HADITHI YA. 28 NAKUUSIENI KUMCHA ALLAAH NA TABIA NJEMA

HADITHI YA. 28 NAKUUSIENI KUMCHA ALLAAH NA TABIA NJEMA

Hadithi Ya 28: Nakuusieni Kumcha Allaah Na Tabia Njema

الحديث الثامن والعشرون

"أوصيكم بتقوى الله وحسن الخلق"

عن أبي نَجيحٍ الْعِرْباضِ بنِ سارِيَةَ رضي اللهِ عنه قال: وَعَظَنَا رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم مَوْعِظَةً وَجِلَتْ مِنها الْقُلُوبُ، وذَرَفَتْ منها الْعُيُونُ، فَقُلْنا: يا رسول اللهِ، كأَنَّهَا مَوْعِظَةُ مُوَدِّعٍ، فأَوْصِنا. قال:

((أُوصِيكُمْ بِتَقْوَى اللهِ عَزَّ وَجَلَّ، والسَّمْعِ والطَّاعَةِ، وإن تَأَمَّرَ عَلَيْكُمْ عَبْدٌ، فإنَّهُ مَنْ يَعِشْ مِنْكُمْ فَسَيَرَى اخْتِلافاً كَثِيراً، فَعَليْكُمْ بِسُنَّتي وسُنَّةِ الخُلفَاءِ الرَّاشِدِينَ المَهْدِيِّينَ، عَضُّوا عَلَيْها بالنَّواجِذِ، وإيَّاكُمْ ومُحْدَثاتِ الأُمُورِ، فإنَّ كلَّ مُحْدَثَةٍ  بِدْعَةٌ وَ كُلَّ  بِدْعَةٍ ضَلاَلَةٌ  وَكُلَّ ضَلاَلَةٍ فِي النَّارِ))  

رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ وَقَالَ: حَدِيثٌ حَسَنٌ صَحِيحٌ. 

 


HADITHI YA. 28 NAKUUSIENI KUMCHA ALLAAH NA TABIA NJEMA

Kutoka kwa Abu Najiih Al 'Irbaadh Ibn Saariyah رضي الله عنه  ambaye alisema kwamba:

Mtume صلى الله عليه وسلم  alituhutubia  hutuba ambayo nyoyo zetu zilijaa hofu na macho yetu yalitutoka machozi.  Tukasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyeezi Mungu!, inaonyesha kama kwamba hii ni hutuba  ya kuaga, kwa hivyo tuusie.  Akasema (Mtume صلى الله عليه وسلم  )  nakuusieni kumcha Allaah سبحانه وتعالى  na kumtii kiongozi wenu hata akiwa mtumwa.  Yule atakayeishi (muda mrefu) ataona ikhtilaaf nyingi (migongano), kwa hivyo fuateni mwendo wangu (Sunnah) na mwendo wa Makhalifa walioongoka (Makhalifa wanne). Shikamaneni nazo kwa magego (kwa nguvu).  Na tahadharini na mambo mapya yanayozuliwa kwani kila jambo jipya ni uzushi, na kila uzushi ni upotofu, na  kila upotofu unapeleka motoni.

 

Imesimuliwa na Abu Dawuud na At Tirmidhi na wamesema ni Hadithi Hasan na Sahihi.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 1259

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Namna ambazo Allah hujibu dua ya mwenye kuomba.

Post hii inakwenda kukufundisha namna ama staili ambazo Allah hujibu dua za watu.

Soma Zaidi...
DUA 113 - 126

DUA ZA WAKATI WA SHIDA Dua ya wakati wa taabu “LAA ILAAHA ILLA-LLAHUL-’ADHIMUL-HALIIMU.

Soma Zaidi...
dua ya kuomba jambo ufanikiwe

hii ni damna ya kuomba dua ukubaliwe, dua ya kuomba jambo ufanikiwe

Soma Zaidi...
Mzazi na msafiri na mwenye kudhulumiwa dua zao hujibiwa kwa haraka

Wapo watu kadhaa ambao waliomba dua hazirudi. Hapa nitakueleza wawili ambao ni mzazi na msafiri.

Soma Zaidi...
DUA ZA WAKATI WA HASIRA

DUA ZA WAKATI UNAPOKUWA NA HASIRA.

Soma Zaidi...