Muendelezo wa simulizi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili....
HADITHI ILIYOSIMULIWA NA MLEVI
Tambua ewe Sultani muadilifu wa Baghdad mwa na wa Rashidi utambulikae kwa Harun, tambua kuwa mimi ni mzaliwa wa Misri na huku nimefika tu kwa sababu za utafutaji wa riziki. Baba yangu alikuwa ni mfanyabishara mzkubwa sana huko misri. Alijulikana sana katika miji na hata viji na nchi za majirani ya misri. Nilikuwa nikishiriki biashara na baba yangu toka nilipokuwa mdogo.
Hatimaye Mwenyezi Mungu akamchukuwa baba yangu na hapo mimi nikarithi kazi ya baba. Katika familia nipo peke yangu na mama yangu alishafariki zamani sana nikiwa mdogo. Nilifanyabiashara misri. Biashara yangu kuu ilikuwa ni kuuza kanzu. Nilikuwa nikizipaka manukato mazuri hata zikawa zikinukia sana na kumvutia mpita njia.
Watu walipenda sana biashara yangu na jina langu lilikuwa hata kumzidi baba yangu. Ila katu sikuweza kusafiri kibiashara kama alivyokuwa akifanya baba yangu. Niliweza kutengeneza chaneli za kibiashara wakawa wafanyabiashara wadogowadogo wanachukuwa mzugo kutoka kwangu. Kwa hakika biashara ya kanzu ilikuwa ikinilipa vyema. Kipindi chote hiki sikuwa mwenye kuoa.
Ilitokea siku moja akaja mtu mmoja na kuulizia bei ya kanzu. Badala ya kumtajia akanipatia kiasi kikubwa cha fedha na kunieleza nimpelekee mzigo wake sehemu ambayo alinitajia. Haikuwa ni kazi nzito kwani ni katika majukumu ya kazi yangu. Nilipomaliza maandalizi nikampelekea mzigo wake. Alipouona akanieleza kuwa nimuuzie mzigo ule pale kwake na faida yeyote nitakayoipata tutagawana.
Kwa uchu wangu wa pesa nikakubali. Yule bwana akaniaga safari ila akanieleza nimtunzie pesa yake mpaka atakapo rejea. Mambo yakawa hivyo nilimaliza kuuza mzigo na nilipata faida kubwa sana. Yule bwana baada ya mwezi akaja na kuniulizia pesa yake. Nikamueleza kuwa ipo salama. Basi akanieleza nimtunzie hadi atakaporudi tena.
Baada ya mwezi akarejea, na kuniambia kuwa ana shughuli nyingi, baada ya kumaliza atakuja kuchuuwa pesa yake. Alipoondoka akakaa kiasi cha mwezi. Hata aliporudi alikuwa mapendeza sana. Alifaa nguo nadhifu na za kupendeza.. alipokuja akanieleza ataondoka tena ila akirudi atachukuwa pesa yake. Mimi nikajiapiza kuwa pindi akija nitamkirimu kama mgeni wa heshma.
Safari hii alikaa kama mwaka hivi na aliporudi akaulizia pesa yake nikamueleza kuwa ipo salama. Basi nikamuomba awe mgeni wangu kwa siku ile na akakubali kwa sharti kuwa matumizi nitakayotumia yasiwe katika ile pesa yake. Nikakubali, baada ya muda kikaletwa chakula safi sana. Nikamnawisha kisha akanawa mgono wa kushoto. Nilistaajabu sana. Apilpoanza kula akala kwa mkono wa kushoto.
Nilistaajabu sana kwa mtu mtanashati na msafi kama huyu alafua anakula kwa shoto. Tulipomaliza kula akanywa maji kw ashoto. Basi baada ya chakula tukaanza kuzimulia za hapa na pale. Ndipo nikamuulza anitoe mashaka kuhusu kula kwake kwa shoto. Huenda ana ugonjwa ama ameumia ama anafanya masifa. Ndipo akatoa mkono wake. Looo! Mkoni wake ni kugupu aani ni kiwete ana mkono lakini kiganja kimekatwa.
Baada ya hapo akanieleza kuwa si kama ametaka kula na kushoto ila kuna sababu ilopelekea hali hiyo. Basi kwa udadisi niauiza kuhusu chanzo bila kusita ndipo akaanza kuzimulia hadithi yake na kukatwa kwa mkono wae:-
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Mankaa Tarehe 2024-09-10 10:53:38 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Masomo File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 162
Sponsored links
👉1
Kitabu cha Afya
👉2
Simulizi za Hadithi Audio
👉3
kitabu cha Simulizi
👉4
Madrasa kiganjani
👉5
Kitau cha Fiqh
👉6
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 20: Kinyozi maishani mwangu
Muendelezo..... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 17: Ufupisho wa ALIFU LELA U LELA KITABU CHA KWANZA
Huu ni ufupisho mfupi kuhusiana na kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 1 Part 2: Simulizi ya kisa cha mfugaji na mkewe
Simulizii hii ni inatoka katika kitabu cha kwanza cha HALIF LELA U LELA Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 18: Hadithi ya fundi cherehani
Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili..... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part24 : Kaka wa tatu wa kinyozi
Muendelezo Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 2 Part 2: Hadithi ya mzee wa kwanza na mbuzi wake
Simulizi za HALIF LELA U LELA zipo nyingi sana na husikiliwa na kusomwa na wakubwa kwa wadogo pia hadithi hizi zimeenea duniani Kate zikisikilizwa na maelfu ya watu mbalimbali. Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 3 Part 4: Kisa cha waziri aliyeadhibiwa
Simulizii hii inapatikana katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 7 Part 10: Jumba la Aladini
Muendelezo..... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 7: Sehemu ya nne ya safari ya Sinbad
Muendelezo wa hadithi ya safari ya safari ya Sinbad iliyopo kwenye hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza..... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 20: Waliodhulumiwa kufanyiwa suluhisho
Ni mojawapo ya simulizi iliyopo kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA.... Soma Zaidi...