Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za Kirumi hapo zamani

(b) WarumiJamii ya Warumi nayo ni miongoni mwa jamii zinazohesabika kuwa zilianza kustaarabika mapema katika historia ya ulimwengu.

Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za Kirumi hapo zamani

(b) Warumi
Jamii ya Warumi nayo ni miongoni mwa jamii zinazohesabika kuwa zilianza kustaarabika mapema katika historia ya ulimwengu. Je jamii hii ilimpa mwanamke heshima na hadhi anayostahiki? Katika historia ya Urumi tunajifunza kuwa Warumi walimwona mwanamke kama mtoto anayetakiwa kuangaliwa na kukemewa. Akiolewa yeye na mali yake ni mali ya mume. Akikosea, mume alikuwa na mamlaka ya kupitisha hukumu yoyote.aliyoweza hata ya kutoa adhabu ya kifo.



Mwanamke alikatazwa kushiriki katika jambo lolote. Hakuruhusiwa kutoa ushahidi wala kumuwekea mtu dhamana. Mumewe akifariki, Shemeji zake walikuwa na haki ya kumrithi.



Hapo awali katika historia ya Urumi, wanawake walibakia nyumbani na ukahaba (umalaya) haukujulikana. Mtu kufanya kitendo cha mapenzi na mkewe kama vile kumbusu mkewe hadharani ilionekana ni kitendo kiovu na utovu wa adabu na heshima. Kiongozi mmoja wa Kirumi alishutumiwa vibaya na raia wake kwa kitendo cha kumbusu mkewe mbele ya binti yake.



Warumi waliposongambele katika maendeleo ya kijamii, waliona wamkomboe mwanamke kwa kulegeza sharia ya ndoa kiasi cha kuifanya kama mkataba wa wawili wanaopendana. Wanawake walipewa haki ya kurithi na walikuwa huru na mamlaka ya baba au mume. Katika wakati huu sio tu kuwa wanawake wa Kirumi walijitegemea kiuchumi bali walikuwa wakiwakopesha waume zao kwa nba kubwa kwa kiasi kwamba Wanaume ambao wake zao walikuwa matajiri walijikuta wamekuwa watumwa wao.
Kutaliki kulikuwa jambo jepesi na ndoa zilikatika bila ya sababu za msingi.


Kwa mfano Seneca (4B.C - 65 A.D), Mwanfalsafa Mashuhuri wa Kirumi alitoa shutuma kwa watu wake kutokana na kiwango cha talaka kilicho kithini katika jamii yake kwa kusema: "Now divorce is not regarded as something shameful in Rome. Woman calculate their age by the number of husbands they have taken."



Tafsiri:
"Talaka sasa hainonekani kuwa nijambo la aibu hapa Urumi. Wanawake wanahesabu umri wao kwa idadi ya Wanaume waliofunga nao ndoa."



Yaani, wanawake wa Kirumi katika wakati huo wa historia, kwa uhuru waliopewa na jamii waliweza kuolewa na wanaume wengi kwa muda mfupi. Kwa mfano Martial (43 A.D - 104 A.D) ameeleza juu ya mwanamke aliyeolewa na wanaume kumi. Juvenal (60 A.D - 130 A.D) ameandika juu ya mwanamke aliyeolewa na wanaume wanane, mmoja baada ya mwingine, katika kipindi cha miaka 8. St. Jerome (340 A.D - 420 A.D) ameeleza juu ya mwanamke wa ajabu ambaye mume wake wa mwisho alikuwa wa 23, mmoja baada ya mwingine. Yeye mwenyewe kwa mumewe huyo wa mwisho alikuwa ni mke wake wa 21. ni katika wakati huu uzinifu ulianza kustawi na wazinifu hawakuhesabiwa kuwa ni wakosaji wanaostahiki kuadhibiwa.



Katika historia hii fupi, tunajifunza jisni mwanamke alivyokandamizwa na jamii hapo awali na tumeona hali ya mwanamke ilivyokuwa baada ya kukombolewa. Je, ukombozi huu ulimpa mwanamke hadhi yake anayostahiki?




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1134

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Taratibu za kutaliki katika uislamu.

Hapa utajifunza taratibu zinazofuatwa wakati wa kukusudia kumuacha mke. Pia utajifunza sababu za kiwepo kwa eda baada ya kuachwa mwanamke.

Soma Zaidi...
Haki ya kumiliki mali na mipaka yake katika uislamu

Je unaijuwa mipaka yako katika kumiliki mali. Ama unajuwa haki zako katika mali inayomiliki. Endelea na somo

Soma Zaidi...
Sifa za imamu wa swala ya jamaa

Post hii inakwenda kukupa sifa za imamu wa msikitini anayepasa kuswalisha swala ya jamii.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kutoa zakat al fitiri na umuhimu wa zakat al fitri kwa waislamu

Hapa utajifunza kuhusu zakat al fitiri, kiwango chake, watu wanaostahili kupewa na kutoa, pia umuhimu wake katika jamii.

Soma Zaidi...
Nini maana ya ndoa katia uislamu na ni upi umuhimu wake

Hapa utajifunza maana ya ndoa kulingana na uislamu na umuhimu wake katika jamiii

Soma Zaidi...
Historia ya adhana na Iqama na jinsi ya kuadhini.

Hadithi hii inakwenda kukufundisha historia fupi ya adhana pia utakwenda kujifunza jinsi ya kuadhini na kuqimu.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa swala yaani kuswali kwa mwanadamu

Kwa nini ni muhimu kuswali? Post hii itakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kusimamisha swala.

Soma Zaidi...