image

Flutter somo la 14: Jinsi ya kuweka picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu widget ya Image ambayo hutumika kuonyesha picha kwenye App.

Kuna aina mbili za kuweka picha kwenye App ya flutter. Kwanza ni picha ya offline, picha hii unaiweka kwenye app yako kama mafaili mengineyo. Njia ya pili ni kuweka picha ambayo ipo online hivyo tunatumia link ya picha hiyo kwenye App yetu.

 

Property za Image:

1. image: (property hii ni lazima kuwepo) Inabainisha picha itakayotolewa. Unaweza kutumia aina ya ImageProvider kama vile AssetImage, NetworkImage, au FileImage kama chanzo cha picha.

 

2.width: Inabainisha upana wa picha. Unaweza kutoa thamani ya double kuweka upana wa picha kwa pikseli za mantiki.

 

3.height: Inabainisha urefu wa picha. Unaweza kutoa thamani ya double kuweka urefu wa picha kwa pikseli za mantiki.

 

4.fit: Inadhibiti jinsi picha itakavyoingizwa ndani ya nafasi yake. Thamani zinazowezekana ni:

 

5.BoxFit.contain: Inapanua picha ili kuingiliana na chombo huku ikidumisha uwiano wake wa asili.

BoxFit.cover: Inapanua picha ili kufunika kontena lote, ikikata ikiwa ni lazima.

BoxFit.fill: Inayeyusha picha ili kujaza kontena lote, ikivuruga uwiano wake wa asili.

BoxFit.fitWidth: Inapanua picha ili ifanane na upana wa kontena huku ikidumisha uwiano wake wa asili.

BoxFit.fitHeight: Inapanua picha ili ifanane na urefu wa kontena huku ikidumisha uwiano wake wa asili.

BoxFit.none: Haina mabadiliko yoyote kwenye ukubwa wa picha.

 

6.alignment: Inabainisha usawazishaji wa picha ndani ya nafasi yake. Thamani inapaswa kuwa ya aina ya Alignment na inaweka picha ndani ya chombo.

 

7.color: Inatumia kichujio cha rangi kwa picha.

 

8.colorBlendMode:  Inabainisha jinsi rangi iliyowekwa na property ya color itakavyochanganywa na picha.

 

9.repeat:  Inabainisha jinsi picha itakavyorudi ikiwa haijaijaza nafasi yake kikamilifu.

 

Jinsi ya kuweka Picha:

Sasa ili tuweke picha tutatumia ImageProvider ambazo nimezitaja kwenye property ya image. Ambazo ni asset na network

 

  1. Kwa kutumia AssetImage

Kwa kutumia jia hii utaweza kutumia faili ambalo utaliweka kwenye app yako. Hivyo kwanza utafuata njia hizi:-

  1. Kwanza ingia kwenye folder la project yako. Folda lenyewe ambalo kuna mafaili mengine kama pubspec.yaml
  2. Utatengeneza folda hapo lipe jina la assets. Unaweza kuweka jina lolote unalotaka. Ndani ya foler hili tengeneza folda linguine liite images pia unawez akuweka jina unalolitaka wewe. Sasa ndani ya folda la images hapo weka picha zako unazotaka zionekane.
  3. Hatuwa inayofuata nenda kwenye faili linaloitwa pubspec.yaml  kisha tafuta mstari ulioandikwa flutter: na hakuna mwingine wenye jina hilo kuelekea chini. Maana mistari yenye flutter ipo mingi ila tafuta ambazo ni wa mwisho. Kisha weka code hizi

assets:

 - assets/images/

Weka kama unavyoziona hapo kwa mtiririko huohuo. Code hizi zinasajili folda letu la assets ambalo lina folda la picha. Baada ya hapo sasa tutakuwa tayari kuweza kutumia picha yetu kwenye App.kuna  worning unaweza kuziona kwenye faili la main.dart. Bofya hizo warning kupata maelekezo zaidi.

 

Sasa ili tuweze kutumia picha tutatumia widget ya picha ikifuatiwa na image provider. Mfano

Image.asset("images/bongo.png")

 

Code nzima hizi hapa

import 'package:flutter/material.dart';

 

void main() => runApp(MyApp());

 

class MyApp extends StatelessWidget {

 @override

 Widget build(BuildContext context) {

   return MaterialApp(

     home: Scaffold(

       appBar: AppBar(

         title: Text("image assets"),

...



           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2024-02-28 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 283


Download our Apps
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Flutter somo la 14: Jinsi ya kuweka picha
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu widget ya Image ambayo hutumika kuonyesha picha kwenye App. Soma Zaidi...

FLUTTER somo la 2: Jinsi ya kutengeneza App ya flutter
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutengeneza App yako ya kwanza ya Flutter hatuwa kwa hatuwa. Soma Zaidi...

Flutter somo la 11: Matumizi ya text widget
Katika Flutter, Text Widget ni kipengele kinachotumiwa kuonyesha maandishi kwenye programu. Kwa kawaida, hutumiwa kama sehemu ya muundo wa UI ya programu za Flutter. Soma Zaidi...

Flutter somo la 7: jinsi ya kutumia Widget ya AppBar
Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu widget ya AppBar. Hata tutaona inavyofanya kazi na baadhi ya property zake. Soma Zaidi...

Flutter: Somo la 3: Mambo muhimu kuhusu App ya flutter
Katika somo hili tutakwend akuyaona baadhi ya maeneo muhimu ya kuanzia kuyajuwa kwa ajili ya course ya flutter kwneye android studio. Soma Zaidi...

Flutter somo la 12: widget ya padding
Katika somo hili utakweda kujifunza jinsi ya kutumia widget ya padding kwenye App yako. Soma Zaidi...

Flutter somo la 6: Scaffold widget, kazi zake na property zake
Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu scaffold widget. Hapa tutakwend kuona properties zake na baadhi ya mifano. Soma Zaidi...

Flutter somo la 15: Jinsi ya kuweka icon kwenye App ya flutter
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia icon yaani kuweka icon kwenye App ya flutter. Soma Zaidi...

Flutter somo la 9: Jinsi ya kutumia widget ya Row
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu row widget. Hii ni widget ambayo ina utofauti na column widget kwa kuwa hii yenyewe inapangilia maudhui kwa safu za mlalo, tofauti na iliyopita inapangilia kwa safu za wima. Soma Zaidi...

Flutter somo la 1: Nini flutter na nini hasa inafanya
Katika somo hili utajifunza historia fupi ya flutter, kazi zake, nini hasa inafanya. pia utajifunza jinsi ya ku install flutter Soma Zaidi...

Flutter somo la 8: Jinsi ya kutumia widget ya column
Katika somo hili utakweda kujifunza kuhsu widget ya column. Widget hii ni moja katika widget zilizo muhimu sana kuzifaham. Soma Zaidi...

Flutter: somo la 4: Jinsi ya kuandika code za App ya flutter, hatuwa kwa hatuwa
Katika somo hili utakwenda kujifunza sasa jinsi ya kuandika code za app yetu kwenye flutter framework. Soma Zaidi...