image

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 7: Hadithi ya safari ya majibu juu ya maswali mawili

Wapendwa wasomaji na wasikilizaji wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza karibu tuendelee kusikiliza hadithi zetu mzuri na za kusisimua....

SAFARI YA MAJIBU JUU YA MASWALI MAWILI.

 

Basi mambo yaka wa hivyohivyo, siku ile wakaniweka kwenye ngozi ya kondoo na kubebwa na roki. Alikwenda kunituwa juu ya mlima na nikatumia kisu na kutoka yule ndege akakimbia. Nikafata ile njia niloambiwa mpaka nikakuta nyumba kubwa sana. Kwa hakika nyumba ilikuwa ni nzuri sana na ni kubwa. Ilikuwa ina vyumba zaidi ya 100. ilikuwa ina vitu vingi vya kuvutia na mabostani ya matunda na miti.

 

Nyumba hii ilikuwa imetulia sana yaani utadahani haina hata mtu mmoja japo utashangazwa kwa usafi wa nyumba hii. Nilianza kuhesabu vymba mpaka nikafika chumba cha 35, na humo nikasikia sauti za wanawake. Nilibisha hodi na kukaribishwa kwa furaha. Nilipewa chakula na malazi, vinywaji na furaha nyingine.

 

Nilikaa pale kwa muda wa siku 5 nikiwa ninabadilishiwa furaha mpa ya mambo mapya kila siku. Huenda hata ningeishi siku 1000 ningepata mabo mapya kila siku. Kwa hakika nyumba hii ilikuwa na kila kitu nilichokisikia na kila uzuri. Niliendelea kukaa pale hata ilipofika mwezi 3 kambla ya kumalizika kwa mwaka kwa siku 10.

 

Siku ile wale wanawake wakaniita na mkubwa wao akaanza kuongea “mgeni wetu, tunapenda sana kuishi na wewe hapa kuwa muda zaidi lakini hatunabudi ya kutengana kwa muda wa sili 100. sisi ni watoto wa wafalme na huwa kila mwisho wa mwaka tunarudi makwetu kwa ajili ya mabo ya kifamilia. Hivyo hatunabudi kutengana nawe ila tutakuacha hapa. Tunakuachia funguo hizi za vyumba 100 humo utafutahia vitu ambavyo hujapata kuviona kwa muda wote uloishi hapa. Ila vyumba vyote fungua isipokuwa cha 100. kama tutakutana baada ya siki hizo tutafurahi sana na tusipokutana usisahau kutuombea dua.”

 

Kwa majonzi niliagana nao sikuile na wakaondoka. Basi nikaanza kufurahia mambo mazuri yaliyomo pale ndani. Nikawa kwa kialsiku Snafunguwa chumba kimoja. Ikawa kila chumba nikuta mambo mazuri ambayo chumba nilichofungua jana hakina. Kwahakika nilifurahia sana harufu nzuri ya mawaidi mule ndani. Sauti nzuri za kupendeza za ndege, chemchem za maji na asali iliyohifadhiwa. Vyakula vya kila namna na vikalio vya kuvutia.

 

Nilifanya hivyo mapaka pale nilipomaliza vyote vyumba 99 kwa siku 99 na kubakia chumba kimoja na siki moja mpaka kurudi wale wenyeji wangu. Sikuile ya 100 ilipofika nikawa sina hamu ya kurudia vyumba vya nyuma hivyo nikataka kufungua kile cha 100. nikaenda kwenye mlango na kuanza kupiga mahesabu ya kufungua. Nilianza kuoiga ramli ya vigole kwa kufumba macho lakni matokea yakawa nisifungue, basi nikaamua niondoke pale mlangoni.

 

Nilizunguruka mule ndani na nikajikuta narudi tena chumba cha 100. mara hii nilikuja na jani nikawa napiga ramli ya majani lakini matokeo yaka wa nisifungue. Dukuduku lilianza kuniumiza kwa nini chumba cha 100. mna nini hasa humu mpaka nisifungue. Basi nikaichukua ile funguo na kufungua kidogo ili nichingulie. Nilipofungua ghafla ilikuja harufu nzuri ya ajabu na hapohapo nikapoteza fahamu.

 

Nilipokuja kuzindukka nikafungua ili nijue kuna nini na ni wapi harupu ile ya kuvutia ilipotokea. Basi nilipofungua tu nikajikuta nipo nje, kumbe kile hakikuwa ni chumbaila ni mlango wa kutokea kwenye bostani. Nilipofika mule nikaona kuna ndege wanaoimba nyinyo nzuri, matunda ambayo sijayaona na mauwa yanayotoa harufu njema ya kuvutia. Maji ya chemchem yenye rangi ya dhahabu na ni ya moto. Halikadhalika vivuli vyenye mumbo

 

Kwa hakika katika bostani lile kulikuwa na mabo mengi na ya kuvutia sana. Cha ajabu zaidi niliona kuna farasi mwenye mabawa na mkia mrefu wa kuvutia wenye mashapupo yanayofanana na miba ya nungunungu. Nilitamani sana kumpanda farasi yule. Nilimsogelea na kutafuta fimbo ya kumuendeshea na nikaiona. Polepoe nikampanda na kuanza kumuendesa mrembo farasi.

 

Farasi yule ghafla akaanza kupaa hata kabla sijakua namna ya kumpaisha, alipofika umbali kadhaa akaanza kunifiga na mashaputo ya mkia wake ulio mrefu. Mashaputo yale yakanipata kwenye jicho langu la kulia na kunitoboa. Nilianguka chini ghafla na kupoteza fahamu. Nilipokuja kushitua nikajikuta nipo karibu na mlima na lile jumba sikuliona tena na hata ile njia sikuiona tena.

 

Basi nikarudi kwa wale wenzangu machongo tukawa tupo chongo11. wale wakanambia siwezi tena kukaa na wao maana wamesha enea. Hivyo yule mkubwa wao akanimalizia majibua ya maswali yangu kuwa sababu ya wao kujitandika na mikwaju ni adhabu ya kuvunja amri ya kutoufungua mlango wa 100. hivyo wakaniambia niende baghadi huko nitakutana nae ali anipangie adhabu yangu.

 

Baada ya hapo nikanyoa nyusi zangu na nywele zangu na kuelekea baghdad na nilipofika hapa nikakutana na wenzangu hawa watatu na usiku ulipotufikia tuakaamua kuomba hifadha hapa kwenu. Hivyo hii ndio stori yangu ewe dada Zubeida.

 

Zubeida alipomaliza kusikiliza stori ya chongo huyu akamuelekea chongowa tatu na kumwambia aeleze stori yake bila ya kuficha kitu na vinginevyo atakufa. Chongo wa tatu akaanza kuelezea kuwa na yeye ni mtotowa mfalme na amepata chongo si kwa sababu ya ubishi wake bali ni qadar tu na hivi ndibyo mambo yalivyokuwa;-





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Mankaa Tarehe 2024-09-09 14:15:06 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Masomo File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 36


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Bostani la kifalme baghadad
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 8 Part 1: Hadithi ya tunda
Simulizi hii pia inapatikana kwenye kitabu cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 13: Wageni wa Baraka kujongea
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 2 Part 2: Hadithi ya mzee wa kwanza na mbuzi wake
Simulizi za HALIF LELA U LELA zipo nyingi sana na husikiliwa na kusomwa na wakubwa kwa wadogo pia hadithi hizi zimeenea duniani Kate zikisikilizwa na maelfu ya watu mbalimbali. Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 19: Mfalme na waziri wake
Hadithi hii inapatikana katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 11: Vidole gumba vilikatwa
Kitabu cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA kina simulizi nyingi nzuri na za kusisimua, muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 7 Part 7: Upendo uliotafsiriwa
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 3 Part 4: Kisa cha waziri aliyeadhibiwa
Simulizii hii inapatikana katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 20: Waliodhulumiwa kufanyiwa suluhisho
Ni mojawapo ya simulizi iliyopo kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Nudhini na mtumwa
Muendelezo....... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Nudhini akiwa hatiani
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 7 Part 10: Jumba la Aladini
Muendelezo..... Soma Zaidi...