picha

Milki ya raslimali katika uislamu

Milki ya RasilimaliIli kujipatia maendeleo ya kiuchumi katika zama zote mwanaadamu anahitaji rasilimali za kumwezesha kufikia azma hiyo.

Milki ya raslimali katika uislamu

Milki ya Rasilimali
Ili kujipatia maendeleo ya kiuchumi katika zama zote mwanaadamu anahitaji rasilimali za kumwezesha kufikia azma hiyo. Miongoni mwa rasilimali kuu (natural re-sources) ni zile zinazohusiana na ardhi, maji na wanyama. Kwa mujibu wa Uislamu rasilimali hizo ni neema za Allah (s.w).


“Na katika ardhi mna vipande vinavyoungana (na kuzaa kwake namna mbali mbali) na mna mabustani ya mizabibu, na mimea mingine, na mitende ichipuayo katika shina moja na isiyochipua katika shina moja. Vyote vinavyonyweshelezwa (vinamiminiw a) maji yale yale; na tunavifanya bora baadhi yake vyengine katika kula (katika utamu). Hakika katika haya zimo ishara kwa watu w anaotia mambo akilini”. (13:4)


(b) Rasilimali za maji na mvua

“… Na unaiona ardhi imetulia kimya lakini anapoyateremsha maji juu yake, inataharaki na kukuwa na kuotesha kila namna ya mimea mizuri.” (22:5)

“Je! Huoni kwamba Mwenyezi Mungu ameteremsha maji kutoka maw inguni. Kisha akayapitisha (chini kwa chini) yakawa chemchem katika ardhi, tena akaotesha kwayo mimea ya rangi mbali mbali (na sura mbali mbali)…” (39:21).

(c)Rasilimali za bahari na samaki

“Mwenyezi Mungu ndiye aliyekutiishieni bahari ili humo zipite merikebu kwa amri yake, na ili mtafute fadhila yake na mpate kushukuru ”. (45:12)

“Na yeye ndiye aliyeitiisha bahari ili humo mule daima kitoweo kipya (samaki) na mtoe humo mapambo mnayoyavaa. Na utaona merikebu zikipasua humo, ili mtafute fadhila zake (kwa kufanya biashara) na ili mpate kushukuru.” (16:14)


(d)Rasilimali za wanyama

“Na (pia) amewaumba wanyama. Katika hao mnapata (vifaa vitiavyo) joto na manufaa; na wengine mnawala(16:5).


Na mnaona raha mnapowarudisha jioni na mnapow apeleka malishoni asubuhi.(1 6:6)

Na (wanyama hao pia) hubeba mizigo yenu kupeleka katika m iji msiyoweza kuifikia isipokuwa kwa mashaka na taabu. Hakika Mola wenu ni Mpole sana (na) Mwenye rehema nyingi”.(16:7)

Na (amewaumba) farasi na nyumbu na punda ili muwapande na (wawe) mapambo. Na ataumba (vipando vyingine) msivyovijua ”. (16:8).


(e) Rasilimali za madini
Muhutasari wa aya hizo juu ya rasilimali unapatikana katika aya ifuatayo:

“Yeye ndiye aliyekuumbieni vyote vilivyomo katika ardhi.” (2:29).



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF Views 1170

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 ai web app     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Kwa nini waislamu wanaoa mke zaidi ya mmoja

Post hiibitakugundisha hekima ya kuruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja katika sheria za kiislamu.

Soma Zaidi...
Riba na Madhara Yake Katika Jamii

- Riba ni kipato chochote kile cha ziada kutokana na mkopo au mtaji bila kushiriki katika faida au hasara.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa funga ya ramadhan

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Namna ya kutayamamu hatuwa kwa hatuwa

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi yavkutayamamu.

Soma Zaidi...