Historia ya Imamu Bukhary Muandishi wa Hadithi za Mtume s.sa. w

Historia ya Imamu Bukhary Muandishi wa Hadithi za Mtume s.sa. w

Hii ni historia ya Imamu Bukhary pamoja na kitabu chake cha sahihul Bukhari.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Kwa majina anaitwa Muhammad bin Isma'il Abu 'Abdallah al'Ju'fi anayejulikana kwa jina la "Imamu al-Bukhari." Alizaliwa 13 Shawwal, 194 A.H./21 Julai, 810 A.D. katika mji wa Bukhara huko Urusi, na alifariki 30 Ramadhan, 256 A.H./31 Agosti 870 .D. Hamu yake ya kuhifadhi Hadith aliipata bado akiwa mtoto wa umri wa miaka kumi na moja. 

Alipofikia umri wa miaka kumi na sita alikwenda kuhiji Makka na kubakia humo humo kujifunza Hadith kwa wanazuoni mbali mbali. Baada ya kutoka Makka alikwenda Misr kisha Basra na sehemu nyingine za Asia ambapo alitembea huku na huku katika kujifunza na kukusanya Hadith kwa muda wa miaka kumi na sita.

Kazi yake ya miaka kumi na sita inaonekana katika kitabu chake mashuhuri kijulikanacho kwa jina la "Al-Jami'u al-Sahihi au Sahihi al-Bukhari".Kitabu hiki ndio kitabu cha kwanza cha Hadith kinachotemgemewa na Umma wa Waislamu baada ya Qur-an, kwa sababu ya uangalifu mkubwa uliochukuliwa na Imamu Bukhari katika ukusanyaji na uchambuaji wa Hadith zake. 

Jumla ya Hadith alizokusanya ni 600,000 na katika hizo alihifadhi Hadith 200,000. Lakini kutokana na uangalifu na tahadhari kubwa aliyoichukua katika kuhakiki usahihi wa Hadith alizozipokea, ni Hadith 7,275 tu zilizotokea katika kitabu cha sahihi al-Bukhari. Kabla hajaikubali Hadith kuwa ni sahihi, ilibidi kwanza achunguze historia ya maisha ya kila mpokeaji wa Hadith hiyo kutokea kwa Mtume (s.a.w) mpaka kumfikia.

Imamu Bukhari amezipanga Hadith katika kitabu chake kufuatana na mada za fiq-h. Ameigawanya kazi yake katika juzuu tisini na saba na katika milango (sura) 3,450.

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 1667

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

DUA ZENYE MANENO HAYA HUJIBIWA
DUA ZENYE MANENO HAYA HUJIBIWA

SIFA ZA (MANENO NA MATAMSHI YA) DUA YENYE KUJIBIWA.

Soma Zaidi...
Al-Arbauwn An-Nawawiyyah hadithi ya 6: ubainifu wa halali na haramu
Al-Arbauwn An-Nawawiyyah hadithi ya 6: ubainifu wa halali na haramu

Post hii inakwenda kukupa tahadhari juu ya mambo ya halali na mambo ya haramu.

Soma Zaidi...
Sura za kujikinga na Uchawi na mashetani
Sura za kujikinga na Uchawi na mashetani

Post hii itakwenda kukufundisha sura katika Quran ambazo ni kinga dhidi ya Wachawi, uchawi na Masheitwani.

Soma Zaidi...
Ni  zipi hadithi sahihi na hadithi Quds
Ni zipi hadithi sahihi na hadithi Quds

Hapa tutajifunza maana ya hadithi sahihi na hadithi Quds na tofaiti zao.

Soma Zaidi...
UHAKIKI WA HADITHI
UHAKIKI WA HADITHI

Uhakiki wa Hadith za Mtume (s.

Soma Zaidi...
Hadithi ya pili: sifa za muumini wa kweli
Hadithi ya pili: sifa za muumini wa kweli

Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Faida za swala ya Mtume
Faida za swala ya Mtume

Hapa utajifunza fadhila za kumswalia Mtume (s.a.w)

Soma Zaidi...
Dua za kuwaombea wazazi
Dua za kuwaombea wazazi

Kwenye Quran kuna duaambazo Allah ametufundisha tuziombe kwa ajili ya wazazi, familia na kwa ajili yetu wenyewe.

Soma Zaidi...