Simulizi za Hadithi EP 5 Part 16: Hadithi ya safari ya saba ya Sinbad

Muendelezo wa safari ya Sinbad.......

SAFARI YA SABA YA SINBAD

 

Walipokusanyika siku ilofata Sinbad akawaambia kuwa kilichofanya nikavunja ahadi yangu ya kutosafiri tena ni kauli ya Sultani Nilipopunzika kwa muda wa miezi miwili nilipata habari kuwa Sultani ananiita. Nilipokwenda alinieleza kuwa anataka nipeleke barua yake kwa mfalme wa Serendib ya kumjibu kuwa ameridhika na urafiki. Nikamueleza kuwa nimeweka ahadi ya kutousafiri tena kutokana na yalonikuta. Sultani alisisitiza sana mimikwenda na akaniambia kuwa mimi ndie mtu nafaa zaidi kwani mfalme wa Serendib ananijua.

 

Basi nilikubaliana na amri ya Sultani na ikaandaliwa safari ya kifalme na jahazi lililo madhubuti zaidi na la kisasa liliandaliwa na Sultani mwenyewe. Baada ya maandalizi kukamilika mali nyingi kama zawadi ziliandaliwa kwa ajili ya mfalme. Safari ilianza salama na tuliwasili Serendib kwa amani muda wa jioni. Mfalme wa Serendib alinipokea mwenyewe na kunikumbatia na kunivika joho lenye ukosi ulochovywa kwenye dhahabu nyekundu.

 

Mfalme alilidhika na zawadi zile na alifurahi sana kwa kuniona. Mfalme alifurahi zaidi kuona barua ile imejibiwa kama atakavyo. Mafalme wa Serendib akaniozesha mtoto wake kama takrima ya udugu wetu. Ndoa ilifanyika salama na baada ya kukaa pale kwa muda wa mwezi mmoja nilipewa ruhusa ya kuondoka mimi na mkewangu na zawadi nyingi kwa ajili yangu na kwa ajili ya Sultani wa Baghadad.

 

Mfalme mwenyewe aliandaa jahazi na kulimadhiubutisha na safari iliandaliwa kifalme kwani ndani mlikuwa na mkwe na mtoto wa mfalme. Tuliwasili Baghadadi baada ya mwe ndo wa siku kumi na tano. Na Sultani alitupokea kwa heshima zote na kukutana na binti wa Mfalme wa Serendib. Sultani alitufanyia sherehekubwa kama ile ilofanyika wakati wa harusi kule Sererndib. Kwa hakika ilikuwa ni furaha kubwa zaidi. Na huu ndio mwisho wa safari zangu saba za majini.

 

Mpaka sasa nina wake watatu mmoja nilishamuoa nilipokuwa kijana na mwingine ni yule nilookoka nae kwenye makaburi na wa tati ni huyu. Na nimebahatika kuoa mabinti wawili wa wafalme. Kisha Sinbad akawaomba wakezake wote waje ili Sinbad wa nchikavu awaone, kisha akamkutaninisha na yule mzee wa bostani alokuja nae Sinbad. Kisha Sinbad wa baharini akamuuliza Sinbad wa nchikavu “je! Unafikiri sistahiki kupata maisha haya kwa sasa?, je! Kuna yeyote unayemfahamu amepata taabu kama mimi?” majibu ya maswali haya alibakia nayo Sinbad moyoni kwa mshangao.

 

Baada ya pale Sinbad wa majini akamwambia Sinbad mbeba mizigo kuwa sasa tumeshakkuwa marafiki. Kwa siku saba hizi umekuwa kama ni ndugu yangu sasa. Naomba uje na familia yako tukae hapa kama ndugu. Sindab mbeba mizigo akakubaliana na ombi lile na waliishi na Sinbad kwa muda mrefu sana. Waliishi kama kaka na ndogoake. Hata alipofariki Ndugu wa Sinbad wakamchagua kijana Sinbad mbeba mizigo awe ndiye msimamizi mkuu wa mali za mzee Sinbad. Kwa hakika maisha yao yalikuwa mazuri sana na mahusiano yao na ya Sultani wa Baghadad na mfalme wa Serendib hayakukoma.

 

Mpaka kufikia hapa Schehrazade akamaliza hadithi hii ya Sinbad, na tayari miezi mingi ilishapita bila ya kuuliwa na Sultani Shahariyar. Baada ya hapa Sultani Shahariyar akauliza “hatujajua kilichomkuta mtoto wa Sinbad aliyemzaa kutoka kwa ‘Aisha mtoto wa mfalme” Dinarzade akamwambia “ni hadithi ya kusisimua sana” na kama utaniongeza muda zaidi wa kuishi nitakusimulia hadithi nzuri zaidi ya yalomkuta mtoto wa Sinbad.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Mankaa image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Burudani File: Download PDF Views 188

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 11: Vidole gumba vilikatwa

Kitabu cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA kina simulizi nyingi nzuri na za kusisimua, muendelezo....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 3 Part 6: Simulizi ya samaki wa rangi nne

Simulizi za HALIF LELA U LELA zipo nyingi na zinasisimua.. kisa hiki cha samaku wa rangi nne kipo katika kitabu cha kwanza

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 3 Part 3: Kisa cha mke na kasuku

Simulizi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza simulizii hii inasimulia kisa cha mke na Kahuku wake....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Mtumwa wa mfalme na mawaziri

Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha tatu.....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 2 Part 3: Hadithi ya mzee wa pili na mbwa wawili weusi.

Simulizi za HALIF LELA U LELA ni nziri sana tuwe pamoja kusikiliza kisa cha mzee wa pili na mbwa wawili weusi...

Soma Zaidi...