Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza.......
KUELEKEA BONDE LA UOKOZI
Alinibeba akapaa angani sana hata sikuona ardhi. Alikwenda kwa muda wa dakika 30-50 na akatua kwenye bonde lenye milima. Alipotua nikajifungua na kwawoga alishituka na kuniacha pale. Nikaondoka kwa haraka na kujificha asijeniona. Muda haukupita roc alikamata nyoka mkubwa sana na kumkata vipande. Alimla na kuondoka na kipande. Alipoondoka na mimi nikatoka mafichoni pale na kuanza kuchunguza eneo lile na kujua vipi nitatoka pale.
Nilipochunguza zaidi eneo lile nikagungua ni bonde lililopochini sana na limezungukwa na milima mirefu yenye mawe. Ni bonde ambalo katu mtu asingeweza kutoka. Mchana mzima nilikuwa nikitafuta pa kutokea lakini bila mafanikio. Japo nilikuwa najishauri kuwa bora hapa kuliko kule kisiwani. Usiku ulipoingia nilijificha kwenye mapango na kulala. Usingizi haukuja kabisa kwa woga. Kwani uksiku nyoka walokuwa wakiogopa mchana kuliwa na roc walikuwa wakitoka kutafuta chakula.
Muda wote nilikuwa nikimuomba Mungu dua aniokoe na wadudu wabaya usiku ule. Mwenyezi Mungu alinilinda na ulipofika asubuhi nikaendelea na uchunguzi wangu wa eneo lile. Kwa ghafla nilishituliwa na kishindo nyuma yangu. Nilipogeuka nikakuta ni kipande kikubwa cha nyama. Nyama. Hapa nikakumbuka hadithi ya zamani sana juu ya bonde la wawinda madini. Wazee wetu walikuwa wakitusimulia kuwa kuna watu wanawinda madini kwa kutumia nyama. Yaani wanatupa nyama kwenye bonde lenye madini, kisha nyama ile inaganda vipande vya madini na pindi ndege wanapokuja kuchukua nyama ile ambayo ina madini yaloganda kutoka bondeni huwakimbiza ndege wale na wanapoidondosha wanachukua madini.
Pale nikawa nawaza huende hii ikawa ndio njia pekee ya mimi kutoka pale. Nikawa naangalia kama nitaona mtu lakini sikuweza kuona kwani juu ni mbali sana. Basi nikaamza kuokota madini mapande makubwa makubwa. Eneo lile lilikuwa na madini mengi na makubwa yalokuwa waziwazi. Niliokota almasi na dhahabu kwa wingi pamoja na madini mengine. Nilipomaliza nikayafunga kwa uzuri sana na kuanza kutengeneza mpango wa kutoroka pale nilipofungwa.
Kwakuwa mapande ya nyama yalokuwa yakitupwa yalikuwa ni makiubwa sana, nikachagua lile kubwa zaisi na kujifunga nali na kujificha kwenye kanzu yangu. Baada ya muda ndege mkubwa sana alikuja ndege aina ya eagle. Ndege yule ana watoto hivyo alichagua pande kubawa na kuondoka nalo. Pande hili ndo lile ambalo nipo. Alinipeleka mpaka kwenye kitundu chake. Na haukupita muda watu wengi wakatokea na kuanza kumtisha ndege yule na kunidondosha mimi na nyama ile.
Kumbe wale wawinda madini kila mmoja alikuwa na kitundu chake, hivyp walishangaa baada ya nyama anatoka na mtu. Niliwasimulia yote yalonopata. Walinipa pole lakini kwa kuwa nilikuwa na madini mengi sana yule mwenye kitundu chake nilimwambia achukue kiasi anachotaka na akachukua pande moja tu. Kisha akaniachia mengie, nikawagawia na wenzie. Tulikaa eneo lile kwa muda wa wiki tukiwinda madini na baada ya hapo tukaanza kurudi baghadadi, kwa kuwa na wale walikuwa wakiishi bafhdad ila hatukuwa tukijuana kwa kuwa ni wa mji mwingine.
Njiani tulipita misitu mikubwa na yakutisha, tulipishana na manyoka wakubwa sana hata tukafika ufukweni na nikauza baadhi ya madini yangu kwenye kisiwa cha Balrora. Nikanunua pale bidhaa kadhaa na zawadi za kupeleka nyambani. Siku tatu baadae tulipanda jahazi la kuelekea baghadad na tulipofika kwanza nikaanza kutoa sadaka na zaka mali zangu na nikawasimulia ndugu zangu yote yaloniptata. Walinipongeza sanana na kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunirudisha salama. Nilikusanya watu na kufanya dua na kutoa sadaka zaidi kama ni shukrani yangu kwa msaada alonipa mwenyezi Mungu hata akanirudisha salama. Niliamua sasa kutofanya biashara nyingine za baharini na kuanza biashara ndogo ndogo. Nilifanya hivi kwa muda wa miezi sita, huku nikawa nafatilia habari za wasafiri. Muda wote huo sikusikia ajali yeyote na walikuwa wakinisifia faida walokuwa wakizipata. Nilivutiwa zaidi na nikasahau machungu yote yalonipata. Nikaamua kuanza safari ingine ya tatau.
Baada ya kumaliza hadithi hii Sinbad wa baharini akampatia Sinbad mbeba mizigo kiasi cha pesa kama ni fidia ya kupoteza muda wake wa kazi na kusikiliza hadithi yake. Kisha akamuahidi kesho awahi ili ajepata yalomkuta safari ya tatu. Akawaambia watu wote walokuwa pale kuwa kesho wawahi maana safari hii amekutwa na mengi ya kustaajabu. Basi watu wote wakatawanyika pale na Sinbad wa baharini akaingia ndani kwake.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Mankaa Tarehe 2024-09-10 09:31:42 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Masomo File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 116
Sponsored links
👉1
kitabu cha Simulizi
👉2
Kitabu cha Afya
👉3
Simulizi za Hadithi Audio
👉4
Kitau cha Fiqh
👉5
Madrasa kiganjani
👉6
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Simulizi za Hadithi EP 10 Part 7: Taharuki
Muendelezo..... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 7 Part 15: Aladini na kitabu
Muendelezo.... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 19: Kinyozi
Hii ni simulizi iliyopo ndani ya kitabi cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA..... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 19: Mfalme na waziri wake
Hadithi hii inapatikana katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA..... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 14: Hadithi ya kifo cha kujionea
Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza Muendelezo wa safari ya Sinbad Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 6: Sehemu ya tatu ya safari ya Sinbad
Muendelezo wa sehemu ya tatu ya safari ya Sinbad iliyopo kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA.... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 17: Ufupisho wa ALIFU LELA U LELA KITABU CHA KWANZA
Huu ni ufupisho mfupi kuhusiana na kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 16: Usaliti
Hadithi za HALIF LELA U LELA zipo nyingi sana na zinavutia na zinasomwa na kusikilizwa kwa wakubwa na wadogo na hii simulizi inatoka kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA...... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 7: Sehemu ya nne ya safari ya Sinbad
Muendelezo wa hadithi ya safari ya safari ya Sinbad iliyopo kwenye hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza..... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 7 Part 16: Kitabu cha ajabu
Muendelezo..... Soma Zaidi...