Milki ya raslimali katika uislamu
Milki ya RasilimaliIli kujipatia maendeleo ya kiuchumi katika zama zote mwanaadamu anahitaji rasilimali za kumwezesha kufikia azma hiyo.
Milki ya Rasilimali
Ili kujipatia maendeleo ya kiuchumi katika zama zote mwanaadamu anahitaji rasilimali za kumwezesha kufikia azma hiyo. Miongoni mwa rasilimali kuu (natural re-sources) ni zile zinazohusiana na ardhi, maji na wanyama. Kwa mujibu wa Uislamu rasilimali hizo ni neema za Allah (s.w).
“Na katika ardhi mna vipande vinavyoungana (na kuzaa kwake namna mbali mbali) na mna mabustani ya mizabibu, na mimea mingine, na mitende ichipuayo katika shina moja na isiyochipua katika shina moja. Vyote vinavyonyweshelezwa (vinamiminiw a) maji yale yale; na tunavifanya bora baadhi yake vyengine katika kula (katika utamu). Hakika katika haya zimo ishara kwa watu w anaotia mambo akilini”. (13:4)
(b) Rasilimali za maji na mvua
“… Na unaiona ardhi imetulia kimya lakini anapoyateremsha maji juu yake, inataharaki na kukuwa na kuotesha kila namna ya mimea mizuri.” (22:5)
“Je! Huoni kwamba Mwenyezi Mungu ameteremsha maji kutoka maw inguni. Kisha akayapitisha (chini kwa chini) yakawa chemchem katika ardhi, tena akaotesha kwayo mimea ya rangi mbali mbali (na sura mbali mbali)…” (39:21).
(c)Rasilimali za bahari na samaki
“Mwenyezi Mungu ndiye aliyekutiishieni bahari ili humo zipite merikebu kwa amri yake, na ili mtafute fadhila yake na mpate kushukuru ”. (45:12)
“Na yeye ndiye aliyeitiisha bahari ili humo mule daima kitoweo kipya (samaki) na mtoe humo mapambo mnayoyavaa. Na utaona merikebu zikipasua humo, ili mtafute fadhila zake (kwa kufanya biashara) na ili mpate kushukuru.” (16:14)
(d)Rasilimali za wanyama
“Na (pia) amewaumba wanyama. Katika hao mnapata (vifaa vitiavyo) joto na manufaa; na wengine mnawala(16:5).
Na mnaona raha mnapowarudisha jioni na mnapow apeleka malishoni asubuhi.(1 6:6)
Na (wanyama hao pia) hubeba mizigo yenu kupeleka katika m iji msiyoweza kuifikia isipokuwa kwa mashaka na taabu. Hakika Mola wenu ni Mpole sana (na) Mwenye rehema nyingi”.(16:7)
Na (amewaumba) farasi na nyumbu na punda ili muwapande na (wawe) mapambo. Na ataumba (vipando vyingine) msivyovijua ”. (16:8).
(e) Rasilimali za madini
Muhutasari wa aya hizo juu ya rasilimali unapatikana katika aya ifuatayo:
“Yeye ndiye aliyekuumbieni vyote vilivyomo katika ardhi.” (2:29).
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Swala ya kuomba mvua swalat istiqaa na jinsi ya kuiswali.
Hapa nitakujulisha kuhusu swala ya kuomba mvia, na taratibu za kuiswali.
Soma Zaidi...Njia za kudhibiti riba
Ufumbuzi wa tatizo la ribaRiba imeenea na kuzoeleka duniani kwa kiasi ambacho watu wengi wanadhani kuwa bila riba hakuna shughuli yoyote ya uchumi inayowezekana.
Soma Zaidi...Hatua za kinga za ugumba na Utasa.
Ugumba ni “ugonjwa wa mfumo wa uzazi unaofafanuliwa kwa kushindwa kupata ujauzito baada ya miezi 12 au zaidi ya kujamiiana bila kinga mara kwa mara. Utasa kutoweza kwa kiumbe hai kufanya uzazi wa ngono au kutoweza kupata mimba au kuchangia mimba.
Soma Zaidi...Ni ipi hukumu ya muislamu anayekula mwezi wa Ramadhani bila ya sababu ya kisheria
Endapo muislamu hatafunga mwezi wa Ramadhani bila ya ruhusa je atatakiwa afanye nini. Je ataweza kuilipa funga hiyo?
Soma Zaidi...