picha

Historia ya Imamu Bukhary Muandishi wa Hadithi za Mtume s.sa. w

Hii ni historia ya Imamu Bukhary pamoja na kitabu chake cha sahihul Bukhari.

Kwa majina anaitwa Muhammad bin Isma'il Abu 'Abdallah al'Ju'fi anayejulikana kwa jina la "Imamu al-Bukhari." Alizaliwa 13 Shawwal, 194 A.H./21 Julai, 810 A.D. katika mji wa Bukhara huko Urusi, na alifariki 30 Ramadhan, 256 A.H./31 Agosti 870 .D. Hamu yake ya kuhifadhi Hadith aliipata bado akiwa mtoto wa umri wa miaka kumi na moja. 

Alipofikia umri wa miaka kumi na sita alikwenda kuhiji Makka na kubakia humo humo kujifunza Hadith kwa wanazuoni mbali mbali. Baada ya kutoka Makka alikwenda Misr kisha Basra na sehemu nyingine za Asia ambapo alitembea huku na huku katika kujifunza na kukusanya Hadith kwa muda wa miaka kumi na sita.

Kazi yake ya miaka kumi na sita inaonekana katika kitabu chake mashuhuri kijulikanacho kwa jina la "Al-Jami'u al-Sahihi au Sahihi al-Bukhari".Kitabu hiki ndio kitabu cha kwanza cha Hadith kinachotemgemewa na Umma wa Waislamu baada ya Qur-an, kwa sababu ya uangalifu mkubwa uliochukuliwa na Imamu Bukhari katika ukusanyaji na uchambuaji wa Hadith zake. 

Jumla ya Hadith alizokusanya ni 600,000 na katika hizo alihifadhi Hadith 200,000. Lakini kutokana na uangalifu na tahadhari kubwa aliyoichukua katika kuhakiki usahihi wa Hadith alizozipokea, ni Hadith 7,275 tu zilizotokea katika kitabu cha sahihi al-Bukhari. Kabla hajaikubali Hadith kuwa ni sahihi, ilibidi kwanza achunguze historia ya maisha ya kila mpokeaji wa Hadith hiyo kutokea kwa Mtume (s.a.w) mpaka kumfikia.

Imamu Bukhari amezipanga Hadith katika kitabu chake kufuatana na mada za fiq-h. Ameigawanya kazi yake katika juzuu tisini na saba na katika milango (sura) 3,450.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sunnah Main: Post File: Download PDF Views 2663

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰2 web hosting     πŸ‘‰3 ai web app     πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰5 Bongolite - Game zone - Play free game     πŸ‘‰6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Al-Arbauwn An-Nawawiyyah hadithi ya 3: Nguzo za uislamu

Katika hadithi hii utakwenda kujifunza nguzo za uislamu

Soma Zaidi...
Faida za Kusoma Surat Al-Mulk

Surat Al-Mulk (Sura ya 67 katika Qur’an) inajulikana kama sura yenye baraka nyingi na kinga kubwa kwa msomaji wake. Katika makala hii, tunaangazia siri za kiroho, faida za kusoma sura hii kila usiku, na jinsi inavyomkinga Muislamu na adhabu za kaburi. Pamoja na hayo, tutaangazia mafunzo ya kimaadili yanayopatikana ndani ya sura hii yenye aya 30.

Soma Zaidi...
Dars 2: Salamu inaleta mapenzi.

Katika darsa hii tutakwenda kujifunza maneno ya Mtume kuhusu salamu kama chanzo cha kuleta upendo baina ya watu.

Soma Zaidi...