Historia ya Imamu Bukhary Muandishi wa Hadithi za Mtume s.sa. w

Hii ni historia ya Imamu Bukhary pamoja na kitabu chake cha sahihul Bukhari.

Kwa majina anaitwa Muhammad bin Isma'il Abu 'Abdallah al'Ju'fi anayejulikana kwa jina la "Imamu al-Bukhari." Alizaliwa 13 Shawwal, 194 A.H./21 Julai, 810 A.D. katika mji wa Bukhara huko Urusi, na alifariki 30 Ramadhan, 256 A.H./31 Agosti 870 .D. Hamu yake ya kuhifadhi Hadith aliipata bado akiwa mtoto wa umri wa miaka kumi na moja. 

Alipofikia umri wa miaka kumi na sita alikwenda kuhiji Makka na kubakia humo humo kujifunza Hadith kwa wanazuoni mbali mbali. Baada ya kutoka Makka alikwenda Misr kisha Basra na sehemu nyingine za Asia ambapo alitembea huku na huku katika kujifunza na kukusanya Hadith kwa muda wa miaka kumi na sita.

Kazi yake ya miaka kumi na sita inaonekana katika kitabu chake mashuhuri kijulikanacho kwa jina la "Al-Jami'u al-Sahihi au Sahihi al-Bukhari".Kitabu hiki ndio kitabu cha kwanza cha Hadith kinachotemgemewa na Umma wa Waislamu baada ya Qur-an, kwa sababu ya uangalifu mkubwa uliochukuliwa na Imamu Bukhari katika ukusanyaji na uchambuaji wa Hadith zake. 

Jumla ya Hadith alizokusanya ni 600,000 na katika hizo alihifadhi Hadith 200,000. Lakini kutokana na uangalifu na tahadhari kubwa aliyoichukua katika kuhakiki usahihi wa Hadith alizozipokea, ni Hadith 7,275 tu zilizotokea katika kitabu cha sahihi al-Bukhari. Kabla hajaikubali Hadith kuwa ni sahihi, ilibidi kwanza achunguze historia ya maisha ya kila mpokeaji wa Hadith hiyo kutokea kwa Mtume (s.a.w) mpaka kumfikia.

Imamu Bukhari amezipanga Hadith katika kitabu chake kufuatana na mada za fiq-h. Ameigawanya kazi yake katika juzuu tisini na saba na katika milango (sura) 3,450.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 1446

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU

BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU.

Soma Zaidi...
Al-Arbauwn An-Nawawiyyah hadithi ya 6: ubainifu wa halali na haramu

Post hii inakwenda kukupa tahadhari juu ya mambo ya halali na mambo ya haramu.

Soma Zaidi...
Uandishi wa Hadithi wakati wa Matabiina

Historia ya uandishi wa hadithibwakati wa Matabiina, yaani wafuasi wa maswahaba

Soma Zaidi...
BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU

BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU.

Soma Zaidi...
Fadhila za udhu yaani faida za udhu

Katika makala hii utajifunza faida za kuwa na udhu

Soma Zaidi...
Hali ambazo akiwa nazo mwenye kuomba dua dua yake hujibiwa

Post hii inakwenda kukifundisha nibhali zipi ukiwa nazo, basi dua yako kuhubaliwa kwa urahisi.

Soma Zaidi...
UHAKIKI WA HADITHI

Uhakiki wa Hadith za Mtume (s.

Soma Zaidi...