kuwa kiongozi, tutakufanya mkuu wetu; na kama unahitaji matibabu, tutakuletea waganga wazuri."
Mtume Muhammad (SAW) alijibu kwa utulivu kwa kumsomea Utbah maneno ya Qur’an kutoka Surah Fussilat (41:1-5), akianza na:
"Kwa Jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu. Hâ-Mîm. Ufunuo kutoka kwa Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu. Kitabu ambacho aya zake zimeelezwa kwa kina…"
Mtume (SAW) alisoma sura hiyo huku Utbah akisikiliza kwa makini, mpaka alipofika kwenye aya inayohitaji kusujudu, Mtume akasujudu. Kisha akamwambia Utbah: “Ewe Abu Al-Waleed, umesikia jibu langu, sasa unaweza kufanya utakavyo.” Utbah alirudi kwa viongozi wenzake wa Makkah na kuwaambia: "Sijawahi kusikia maneno kama hayo; hayana mashiko ya ushairi, uchawi, au uaguzi. Naomba msimwonee, mwacheni afanye atakavyo."
Hata hivyo, viongozi wa Quraish hawakushawishika. Walimcheka Utbah na kusema kuwa Mtume (SAW) alikuwa amemroga.
Katika simulizi nyingine, Utbah aliendelea kusikiliza maneno ya Mtume (SAW) hadi alipofika aya isemayo:
"Lakini kama wakigeuka, waambie: ‘Nimewaonya kuhusu Sa’iqa (kilio kikubwa, adhabu kali, radi) kama ile iliyoipata kaumu ya ‘Ad na Thamûd." [41:13]
Utbah, akiwa na hofu kubwa, alisimama na kumwomba Mtume (SAW) aache ili watu wa Quraish wasije wakaangukiwa na adhabu hiyo. Alirudi haraka kwa watu wake na kuwaambia yale aliyoyasikia, lakini walikataa kumsikiliza.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Wana wa Abd Manaf wanaungana kumlinda Mtume Muhammad isipokuwa Abu Lahab yeye amekataa kuungana na ndugu zake.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kazi ambazo alikuwa akifanya Mtume Muhammad ﷺ kabla ya kupewa utume
Soma Zaidi...Baada ya Maquraish kufeli mpango wao wa kuwarejesha Wahamiaji, wakaamuwa wafanye mbinu nyingine kwa ajili ya kuzuia harakati za Mtume Muhammad
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu historia ya Amina mama wa Mtume Muhammad ﷺ
Soma Zaidi...Baada ya kukatika kwa Wahyi kwa muda wa masiku kadhaa hatimaye Jibril akaleta tena wahyi kwa mara nyingine.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu amri ya kulingania wtu wote, yale yaliyojiri katika mkutano wa kwanza na laana ya Abu Lhab. TUkio hili lilianyika katika mlima As-safa
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu historia ya mkataba wa al-Fudhul na matokeo yake katika kusimamaia haki za wafanyabiashara.
Soma Zaidi...Katikasomo hili utakwenda kujifunza stori maarufu ya Bahira kuhusu kukutana na Mtume Muhammad ﷺ na kumtambuwa utume wake.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu historia ya safari ya sira na miraji na yanayopatikana katika safari hiyo
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuusu malezi na makuzi ya Mtume Muhammad ﷺ akiwa kwa bibi Halima
Soma Zaidi...